Matokeo ni batili - Odinga azungumza kwa mara ya kwanza tangu kutangazwa ameshindwa
Mshindi wa pili katika uchaguzi wa urais nchini Kenya amezungumza na kusema “Takwimu zilizotangazwa na Bw Chebukati ni batili na ni lazima zifutiliwe mbali na mahakama.
Moja kwa moja
Ukraine yatangaza shambulio kubwa dhidi ya kambi ya wanajeshi wa Urusi
Vikosi vya
Wanajeshi vya Ukraine viliharibu kambi ya wanajeshi wa Urusi huko Nova
Kakhovka, mkoa wa Kherson, kulingana na huduma ya vyombo vya habari ya Vikosi
vya Wanajeshi wa Ukraine na huduma ya mpaka wa serikali.
Video
inayoonyesha athari ya shambulio la kombora imeibuka mtandaoni.
Upande wa Ukraine
unakadiria mauaji ya kati ya 10-15 wa Urusi.
BBC hatahivyo haiwezi
kuthibitisha kwa haraka habari katika hali ya mapigano.
Na kufikia hapo ndio tunakamilisha matangazo yetu kwa hii leo.
Kuna ukweli kuhusu madai ya makosa ya hesabu ya matokeo ya uchaguzi?
Maelezo kuhusu taarifa
Author, Peter Mwai
Nafasi, BBC Reality Check
Makamishna wanne wa tume ya uchaguzi waliojitenga na matokeo
ya uchaguzi yaliyotangazwa hapo jana Jumamatu wamedai kwamba matokeo hayo sio
sahihi kwasababu Jumla ya asilimia iliyotolewa inapita asilimia 100.
Ni madai ambayo yamewekwa mitandaoni na wafuasi wa kiongozi
wa upinzani Raila Amollo Odinga.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
Asilimia 100.10% inaweza kuelezewa kupitia hesabu.
Kwasababu ya kukadiria juu au chini wakati unapopiga hesabu za kila asilimia mpaka nafasi mbili za desimali, uwezekano wa kupata chini au zaidi ya 100% hutokea.
Unaweza tu kupata asilimia halisi ya 100% unapofanyia kazi sehemu zote za desimali.
Kulingana na matokeo yaliyotangazwa na mwenyekiti wa IEBC, mshindi William Ruto alipata 50.49% ya kura, Odinga (48.85%), George Wajackoyah (0.44%) na Mwaure Waihiga (0.23%).Jumla ni 100.01%.
Nambari zote zimekadiriwa hadi nafasi mbili za desimali na 0.01% ya ziada inaonekana kwa sababu nambari ya desimali kabla ya kukadiriwa ilikuwa tano au zaidi.
Makamishna hao hao pia walitoa madai yasiyo ya kweli kuwa 0.01% ya jumla ya kura halali zilizopigwa zingewakilisha kura 142,000 na kusema "italeta mabadiliko makubwa katika matokeo."Hatahivyo, idadi sahihi itakuwa kura 1,420.
Hata hivyo kuna tofauti ya kura 110 kati ya jumla ya kura halali zilizotangazwa na mwenyekiti, 14,213,137, na jumla ya kura zilizopatikana na wagombea wote wanne.
Soma zaidi:
Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Raila Odinga apinga matokeo ya uchaguzi
Makamishna wa Tume ya Uchaguzi waliojitenga na matokeo wazungumza
Je wafuasi wa Rais Mteule wa Kenya wana hofia ushindi wake kupingwa mahakamani?
Je wafuasi
wa Rais Mteule wa Kenya wana hofia ushindi wake kupingwa mahakamani?
Tazama video hii...
Maelezo ya video, Je wafuasi wa Rais Mteule wa Kenya wana hofia ushindi wake kupingwa mahakamani?
Rais wa Kenya akaa kimya baada ya kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi mkuu
Chanzo cha picha, Getty Images
Maelezo ya picha, Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta
Ni wiki moja
sasa tangu Wakenya walipomuona ama kumsikia Rais Uhuru Kenyatta.
Alizungumza
kwa ufupi na wanahabari Jumanne iliyopita baada ya kupiga kura katika mji
aliozaliwa nje kidogo ya mji mkuu, Nairobi.
Alikuwa
anamuunga mkono aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga kuchukua nafasi yake badala
ya naibu wake, William Ruto, ambaye alitangazwa mshindi wa uchaguzi wa Agosti
9.
Wawili hao
walipochukua madaraka mwaka wa 2013 walikuwa na uhusiano wa karibu, kila mara
wakiitana “kaka”, wakipiga makofi hadharani baada ya kutaniana na wakati
mwingine kuwa na mahusiano ya karibu sana.
Haijulikani
kwanini walikosana, lakini uhusiano wao ulizidi kuwa mbaya na kuzorota kuelekea
siku za kuelekea uchaguzi wa mwaka huu ambapo walirushiana maneno makali.
Licha ya Bw
Kenyatta kutokuonekana hadharani, serikali yake ilitangaza leo kwamba mchakato
wa kumpata Rais mpya bado unaendelea.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Matokeo ni batili - Odinga azungumza na kumshutumu Chebukati kwa uonevu
Chanzo cha picha, AFP/Getty
Maelezo ya picha, Raila Odinga amehutubia taifa
Raila Odinga
amehutubia taifa baada ya kushindwa katika uchaguzi
Mgombea wa
pili wa Urais Raila Odinga, ambaye muungano wake wa Azimio La Umjoa unadai kulikuwa
wizi wa kura katika matokeo ya Jumatatu, amezungumza hadharani kwa mara ya
kwanza tangu kushindwa kwake.
Akihutubia
taifa kutoka Makao Makuu ya vyombo vya habari vya Azimio jijini Nairobi,
anasema: “Mamilioni ya Wakenya walijitokeza kwa wingi kuchagua viongozi wao... Lakini
jana demokrasia yetu ilikabiliwa na msukosuko mkubwa.’’
Raila Odinga amshutumu Chebukati kwa uonevu
‘’Kwa kuepuka shaka, nataka kurudia: Tunakataa kabisa na bila kusita matokeo ya urais yaliyotangazwa jana na [Mwenyekiti wa tume Huru ya uchaguzi] Bw Chebukati,’’ Bw Odinga asema.
Pia anamshutumu mwenyekiti wa uchaguzi kwa kuwadhulumu wanachama wengine wa Tume hiyo ambao hawakukubaliana naye.
Kenya yawahakikishia raia usalama na kuwataka kurejelea shughuli za kibiashara
Maelezo ya picha, Kitengo cha juu cha usalama nchini Kenya chazungumza
Kitengo cha
juu cha usalama nchini Kenya kimewahakikishia raia usalama kufuatia hofu ya kuwepo
kwa ghasia zinazohusiana na uchaguzi.
Mamlaka
imewataka Wakenya kuanza tena shughuli zao za kibiashara wakisema nchi iko
salama na usalama umeimarishwa katika kipindi hiki.
Wingu la
wasiwasi limetanda nchini kufuatia machafuko yaliyotangulia baada ya kutangazwa
kwa matokeo ya urais Jumatatu.
Kamati ya
ushauri ya usalama wa taifa nchini imechukua hatua ya kuondoa hofu ya kutokea
ghasia kufuatia mzozo wa matokeo ya uchaguzi wa Rais.
Timu hiyo
ilisema hali ya usalama nchini iko shwari baada ya tathmini ya awali mapema
Jumanne na mamlaka imechukua hatua kuhakikisha nchi iko salama.
Kulikuwa na
ripoti za ghasia katika maeneo ya mji mkuu Nairobi na katika mji wa Kisumu
magharibi mwa Kenya baada ya waandamanaji kupinga kuthibitishwa kwa William
Ruto kama mshindi wa uchaguzi wa Agosti 9.
Chaguzi za
urais zilizoshindaniwa hapo awali zimesababisha ghasia zilizogharimu maisha ya
watu wengi na uharibifu wa mali.
Viongozi kadhaa kutoka ngome ya Raila wasihi wafuasi wao kudumisha amani
Chanzo cha picha, Gavana wa Kisumu Anyang Nyongo ?TWITTER
Maelezo ya picha, Gavana wa Kisumu Anyang Nyongo
Gavana wa Kisumu Anyang Nyong'o amewataka wakaazi wa Kisumu kusitisha maandamano
yao yanayoendelea na kusalia kwa amani huku uongozi wa Azimio ukitoa mwanya wa
kusonga mbele.
Nyong'o
kupitia taarifa iliyotolewa Jumanne asubuhi aliwaambia wakazi hao kusalia na
amani hata iwapo tangazo la William Ruto kuwa Rais mteule litapingwa.
“Tafadhali
sitisha aina yoyote ya maandamano na uharibifu wa mali tunapojiandaa
kuwajulisha hatua inayofuata,” alihimiza.
Nyong'o
aliendelea kuwaomba wakaazi hao kuwa na imani na uongozi wa Azimio
wanapojitahidi kuhakikisha mgombea wao anapata haki.
Wakati huo huo, Gavana
mteule wa eneo la Homa Bay Mheshimiwa Gladys Wanga, ametoa taarifa akishirikisha
wafuasi wa eneo lake uchungu na kukatishwa kwa matumaini ambako pamoja na wafuasi
wa Muungano wanapitia kwa sasa.
Bi Wanga amewahakikishia wafuasi kwamba timu
yao ya sheria inashughulikia kile kilichotokea kwa madai kwamba makosa
yaliyotokea ikiwa ni pamoja na ukiukwaji wa kanuni za uchaguzi.
Pia
amewataka wakazi kuwa watulizu, kumuunga mkono Raila Odinga na kumuombea.
Aidha, aliwahakikishia
wafuasi wa Raila kwamba timu ya wanasheria ya Azimio la Umoja itafanya yote
wanayoweza ili kuhakikisha mshindi sahihi wa uchaguzi anatangazwa.
‘’Zoezi hilo
lilikuwa na dosari kubwa na kuthibitishwa na makamishna wanne ambao ndio wengi
wa tume ya IEBC. Kwa hivyo suala hili halijaisha,’’ Gladys Wanga ameandika.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Raila Odinga kuvunja ukimya mchana wa leo baada ya kushindwa katika uchaguzi wa urais
Chanzo cha picha, AFP
Maelezo ya picha, Kuna uvumi kwamba huenda akapinga matokeo mahakamani (picha kutoka maktaba)
Mshindi wa
pili katika uchaguzi wa urais nchini Kenya anatazamiwa kuzungumza hadharani kwa
mara ya kwanza tangu kushindwa kwake katika uchaguzi wa urais uliofanyika
Jumatatu.
Imetangazwa
kuwa Raila Odinga atahutubia wanahabari saa 14:00 saa za eneo (11:00 GMT).
Hii ilikuwa
mara ya tano kwa mzee huyo mwenye umri wa miaka 77 kugombea nafasi hiyo ya juu
na wengi wanadhani itakuwa mwisho wake.
Salim Lone,
aliyekuwa mshauri wa Bw Odinga, aliambia BBC Jumanne kwamba bosi wake wa zamani
alifananisha mchakato mzima na ‘’ubakaji wa demokrasia’’.
Kabla ya Bw
Ruto kutangazwa na mkuu wa tume ya uchaguzi kuwa mshindi Jumatatu kwa asilimia
50.49 ya kura, maajenti wa uchaguzi wa Bw Odinga walikuwa wamesema hawakuweza
kuthibitisha matokeo.
Pia yalitiliwa
shaka na makamishna wanne kati ya saba wa uchaguzi, ambao waliambia waandishi
wa habari hawakuweza ‘’kuchukua umiliki wa matokeo’’.
Kundi la waangalizi wa uchaguzi wa Kenya ELOG lasema matokeo ya IEBC yanaendana na yake
Kundi la waangalizi wa uchaguzi wa Kenya ELOG limesema matokeo ya uchaguzi wa Rais yaliyotangazwa Jumatatu na mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Wafula Chebukati yanaendana na hesabu walizofanya kundi hilo,zilizoonesha ushindi wa Bwana William Ruto na kuyataja matokeo hayo kuwa ya wazi.
Matokeo huru yaliyofanywa na kundi hilo la waangalizi yalimuweka William Ruto mbele kwa asilimia 50.7, ilhali matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi nchini Kenya IEBC yalionesha Bwana Ruto alishinda kwa asilimia 50.49 dhidi ya mshindani wake wa karibu Waziri mkuu wa zamani Raila Odinga aliyepata asilimia 48.7 ya kura hilo.
Kulingana na ELOG, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Wafula Chebukati alikuwa na haki kikatiba kama afisa mkuu wa kitaifa wa Uchaguzi kutangaza mshindi wa uchaguzi wa Rais.
Makamishna wanne kati ya saba wa tume ya IEBC walikataa kutambua matokeo ya urasi wakihoji hayakuwa wazi.
ELOG ikiongozwa na mwenyekiti wake Anne Ireri, imewataka walio na mashaka na matokeo ya uchaguzi mkuu kupeleka pingamizi la kisheria katika mahakama ya juu na kutoa wito kwa wanasiasa wa pande zote kusalia watulivu. Aidha ELOG imesema inaendelea kufuatilia kwa karibu mazingira ya kisiasa Kenya.
Kundi hilo la waangalizi liliendesha zoezi huru la kuhesabu na kujumuisha matokeo kutoka kwa waangalizi elfu moja waliofuatilia matokeo kutoka kwa vituo kadhaa kote nchini.
Kwa jumla,kundi hilo lilikuwa na waangalizi elfu tano kote nchini kufuatilia uchaguzi mkuu wa Kenya uliofanyika Agosti Tisa.
Muungano wa Azimio unaoongozwa na Bwana Odinga umekataa kutambua matokeo ya Urais na baadhi ya wandani wake wamesema wanakusudia kuelekea katika mahakama ya juu kupinga matokeo yaliyompa ushindi Bwana Ruto.
Soma zaidi:
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kushinda urais Kenya
Vita vya Ukraine: Milipuko yatikisa ngome ya Urusi katika Crimea ya Ukraine
Chanzo cha picha, SCIAL MEDIA
Maelezo ya picha, Kulikuwa na milipuko ya mara kwa mara katika kambi ya jeshi la Urusi mapema Jumanne
Kambi ya
kijeshi huko Crimea inayokaliwa na Urusi imekumbwa na msururu wa milipuko,
ikiripotiwa kuwaacha takriban watu wawili wakwa wamejeruhiwa.
Maafisa wa
Urusi walisema moto ulisababisha milipuko katika ghala la silaha eneo la
Dzhankoi kaskazini mwa Crimea.
Moto pia ulionekana kwenye kituo kidogo cha umeme.
Kilichosababisha milipuko hiyo hakijulikani, lakini wiki
iliyopita ndege za kivita za Urusi ziliharibiwa katika shambulio dhahiri la
Ukraine kwenye pwani ya Crimea.
Wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema moto huo ulizuka katika
eneo la kuhifadhia silaha kwa muda karibu na kijiji cha Maiske mwendo wa 06:15
saa za Moscow (03:15 GMT) na kwamba chanzo kinachunguzwa.
Wizara hiyo ilisema hakukuwa na ‘majeruhi mbaya’, lakini
afisa mmoja aliyeteuliwa na Urusi alisema watu wawili wamejeruhiwa.
Mshauri wa ofisi ya rais wa Ukrain Mykhailo Podolyak
alielezea tukio hilo kama ‘’kuondoa wanajeshi’’, akionyesha kuwa milipuko hiyo
haikutokea kwa bahati mbaya.
Kiongozi wa Tatar wa Crimea, Refat Chubarov, pia
alielezea milipuko hiyo kama ‘pigo’.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe
Crimea ilitekwa kutoka Ukraine na kisha kutwaliwa na
Urusi mapema 2014, na wakati majeshi ya Urusi yalipoanzisha uvamizi mpya mwezi
Februari walitumia vituo vyao kwenye rasi kukamata maeneo makubwa ya kusini mwa
Ukraine.
Wafuasi wa Raila Odinga: Kulikuwa na 'Ubakaji wa demokrasia' katika uchaguzi wa Kenya
Mgombea wa upinzani na Waziri mkuu wa zamani wa Kenya Raila hajazungumza hadharani baada ya hasimu wake William Ruto kutangazwa kuwa Rais mteule.
Haijawa wazi iwapo Bw Odinga atawasilisha mashitaka kupinga matokeo ya uchaguzi
Mshauri wa zamani wa Bw Odinga, Salim Lone, ameieleza BBC maoni yake kuhusu kupoteza ushindi kwa mkuu wake wa zamani.
Ujumbe wa nukuu ’’Nimekuwa na mazungumzo marefu nay eye na amesema wazi kwamba anadhani ni kama huu ulikuwa ni ubakaji wa demokrasia.
Kwahiyo, haoni kuwa hii inakubalika kabisa’’
Unumbe wa nukuu : ‘’Tatizo letu ni kwamba huu ni uchaguzi wa nne wenye ushindani mkali na huu ulikuwa mbaya zaidi wakati tulidhani kuwa hatimaye huu ungekuwa bora zaidi.
Sio wa kuaminika kwa sababu makamishna wanne kati ya saba hawakusaini katika tangazo kuhusu kutangazwa kwa Bw Ruto kwamba alichaguliwa kisheria ."
Mgombea mwenza wa Bw Odinga Martha amesema kwenye Twitter kwamba : "haijaisha hadi iishe’’
Afisa wa uchaguzi wa Kenya aliyetoweka apatikana amefariki - ripoti
Aliyekuwa
msimamizi wa uchaguzi katika kituo cha kupigia kura katika mji mkuu wa Kenya,
Nairobi, amepatikana akiwa amefariki siku chache baada ya familia yake kuripoti
kuwa ametoweka, vyombo vya habari vya Kenya vinaripoti.
Mwili wa
Daniel Mbolu Musyoka ulipatikana katika msitu wa Loitoktok chini ya Mlima
Kilimanjaro karibu na mpaka na Tanzania, ripoti zinamnukuu mkuu wa polisi
akisema.
Mwili
huo ulitambuliwa na dada zake wawili, gazeti la Daily Nation linaongeza.
Inasema mwili huo ulipatikana na wafugaji na ulikuwa na alama zinazoonyesha
alifanyiwa mateso.
Bw
Musyoka alikuwa afisa msimamizi katika eneo la Embakasi Mashariki jijini
Nairobi.
Kutoweka
kwake kuliripotiwa Ijumaa iliyopita na tume ya uchaguzi, ambayo ilisema
alitoweka akiwa kazini katika kituo cha kujumlisha kura.
Soma zaidi:
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kushinda urais Kenya
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Kwa picha ngome ya Raila Odinga Kisumu ni shwari baada ya matokeo
Biashara nyingi zimefungwa mjini Kisumu katika ngome ya Raila Odinga magharibi mwa Kenya, mwandishi wa BBC Roncliffe Odit anasema.
Bw Odinga alishindwa kwa kura chache katika uchaguzi wa urais na William Ruto - ambaye alitangazwa mshindi Jumatatu kwa 50.49% ya kura.
Baadhi ya maandamano katika ngome za Bw Odinga yalifuatia tangazo la Jumatatu la Bw Ruto kuwa mshindi wa uchaguzi huo.
Bw Odinga bado hajazungumza hadharani kuhusu matokeo ya uchaguzi huo.
Jumanne asubuhi, ni shwari katika jiji, kama picha hizi kutoka mitaani zinavyoonyesha:
Soma zaidi:
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kushinda urais Kenya
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Marekani yasema kutangazwa kwa ushindi wa Ruto ni 'hatua' muhimu
Chanzo cha picha, Reuters
Maelezo ya picha, William Ruto alitangazwa kama mshindi kwa kupata 50.49% ya kura
Ubalozi wa Marekani nchini Kenya
umewapongeza Wakenya kwa uchaguzi wa amani na kuzitaka pande zote kushirikiana
kutatua hofu yoyote iliyosalia kwa amani.
Ulisema kutangazwa kwa William Ruto kama rais mteule wa Kenya ni ‘’hatua
muhimu katika mchakato wa uchaguzi”.
“Kusonga mbele, tunaziomba pande zote kushirikiana kwa pamoja kutatua hofu
zilizosalia kuhusu uchaguzi huu kwa njia zilizopo za utatuzi ” uliongeza.
Ubalozi huo umewataka viongozi wa kisiasa kuwatolea wito wafuasi wao
kuendelea kuwa watulivu na kuepuka ghasia wakati wa mchakato wa uchaguzi.
Bw Ruto alitangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi akiwa na 50.49% ya kura- akimshinda mpinzani wake, waziri mkuu wa
zamani Raila Odinga.
Mawakala wa uchaguzi wa Bw Odinga hatahivyo walisema hawakuweza kuhakiki
matokeo na baadhi ya makamishha wa Tume ya uchaguzi walitangaza kwamba
hawakuweza "kuchukua udhibiti wa matokeo".
Bw Ruto aliahidi kufanya kazi kwa ajili ya Wakenya wote, akisema kuwa mchakato
wa matokeo ulikuwa "wa uwazi zaidi kuwahi kushuhudiwa " nchini Kenya.
Sherehe, vifijo, shangwe na nderemo viliibuka katika ngome ya Bw Ruto huku maandamano
ya kupinga yakiripotiwa katika ngome kuu za Bw Odinga.
Soma zaidi:
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kushinda urais Kenya
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Salamu za pongezi kwa rais mteule wa Kenya William Ruto zaendelea kumiminika
Viongozi mbali
mbali wa kimataifa wameendelea kutuma salamu za pongezi kwa rais mteule wa
Kenya William Ruto kufuatia kutangazwa kwake Jumatatu kama mshindi wa uchaguzi wa
urais uliofanyika tarehe 9 Agosti.
Katika ujumbe
wake wa Twitter Rais wa Burundi Evariste Ndayishimiye amesema ''ningependa kumpongeza
rais mteule wa Kenya William Ruto na watu wa Jamuhuri ya Kenya kwa kuendesha
uchaguzi wa huru, haki na wa amani.''
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 1
Naye Rais wa Nigeria Mahammadu Buhari amesema ningependa kuwapongeza watu wa Kenya kwa uchaguzi wa amani, na
matokeo yenye uwazi, ambayo kwa mara nyingine tena yanaonyesha kuwa mchakato wa
demokrasia ,maadili na kanuni vinasalia kuwa njia bora kwa watu kwa kuwachagua viongozi
wao na kuwawajibisha
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 2
Naye Rais wa Tanzania Samia Suluhu kupitia ukurasa wake wa Twitter alisema:’’
Ninawapongezaa Wakenya kwa uchaguzi wao mkuu wa amani na kutangazwa kwa Dr
William Ruto kama Rais mteule. Tunatazamia
kuendelea kufanya kazi na makaka na madada zetu nchini Kenya kuimarisha uhusiano
wetu wa karibu. Tuko pamoja’’:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 3
Hali kadhalika
Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mahamud amendika kwenye ukurasa wa Twitter
akimpongeza Bw William Ruto kwa kuwa rais wa tanowa Kenya:
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Onyo: BBC haihusiki na maudhui ya nje
Mwisho wa X ujumbe, 4
Soma zaidi:
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kushinda urais Kenya
Raia wa maeneo mbalimbali waendelea kusheherekea Kenya
Nchini Kenya
raia kutoka maeneo tofauti tofauti waendelea kusherehekea.
Hili linawadia
baada ya Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi Kenya Wafula Chebukati kumtangaza William
Ruto kuwa mshindi wa uchaguzi mkuu.
William Ruto
ametangazwa kuwa Rais mteule wa Kenya, na kupata asilimia 50.49 ya kura.
Mshindani wake wa
karibu alikuwa Raila Odinga, ambaye tume ya uchaguzi inasema amepata 48.85%
Waliofuatia kwa mbali
walikuwa ni George Wajackoyah na David Mwaure ambao kwa pamoja wamepata chini
ya 1% .
Maelezo ya video, Raia wa maeneo mbalimbali waendelea kusherehekea Kenya
Mgombea mwenza Martha Karua asema 'haijaisha'
Hadi muda mfupi uliopita, hatukusikia lolote kutoka kwa kambi ya Raila Odinga.
Lakini mgombea mwenza , Martha Karua, kwa sasa amevunja ukimya kwa kutuma ujumbe wa Twitter akisema "Haijaisha hadi iishe."
Hatuwezi kusema kwa uhakika maana ya tweet hiyo yenye utata kidogo, lakini watu wengi wanashuku kwamba muungano wa Bw Odinga wa Azimio utapinga matokeo ya uchaguzi wa mahakamani.
Chini ya sheria za Kenya, wagombea urais wana siku saba za kukata rufaa.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Wakenya sasa
wameambiwa kwamba walimchagua William Ruto kama rais wao ajaye, dakika chache
kabla ya tangazo hilo makamu mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, Juliana Cherera,
alisema yeye na makamishna wengine watatu wa uchaguzi hawakuweza kuwa na kauli
juu ya matokeo.
Kuna
makamishna saba tu.
Tangazo la
kundi hilo lililojitenga limeongeza wasiwasi nchini humo.
Sheria ya
uchaguzi hata hivyo inampa mwenyekiti jukumu la kutangaza matokeo ya uchaguzi
wa urais.
Wafula
Chebukati alifanya hivyo na sasa Bw Ruto ametangazwa kuwa rais ajaye.
Timu ya
Raila Odinga inaweza kupinga matokeo hayo mahakamani na ina siku saba
kuwasilisha kesi.
Kumbuka kwamba
mwaka 2017 alifanya hivyo na hatimaye mahakama ya juu iliamua kwamba uchaguzi
wa urais ulipaswa kurudiwa.
Soma zaidi:
Shangwe tele baada ya ushindi wa William Ruto
Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: William Ruto ndiye rais mteule Kenya
William Ruto: Muuza kuku aliyepanda ngazi hadi kushinda urais Kenya
Wafuasi wa Raila Odinga waweka vizuizi barabarani
Maelezo kuhusu taarifa
Author, Roncliffe Odit
Nafasi, BBC KISUMU
Chanzo cha picha, Supplied
Kuna masikitiko makubwa na uchungu kwa wafuasi wa Raila Odinga kutokana na kupoteza nafasi ya kushinda nafasi ya urais.
Mamia ya watu wamekuwa wakikusanyika katika mitaa ya Kisumu - ngome ya wafuasi wake - ambapo hali imebadilika kutoka kwa msisimko hadi kuwa hasira.
Baadhi ya watu wameweka vizuizi vya barabarani na moto. Polisi wa kupambana na fujo walitumwa sehemu za jiji mapema.