Matokeo ni batili - Odinga azungumza kwa mara ya kwanza tangu kutangazwa ameshindwa
Mshindi wa pili katika uchaguzi wa urais nchini Kenya amezungumza na kusema “Takwimu zilizotangazwa na Bw Chebukati ni batili na ni lazima zifutiliwe mbali na mahakama.
Moja kwa moja
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Shangwe makao makuu ya chama cha William Ruto jijini Nairobi, ambapo watu wamevamia densi baada ya ushindi wake katika uchaguzi.
Ruto aipongeza Tume ya uchaguzi na kuahidi 'serikali yenye uwazi'
Maelezo ya picha, William Ruto- Rais Mteul Kenya
Ruto aipongeza Tume ya uchaguzi na kuahidi 'serikali
yenye uwazi'
William Ruto amehutubia taifa baada ya kutangazwa
mshindi.
"Watu wa Kenya wameonyesha kutuamini, sio kwa sera
za makabila yetu, bali kwa kile tulichokuwa tunakizungumzia."
Pia amepongeza mchakato wa uchaguzi, licha ya kwamba
mapema kidogo kundi la makamishna walisema hawakuweza kushiriki katika utoaji
wa matokeo.
"IEBC ambayo ni tume ya uchaguzi ilitushangaza sote…ninataka
kupongeza IEBC kwa kuongeza uaminifu wa viwango vingine.
"Wafula Chebukati ambaye ni mwenyekiti wa tume ya
uchaguzi ndiye shujaa wetu."
Ruto aahidi 'serikali yenye uwazi'
Alipokuwa anazungumza, Bw. Ruto amesema anafahamu kuwa
anakabiliwa na wapinzani wengi baada ya kupata zaidi kidogo tu ya asilimia 50
ya kura.
"Nitaendesha serikali ya uwazi, na ya
kidemokrasia," amesema.
"Ninataka kuwaahidi watu wote wa Kenya, kwa njia
yoyote waliyopiga kura kwamba hii itakuwa serikali yao.
"Nataka kuwaambia wapinzani kwamba hawana chochote
cha kuogopa, hakuna nafasi ya kulipiza kisasi. Ninafahamu kabisa kwamba nchi
yetu ipo katika hatua ambayo tunahitaji juhudi za pamoja ili kusonga mbele.’’
"Hatuna haja ya kuangalia nyuma. Hatuna haja ya kunyoosheana
vidole. Hatuna tamaa wala haja ya kutupiana lawama. Ni lazima tushirikiane kwa
ajili ya Kenya inayofanya kazi, ya kidemokrasia na yenye ustawi."
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 1
Rais wa Zimbambwe Emmerson Mnangagwa amempongeza William
Ruto kwa kuchaguliwa kuwa Rais ajaye wa tano wa Kenya.
Katika ujumbe wake kwenye mtandao wa Twitter:
Hongera William Ruto kwa kuchaguliwa kuwa Rais ajaye wa
Kenya.
Sina shaka ataitumikia nchi yake, watu wake na bara letu
kwa upekee.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 2
Waziri wa
kwanza azungumza
Waziri wa
Utalii wa Kenya Najib Balala amekuwa waziri wa kwanza katika baraza la mawaziri
kumpongeza William Ruto.
Balala
amekuwa miongoni mwa mawaziri ambao hawakumfanyia kampeni waziwazi mgombea wa
Rais Uhuru Kenyatta Raila Odinga.
Wakati wa
kampeni yake, Bw Ruto aliwashtumu mawaziri waliokuwa wakihudhuria kampeni za
mpinzani wake kwa kuingiza baraza la mawaziri kisiasa kinyume na sheria
inayowazuia watumishi wa umma kujihusisha na siasa.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 3
Habari za hivi punde, Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Ruto anazungumza baada ya kutangazwa mshindi
Chanzo cha picha, William Ruto/ FACEBOOK
Maelezo ya picha, William Ruto- Rais mteule Kenya
Ruto
anazungumza baada ya kutangazwa mshindi
William Ruto
baada ya kutangazwa kuwa mshindi, sasa anazungumza:
‘’Ni jioni nzuri sana... mamlaka yote ni ya watu wa
Kenya. Nataka kumshukuru
Mungu kwa kutufikisha hapa.
‘’Najua
kulikuwa na utabiri kwamba hatungefika hapa - lakini kwa sababu kuna Mungu
mbinguni, tuko hapa. Shukrani nyingi ziende kwa watu wa Kenya.’’
Habari za hivi punde, Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Vurugu zaibuka katika kituo cha kutolea matokeo
Kufuatia tangazo
la makamishna wanne wa uchaguzi kwamba hawawezi kushiriki katika kutangaza
matokeo, kumekuwa na matukio ya fujo katika kituo cha matokeo.
Ilionekana kuwa
msaidizi wa Raila Odinga alijaribu kumzuia mkuu wa tume ya uchaguzi kutoa
hotuba. Kisha polisi mmoja akamsimamisha na kumpeleka eneo lililo mbali na jukwaa.
Habari za hivi punde, Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Tume Huru ya uchaguzi ya Kenya (IEBC) yagawanyika
Maelezo ya picha, Baadhi ya Makamishna wa Tume Huru ya uchaguzi Kenya
Makamishna
wanne wa Tume Huru ya uchaguzi ya Kenya(IEBC) wamefanya mkutano na waandishi wa
habari wakisema ‘’hawawezi kumiliki matokeo’’ kwa sababu ya ‘’hali isiyoeleweka
ya jinsi awamu hii imekuwa ikishughulikiwa’’.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022:Timu ya Raila inasema imeshindwa kuthibitisha matokeo ya mwisho
Chanzo cha picha, Citizen
Maelezo ya picha, Ajenti mkuu wa uchaguzi wa Raila Odinga Saitabao Kanchory akizungumza na vyombo vya habari
Wakala mkuu wa uchaguzi wa Raila Odinga Saitabao Kanchory
amesema timu yake haijaweza kuthibitisha baadhi ya matokeo na hivyo basi
haitamtaka mgombea wao wa urais kufika katika kituo cha kujumlisha matokeo.
Katika maelezo mafupi ambayo yaliwasilishwa kwa
watangazaji wa ndani, aligusia baadhi ya dosari za uchaguzi.
Bw Kanchory alikuwa ameandamana na baadhi ya viongozi
kutoka muungano wa Bw Odinga wa Azimio, Gavana wa Kisumu Anyang Nyong'o na
Gavana Mteule wa Siaya James Orengo.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Raila Odinga yuko wapi?
Wakenya kwenye mitandao ya kijamii wanashangaa alipo
Raila Odinga, kabla ya kutangazwa kwa rais mteule.
Bado hajafika katika kituo cha kitaifa cha kuhesabu kura
kama ilivyo kwa mpinzani wake mkuu William Ruto.
Kulikuwa na shamrashamra fupi wakati msafara wa magari
uliposimama katika kituo cha matokeo, lakini ikafahamika kwamba alikua mama
yake Ruto.
Walinzi nje ya ofisi ya Bw Odinga katika kitongoji cha
Karen jijini Nairobi wamemweleza mwandishi wa BBC Mercy Juma kwamba mgombea
huyo bado yumo ndani ya eneo hilo.
Timu za waandishi wa habari zimekita kambi kwenye kizuizi
karibu na ofisi yake.
Kuna uvumi kwamba huenda Odinga asifike katika kituo cha
kujumlisha kura kipindi hiki.
Hata hivyo, hakuna sharti kwamba wagombea wote wawepo kwenye
eneo la utangazaji wa matokeo na Odinga hakuwepo katika eneo hilo la
ujumlishaji wa matokeo wakati alipowania urais mara nne.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Foleni ndefu zashuhudiwa kwenye barabara kadhaa
Foleni ndefu
zimeshuhudiwa katika barabara mbalimbali kwenye mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
Vyombo vya
habari vya ndani na Wakenya kwenye mtandao wa Twitter wanaripoti msongamano wa
magari katika sehemu za jiji hilo.
Huku
Jumatatu ikiwa siku ya kazi, wakati wa mchana Wakenya wengi wamejipata wakiwa
katika harakati za kukimbilia kwenda majumbani mwao mapema, wengine wakiwa na
wanafunga biashara zao, huku raia wengine wakiwa wanakimbilia kununua bidhaa.
Kuna
msongamano wa magari kwenye barabara kuu mbili za Nairobi.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Ukraine yashambulia makao makuu ya mamluki ya Wagner Urusi mashariki
Chanzo cha picha, AFP
Maelezo ya picha, Popasna ipo karibu na Severodonetsk (kama inavyoonekana kwenye picha) - sasa iko mikononi mwa Warusi baada ya mapigano makali
Ndege za
kijeshi za Ukraine zimeshambulia makao makuu ya kundi la jeshi la mamluki la Wagner
mashariki mwa Ukraine, ripoti zinasema.
Shambulio hilo
la Popasna liliripotiwa na Serhiy Hayday, Gavana wa Ukraine wa mkoa wa Luhansk,
na waandishi kadhaa wanaoripoti kuhusu mambo ya vita wanaounga mkono Kremlin.
Idadi ya
waliopoteza maisha bado haijulikani na maelezo yanabaki kuwa ya mchoro.
Picha
zinazosemekana kuonesha uharibifu ziliwekwa kwenye mtandao wa Telegram.
Kundi la Wagner limekuwa likihusishwa na uhalifu wa kivita.
Kundi hilo
lilitumwa Crimea na eneo la Donbas nchini Ukraine mwaka 2014, wakati wanajeshi
wanaoungwa mkono na Kremlin walipowatimua wanajeshi wa Ukraine katika maeneo
ambayo baadaye walitangaza kuwa sehemu ya Urusi.
Vikosi vya
Wagner pia vimetumwa Syria, Libya, Mali na Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Kremlin
haikubali kuwepo kwa kundi la Wagner, lakini ujasusi wa Magharibi unahusisha
kundi hilo na Yevgeny Prigozhin - jina la utani ‘’mpishi wa Putin’’ kwa sababu
biashara yake ya upishi imemsaidia kwa muda mrefu Rais Vladimir Putin na vikosi
vya jeshi.
Bw
Prigozhin, kama maafisa wengine wengi wa Urusi, yuko chini ya vikwazo vya
Magharibi.
Kundi la Wagner
linajulikana kama PMC - kampuni binafsi ya kijeshi.
Lakini ni
mamluki wanaofadhiliwa na serikali ambao wanafanya kazi kwa maslahi ya Kremlin,
wataalamu wa Magharibi wanasema.
Wameshutumiwa kwa uhalifu wa mara kwa mara wa kivita na
ukiukaji wa haki za binadamu.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Matokeo yanavyoweza kuwa
Maelezo ya picha, Ukumbi wa IEBC
Tunapoendelea
kusubiri matokeo,nikukumbushe tu kwamba
kuna matokeo matatu yanayoweza kutokea baada ya kura ya Jumanne iliyopita:
• William
Ruto atangazwe kuwa mshindi
• Raila
Odinga atangazwe kuwa mshindi
• Uchaguzi uingie
katika duru ya pili ya uchaguzi
Duru ya pili
ya uchaguzi itatangazwa ikiwa hakuna hata mmoja kati ya wagombea aliyepata kura
zaidi ya 50% ya kura - hii inawezekana kwa kuwa kuna wagombea wengine wawili
wanaowania urais, ingawa kwa pamoja wameonesha kupata chini ya 1% ya kura.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Tume ya uwiano inawataka Wakenya kudumisha amani
Tume ya uwiano nchini Kenya imewataka Wakenya kudumisha
amani wakati na baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais.
Tume ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano (NCIC) imewataka
Wakenya wote “kukubali matokeo na kuruhusu masuala yoyote yatakayojitokeza
kushughulikiwa na mahakama zetu”.
‘’Tangazo hili muhimu litatoa mwelekeo wa mustakabali wa
nchi yetu lakini sio hali ya kufa na kupona. Kenya itasonga mbele kwa mafanikio bila kujali nani ni
rais kwa hivyo watu wetu hawana haja ya kuwa na wasiwasi,’’ anasema mwenyekiti
wa NCIC Samuel Kobia.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
NCIC
ilianzishwa kufuatia ghasia zilizofuatia uchaguzi wa mwaka 2007 ambapo watu
wasiopungua 1,200 waliuawa na 600,000 kukimbia makazi yao baada ya madai ya
kuibiwa kwa kura.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Matokeo kutangazwa saa mbili zijazo
Maelezo ya picha, Tangazo la IEBC
Maandalizi yanaendelea
kupamba moto kwa ajili ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi.
Watu ndani
ya kituo kikuu cha kutangazwa kwa matokeo wamekuwa wakifurahia kwaya zinazoendelea
tumbuiza - lakini burudani hii italazimika kuendelea kwa saa mbili zaidi.
Tume ya
uchaguzi imesema kwamba matokeo ya mwisho yatatoka saa 15:00 kwa saa za ndani
(12:00 GMT).
Matokeo ya Uchaguzi Kenya: Wagombea wa uchaguzi Wajakoyah na Mwaure wawasili katika ukumbi wa Bomas
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, David Mwaura na George Wajackoyah wamekuwa wakipata kura chache zaidi katika matokeo ya awali ya uchaguzi wa urais
Wagombea wa urais George Wajackoyah wa chama cha Roots na David Mwaure wa chama cha Agano Party wamewasili katika ukumbi wa Bomas, inakofanyika shughuli ya kujumlisha kura, huku rais mteule akitarajiwa kutangazwa rasmi
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
Wawili hao wamekuwa wakipata idadi ya chini ya kura katika matokeo ya awali tya urais ambayo yamekuwa yakitangazwa na vyombo vya habari - wakiwa na chini ya 1% ya kura kila mmoja
Bw Mwaure alikubali kushindwa Jumapili na kumuidhinisha Naibu Rais William Ruto.
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Wakenya wasubiri kutangazwa kwa Rais Mteule
Maelezo ya picha, Ukumbe wa Bomas of Kenya, umeshuhudia vikundi vya kwaya za kidini ambazo zimekuwa zikitumbuiza Wakenya huku wakisubiri matokeo ya uchaguzi mkuu
Tume ya uchaguzi
na mipaka nchini Kenya(IEBC), imekamilisha mchakato wa uhakiki wa kura za urais
Macho yote sasa
ni kwa Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati wakimsubiri atangaze matokeo.
Wakati hayo yakijiri
viongozi wa vyama vyote vya kisiasa walio katika ukumbi wa Bomas ambao ndio kituo kikuu cha kujumlisha kura wameonekana wakicheza nyimbo za dini, zinazotumbuizwa na kwaya katika ukumbi huo .
Tume ya uchaguzi inatarajiwa kumtangaza rais mteule leo. Tume hiyo ina siku hadi saba za kutangaza matokeo baada ya uchaguzi kufanyika. Uchaguzi mkuu
wa Kenya ulifanyika Jumanne wiki
iliyopita tarehe 9 Agosti.
Iwapo mshindi wa urais atatangazwa
leo,na iwapo hapatakuwa na pingamizi ya ushindi wake mshindi anafaa kuapishwa tarehe 30 mwezi huu wa Agosti.
Unaweza pia kusoma:
Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022:Kenya huenda ikamjua rais ajaye leo-IEBC itamtangaza Raila Odinga ama William Ruto?
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Raila Odinga na William Ruto katika ushindani mkali
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Waliokuwa vigogo na kutupwa nje kwa muda wachaguliwa tena
Matokeo ya Uchaguzi Kenya:Picha katika ukumbi wa Bomas,Kisumu na Eldoret
Kabla ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais nchini Kenya ,baadhi ya wakazi katika maeneo ya Kisumu na Eldoret wamefurika barabarani kuanza kusherehekea huku wakitaka mshindi kutangazwa.Katika Picha:
Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Fatuma Achani gavana pekee wa kike pwani ya Kenya
Maelezo kuhusu taarifa
Author, Aboubakar Famau
Nafasi, BBC News, Mombasa
Chanzo cha picha, Fatuma Achani/Facebook
“Haikuwa
kazi rahisi, nilinyanyaswa nilitukanwa na watoto wangu, ilikuwa sio siasa tena,
lakini ni mashambulizi dhidi yangu”
Vikundi
vya ngoma za kienyeji vilikuwa kila pembe ya kaunti ya Kwale, huku wengine
wakitanda nje ya uzio wa jengo ambalo Tume Huru ya Uchaguzi ilikuwa ikiendesha
shughuli zake.
Sherehe
zilizokuwa zikiendelea ilikuwa ni furaha ya ushindi wa kiti cha gavana wa
Kwale, ambacho mara hii kimekwenda kwa Fatuma Achani, mwanamke pekee aliyeibuka
kidedea katika nafasi hiyo Pwani ya Kenya.
Achani,
mwenye miaka 38, anasema ingawa alikuwa naibu gavana katika serikali iliyopita,
lakini kampeni ya kutaka nafasi ya gavana haikuwa kazi rahisi.
“Nilitukanwa,
nilidhalilisha mitandaoni pamoja na watoto wangu, haikuwa siasa tena, ilikuwa
ni mashambulio binafsi,” anasema Achani.
Achani
anaongeza kusema kuwa, kwa sababu yeye ni mwanamke katika jamii ambayo
haijazoea kuongozwa na wanawake, yeye aliongeza juhudi kuliko wapinzani wake wa
kiume, ili kuthibitisha uwezo wake wa kazi.
Wakiwa
wamebeba bango lenye picha ya Achani, mmoja wa wafuasi wake alisema,
“Tunafuraha kupata ushindi. Tuna matumaini mama atatuwakilisha vizuri.”
Wanawake kadhaa wameingia katika kinyang’anyiro cha nafasi ya gavana katika eneo la Pwani, lakini ni Achani pekee ndie aliyeweza kuwafuta machozi wenzake walioshindwa. Mpaka sasa kuna magavana saba wanawake walioshinda katika maeneo mengine kati ya 47 nchi nzima.
Safari inaonekana bado ndefu kwa kina mama hawa, ambao licha ya kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika siasa, lakini bado wana kazi kubwa ili kujihakikishia ushindi.
Unaweza pia kusoma:
Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022:Kenya huenda ikamjua rais ajaye leo-IEBC itamtangaza Raila Odinga ama William Ruto?
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Raila Odinga na William Ruto katika ushindani mkali
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Waliokuwa vigogo na kutupwa nje kwa muda wachaguliwa tena
Matokeo ya uchaguzi 2022:Maafisa Zaidi wa polisi waingia katika ukumbi wa Bomas
Maelezo ya picha, Katika ukumbi wa IEBC, maafisa wa usalama wanaonekana kuimarisha ulinzi
Usalama umeimarishwa ndani na nje ya ukumbi wa
Bomas unaotumiwa kama kituo cha kitaifa cha kujumlisha kura za urais .
Jumatatu asubuhi
maafisa zaidi wa polisi waliingizwa katika ukumbi huo ili kuimarisha usalama
huku tume ya Uchaguzi na mipaka IEBC ikitarajiwa kumtangaza mshindi wa uchaguzi
wa urais hii leo .
Maelezo ya picha, Ukumbi wa IEBC
Shughuli katika
ukumbi huo zimeendelea kwa utulivu baada ya visa kadhaa vya makabiliano hapo
awali kati ya maajenti wa miungano ya Kenya kwanza na Azimio wakati mchakato wa
kuhakiki kura ukiendelea.
Wakati huo huo madawati yote ya uhakiki wa matokeo ya kura yamebaki matupu, eneo la wanadiplomasia linakaliwa na watu wengine kinyume na siku za nyuma wakati yamekuwa wazi.
Unaweza pia kusoma:
Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022:Kenya huenda ikamjua rais ajaye leo-IEBC itamtangaza Raila Odinga ama William Ruto?
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Raila Odinga na William Ruto katika ushindani mkali
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Waliokuwa vigogo na kutupwa nje kwa muda wachaguliwa tena
Vikosi vya Burkina Faso vimeshutumiwa kwa mauaji ya raia 40
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, Jeshi la Burkina Faso ilikanusha shutuma za ukiukaji wa haki za binadamu
Makundi ya kutetea haki za binadamu nchini Burkina Faso yamelishutumu jeshi kwa kuwauwa
zaidi ya watu 40 kaskazini mwa nchi.
Shirika hilo la Collective Against Immunity and
Stigmatisation of Communities limesema
kumekuwa na visa vingi vya utekaji nyara na kufuatiwa na mauaji ya watu kunyongwa kiholela
Ilisema
miili ya wahasiriwa ilipatikana kwenye barabara kati ya Taffogo na Bouroum
ikiwa imefungwa macho na mikono .
Kundi
jingine la kutetea haki za binadamu, Observatory of Human Dignity, lilisema
wengi wa wahasiriwa walikuwa Wafulani - kabila lenye Waislamu wengi wa wafugaji
wanaohamahama.
Jeshi la
Burkina Faso limekanusha madai ya mara kwa mara ya ukiukaji wa haki.
Kisa
hicho kinasemekana kutendeka mapema mwezi huu katika kijiji cha Taffogo huko
Tougouri.
Jeshi la
Burkina Faso limekuwa likipambana na uasi wa makundi yanayoshukiwa kuwa na
uhusiano na al-Qaeda au kundi la Islamic State, ambao umesababisha vifo vya
zaidi ya watu 2,000 na kuwalazimu
takriban watu milioni 1.9 kuondoka makwao.
Urusi yaapa kuimarisha uhusiano na Korea Kaskazini
Chanzo cha picha, Getty Images
Urusi imeapa "kuimarisha
uhusiano [wake] wa kina na wa kujiboresha " na Korea Kaskazini, amesema Rais
wake Vladimir Putin.
Katika barua
iliyotumwa kwa mwenzake Kim Jong un siku ya ukombozi wa Pyongyang, Bw Putin
alisema hatua hiyo itakuwa kwa maslahi ya nchi zote mbili.
Kwa upande wake,
Bw Kim alisema urafiki kati ya mataifa yote mawili ulianza katika Vita vya Pili
vya Dunia na ushindi dhidi ya Japan.Aliongeza kuwa "uhusiano wao wa
kirafiki" utaimarika zaidi.
Kulingana na
ripoti ya chombo cha habari cha serikali ya Korea Kaskazini KCNA, Bw. Putin
alisema uhusiano huo uliyoimarishwa "utaendana na maslahi ya nchi hizo
mbili."
Katika barua
yake, Bw Kim alisema urafiki wa Russia na Korea Kaskazini "ulioanzishwa
katika vita dhidi ya Japan" "umeimarishwa na kuendelezwa karne baada
ya karne" .
Iliongeza "ushirikiano
wa kimkakati na wa kimbinu, uungaji mkono na mshikamano" kati ya nchi hizo
mbili "umewekwa kwenye hatua mpya ya juu, katika mstari wa pamoja kwa
ajili ya kukatisha tamaa tishio la kijeshi la vikosi vya uhasama na
uchochezi".
Pyongyang
haikutambua majeshi hayo kwa majina, lakini neno hilo limetumiwa mara kwa mara
na Korea Kaskazini kurejelea Marekani na washirika wake.
Umoja wa
Kisovyeti ulikuwa mshirika mkuu wa Korea Kaskazini, ukitoa ushirikiano wa
kiuchumi, mabadilishano ya kitamaduni na misaada.