Trump: Nitachunguza kabla ya kukubali matokeo
Katika mahojiano na kituo kimoja cha Runinga ,Donald Trump amesema kuwa ''atachunguza vile mambo yanavyoelekea'' kabla ya kukubali matokeo.
Aliambia kituo cha runinga ya Fox News kwamba amesikia kuhusu visa vya dosari katika upigaji kura,ijapokuwa hakutoa maelezo zaidi.
Wakati wa kampeni bwana Trump alidai kwamba uchaguzi ulikuwa unakabiliwa na udanganyifu na akasema kwamba atapinga matokeo ambayo yana dosari.