Kuchagua kuondoka au kukaa katika jiji lililoshambuliwa la Bakhmut

Iliyochapishwa

Mwili wake ulilala mahali alipoanguka, peke yake, ghorofa mgongoni mwake, chini ya jua hafifu la Septemba.

Aliuawa mwendo wa saa sita mchana tarehe 24 Septemba wakati wa saa kadhaa za mashambulizi makali katika mji wa Bakhmut katika mkoa wa Donbas mashariki mwa Ukraine.

Tulimpata kwa bahati, na tukajua baadaye jina lake kuwa ni Andriy Yablonsky, na alikuwa na miaka 52.

Mwanamke aliyevaa koti jekundu alipiga kelele kwa uchungu karibu na hapo, alikuwa amejificha mlangoni. Huyu alikuwa dada yake Andriy. "Nifanye nini kaka yangu?" Yeye aliomboleza.

Kwa zaidi ya saa moja hakuweza hata kusogezwa kwa sababu hakukuwa na hali ya unafuu dhidi ya milio ya risasi na makombora.

Maisha ya Andriy yalitumika kuokoa wengine. Alifanya kazi kama dereva wa gari la wagonjwa na aliuawa karibu na bohari yake mwili wake ulitobolewa na vipande vya mabomu.

Jina lake sasa limeongezwa kwenye orodha ya waathirika wa Urusi huko Bakhmut.

Zaidi ya raia 70 wameuawa kwa kushambuliwa kwa makombora na maadui katika miezi ya hivi karibuni, kulingana na gavana wa eneo hilo Pavlo Kyrylenko.L

Inawezekana tulisikia bomu lililomuua Andriy.

Kwa saa nyingi asubuhi hiyo katikati ya jiji, kulisikika mwangwi wa ving'ora na mlio wa wa makombora kutoka kwa vikosi vya Urusi, na kishindo cha risasi zinazotoka kutoka kwa Waukraine.

Mapigano ya silaha yalikuwa yakicheza karibu nasi, majibizano ya haraka sana ilikuwa vigumu kufuatilia. "Ni kama mchezo wa badminton," mfanyakazi mwenza wa Ukraine alisema.

Raia kumi na wawili wakiwa wamejibanza kwenye ukuta, wakiteleza na kupepesuka, huku mlipuko mmoja ukifuata mwingine, mali zao muhimu ziliwekwa kwenye mabegi ya kusafiria miguuni mwao. Walikuwa wakisubiri timu ya kuwahamisha ya mtu mmoja ili kuwatoa nje ya jiji.

Kabla ya uvamizi wa Warusi mnamo Februari, Bakhmut ilikuwa nyumbani kwa watu wapatao 70,000, na ilijulikana kwa migodi yake ya chumvi na uzalishaji mzuri wa mvinyo.

Sasa umepigwa, na kwa kiasi kikubwa hauna uhai.

Iryna mwenye umri wa miaka 48 aliyevalia koti la njano linalong'aa alimtazama kwa woga binti yake Yelizeveta mwenye umri wa miaka 14 ambaye alikuwa amejifunika kofia ya koti lake.

Mama na binti huyo wakati fulani walikuwa wakiogopa na kuchukua hatua za haraka kuondoka kutokana na sauti za vita. Vinginevyo, kijana alijishughulisha na kutoa huduma kwa wanyama wa majumbani

Kuondoka kwa Iryna huku akisita kutoka katika mji wake ilikuwa kwa ajili ya mtoto wake.

"Ni ngumu sana," aliniambia, "ngumu sana. Nisingependa kuondoka mahali hapa isipokuwa kwasababu ya vita. Jambo kuu ni kuokoa maisha ya binti yangu. Pia tunachukua paka wetu, ili sote tuokoke."

Na je ataweza kurudi siku nyingine?

"Nataka kurudi Bakhmut," alijibu. "Vikosi vyetu vya kijeshi vitarudisha maeneo na kila kitu kitakuwa sawa." Taarifa hii ni sala na makala ya imani kwa wengi nchini Ukrainia.

Zaidi ya miezi sita baada ya uvamizi huo, lengo lililotajwa la Urusi lililorudiwa hivi karibuni na Rais Putin ni kupata udhibiti wa Donbas yote. Na Bakhmut ni kikwazo.

Vikosi vya Urusi vinaweza kutumia ushindi hapa baada ya kushindwa kwao hivi karibuni maeneo ya kaskazini-mashariki mwa Ukraine.

Kwa sasa, wanajeshi wa Ukraine wanawazuia katika ukingo wa mashariki wa mji huu wa kimkakati.

Hata hivyo makabiliano ya Bakhmut yanaweza kumalizika, Iryna na Yelizeveta wana wasiwasi hivi karibuni zaidi - wanaendelea kuishi hadi mwisho wa siku.

Wanakusanya vitu vyao kwa haraka na kugonga nyuma ya gari, likiendeshwa na mfanyakazi wa kujitolea anayeitwa Serhiy Ivanov.

Mwanaume wa miaka 39 - ambaye huvaa kofia na miwani - alikuwa mpiga ngoma katika bendi ya rock. Siku hizi ni sehemu ya mtandao unaoitwa 'Rescue Now'.

Tatoo iliyoandikwa Kilatini kwenye mkono wake wa kulia inasomeka "carpe diem", au "kamata siku". Kwa miezi kadhaa sasa amekuwa akifanya hivyo, akiwachukua raia kutoka kwenye njia ya hatari katika maeneo ya mstari wa mbele.

Anapunguza hatari ya maisha yake kwenye misheni hizi za kila siku. "Nadhani ni kawaida kwangu," anasema "na kawaida kwa raia yeyote wa Ukraine.

Ninahisi furaha ninapoona tabasamu kwenye nyuso hizi. Ninapenda maisha, napenda Ukraine na ninawapenda watu."

Baada ya hayo, anaondoka kwa mwendo wa kasi kwenye barabara zenye mashimo.

Kwa Iryna na binti yake ni hatua ya kwanza ya safari ya kuelekea sehemu salama kwa jamaa wa mji mkuu, Kyiv.

Wengine huchagua kubaki katika jiji hili, wafungwa wa umri na kumbukumbu kama Lidiya mwenye umri wa miaka 80 ambaye tulikutana naye katika mji huo.

Ukatili wa kivita unammuangalia usoni. Nyumba yake ya kawaida ni mkabala na jumba la ghorofa tano lililoharibiwa na shambulio la anga la Urusi tarehe 15 Septemba.

Raia watano waliuawa katika shambulio hilo, kulingana na watoa huduma za dharura.

Walipokuwa wakipekua kwenye vifusi siku iliyofuata mmoja wa timu yao aliuawa kwa kupigwa makombora.

Lidiya anakaa kwenye benchi mbele ya nyumba yake, ameinamia juu ya fimbo yake machozi yake yanakuja haraka mara tunapoanza kuongea.

Anamuomboleza Volodymyr, mume wake wa miaka 60 ambaye alifariki hivi majuzi kutokana na ugonjwa, na amani waliyokuwa wakifurahia.

"Kwa miaka 70, hapakuwa na vita yoyote. Kwa nini walianza? Wanapigania nini? Nataka kulia mchana na usiku, "ananiambia. "Naomba mume wangu anichukue. Watoto wangu wamehamishwa. Maisha yao yameharibika pia. Na watoto wadogo wamehamishwa. Wanatutesa, 100%.

Lidiya anarejelea pande zote mbili, "Utakuwaje msimu huu wa baridi," anapumua. "Hakuna gesi, katika nyumba baridi. Ningefurahi ikiwa tu wangeacha kupiga makombora."

Tulipoondoka Bakhmut, moshi ulikuwa bado ukiongezeka baada ya shambulio la anga la Urusi siku chache mapema kwenye jengo lingine la ghorofa. Kulikuwa na majivu yanayofuka kwenye kifusi.

Katika azma yake ya kuutwaa mji huo, Urusi inaonekana iko tayari kuuangamiza.

Ni muundo ambao umeonekana katika miji mingine iliyoharibiwa na kubaki magofu Ukraine. Makombora, kuua, na kurudia ndio njia ya jeshi la Urusi.