Vita Ukraine: Picha zimeonesha jinsi meli ya Urusi ya Moskva inavyozama baada ya kushambuliwa na Ukraine

Iliyochapishwa

Picha - na video za kuaminika - za meli ya kivita ya Urusi Moskva zilionekana mtandaoni kabla ya kuzama wiki iliyopita.

Video na picha hizo zinaonesha meli hiyo ikiwa inafanana na muundo wa kombora.

Urusi inasema moto uliotokea kwenye boti ulisababisha risasi kulipuka na meli hiyo kuzama ilipokuwa inapambana na dhoruba wakati Ukraine inasema iliipiga kwa makombora.

Picha mpya haziashirii moja kwa moja madai ya pande zote mbili - lakini hakuna dalili ya dhoruba wakati huo.

Je, video na picha zinaonesha nini?

Picha hizo zinadaiwa kupigwa tarehe 14 April, siku moja baada ya Ukraine kudai kuwa iliilipua meli ya kivita.

Kipande cha video cha sekunde tatu - ambacho kinawezekana kilichukuliwa kutoka katika boti ya uokoaji - kinaonesha meli ya Moskva kwa mbali ikiwa imelemewa upande wa mizigo.

Meli hiyo ya Urusi ikiwa imegemea upande wake wa kulia.

Moshi unaonekana ukifuka kwenye meli, huku sehemu ya mbao ikionesha ikiwa imeharibika sana.

Mashimo pia yanaonekana katika sehemu zingine za ubao kwenye picha moja, ikionesha kuwa meli ya kivita ilikuwa imeingia maji mengi.

Pia inaonekana boti zote za kuokoa meli za uokoaji zilikuwa hazipo.

Kuna maelezo zaidi juu ya chanzo cha meli hiyo kuzama?

Ukraine inasema ilifanikiwa kuishambulia Moskva kwa makombora mawili ya Neptune yaliyotengenezwa hivi karibuni na Ukraine Jumatano iliyopita.

Maafisa wa Marekani ambao hawakutajwa majina wameviambia vyombo vya habari vya Marekani kwamba wanaamini kuwa ni kazi ya Ukraine.

Urusi inadai kuwa iliharibiwa baada ya mlipuko na baadaye kuzama kwa sababu ya "bahari yenye dhoruba".

BBC ilionesha kanda hiyo kwa wataalam watatu wa jeshi la majini ambao walikubali uharibifu huo ulionekana kuambatana na shambulio la kombora, lakini hawakukubaliana ikiwa sababu zingine bado zinawezekana kusababisha meli hiyo kuzama.

Jonathan Bentham, wa Taasisi ya Kimataifa ya Mafunzo ya Kimkakati, alihitimisha kwamba meli kwenye picha hakika ilikuwa ya Slava-class na "pengine" Moskva.

Bw Bentham alisema uharibifu unaoonekana katika meli hiyo ni kana kwamba ulisababishwa na shambulio la kombora la Neptune, lakini alisisitiza kuwa haiwezekani kuondoa sababu zingine katika hatua hii.

"Ishara ya moshi kwenye eneo lake la mizigo zinaonekana kuwa karibu na njia ya maji. Hiyo inaweza kuashiria makombora ya kuteleza baharini, ambayo makombora ya Neptune yanaripotiwa kuepo," Bw Bentham alisema.

Mafuta kuvuja

Mtaalamu mwingine, Chris Parry, ambaye hapo awali aliongoza maangamizi ya Jeshi la Wanamaji wa Kifalme, aliiambia BBC kwamba alikuwa na uhakika kwamba uharibifu huo ulisababishwa na shambulio la kombora.

"Unaweza kuona upande wa meli iliyokwama sana," Parry alisema. "Iwapo ungekuwa mlipuko wa ndani, ungeona mchoro ukining'inia nje badala ya ndani. Lakini hii inaonekana kupenya na mlipuko uliofuata. Bila shaka imepigwa na kombora moja au mawili."

Kamanda huyo wa zamani wa Nato alisema sababu moja ya uharibifu mkubwa uliosababisha moshi ni kwamba makombora yaliyokuwa yamehifadhiwa ndani ya meli yalisababisha mafuta kuvuja kwenye meli, na hivyo kusababisha moto kuwaka.

"Unaweza kuona , meli nzima inaonekana imeteketea. Nadhani mafuta yanaweza kuwa chanjo," alieleza.

Mlipuko wa Risasi

Mtaalamu mwingine wa kijeshi, Sidharth Kaushal wa Taasisi ya Royal United Services, aliiambia BBC kwamba eneo kuu la uharibifu wa moto ni "ambapo kuna risasi za bunduki za ndege za anga ".

"Dhana moja inayofanya kazi ni kwamba moto ulioanzishwa na shambulio la awali uliondoa risasi kutoka kwa bunduki za ndege," Kaushal alisema.

Hali ya bahari

Ingawa hali zinaweza kutofautiana kwa nyakati tofauti, hakuna chochote kwenye video kuthibitisha madai ya awali ya Kremlin kwamba Moskva ilizama kutokana na hali ya dhoruba.

Kabla ya kuzama, wizara ya ulinzi ya Urusi ilitoa taarifa ikisema "meli hiyo imeharibika vibaya. Wafanyakazi wote wameokolewa".

BBC haijaweza kuthibitisha madai hayo.

Urusi pia haijakubali kuwa majeruhi yoyote au vifo. Siku ya Jumamosi, wizara ya ulinzi ya Urusi ilichapisha picha zinazoonesha kile kilichoeleza kama wafanyakazi wa Moskva wakiwa katika mji wa bandari ya Crimea ya Sevastopol.

Meli hiyo ya kivita ya wafanyakazi 510 ilikuwa imeongoza mashambulizi ya wanamaji ya Urusi dhidi ya Ukraine, ambayo yaliifanya kuwa shabaha muhimu ya kiishara na kijeshi.

Hapo awali katika mzozo huo, Moskva ilipata sifa mbaya baada ya kuwaita wanajeshi wa mpaka wa Ukraine wanaotetea Kisiwa cha Snake katika Black sea kujisalimisha - ambapo kwa kumbukumbu walitangaza ujumbe wa kukataa ambao unatafsiri kwa urahisi kama "kwenda kuzimu".

Unaweza pia kusoma