Trump ndiye mshindi Florida
ABC News wametangaza kwamba makadirio yao yanaonyesha Trump ameshinda jimbo muhimu la Florida.Sasa Trump ana kura 222 za wajumbe na Clinton 197 za wajumbe. Mshindi anahitaji kura 270.
Jimbo hilo huwa muhimu sana kwa mgombea yeyote.
Jimbo hilo lilimpigia Obama mwaka 2008 na 2012 (Democratic), lakini George W Bush (Republican) alishinda uchaguzi uliotangulia 2000 na 2004. Jambo la kushangaza ni kuwa alikuwa mbele na kura 537 pekee mwaka 2000.
Hata hivyo, ilichukua siku 36 kwake kuthibitishwa kuwa mshindi, kwa hivyo iwapo wagombea watakaribiana sana usitarajie matokeo yatangazwe haraka.