Upigaji wa kura mapema ulifanyika katika majimbo mengi nchini Marekani na kufikia sasa inakadiriwa kwamba Wamarekani 46 milioni tayari wamepiga kura.
Ingawa kura hizi zitahesabiwa baada ya vituo kufungwa Jumanne, baadhi ya majimbo huta takwimu na maelezo kuhusu waliopiga kura kwa mfano kuhusu idadi ya waliopiga kura na iwapo wamejiandikisha kuwa wa chama cha Republican au Democratic.
Jimbo la Nevada, kwa mfano, tunajua kwamba karibu watu 800,000 walipiga kura kabla ya kufungwa kwa upigaji wa kura za mapema tarehe 4 Novemba.
Asilimia 42 walikuwa wanachama wa Democratic na 36% wanachama wa Republican. Takwimu hizo hazina tofauti kubwa na hali 2012, ambapo Barack Obama aliongoza kwa 6.7%.