Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Waliokuwa vigogo na kutupwa nje kwa muda wachaguliwa tena

Farah Maalim

Chanzo cha picha, Farah Maalim /FACEBOOK

Maelezo ya picha, Farah Maalim
    • Author, Asha Juma
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Iliyochapishwa

Raia nchini Kenya wanaendelea kusubiri matokeo kujua nani atakayekuwa rais mpya baada ya shughuli ya kupiga kura kukamilika Agosti 9, 2022.

Na hadi kufikia sasa, wananchi wameanza kutambua viongozi wao katika nyadhifa tano zilizosalia yaani gavana, seneta, mbunge, mwakilishi wa kina mama na mbunge wa bunge la kaunti.

Hata hivyo miongoni mwa waliobahatika kurejea tena kwenye ulingo wa siasa baada ya kukaa nje kwa muda ni pamoja na Farah Maalim.

Farah Maalim arejea baada ya kuwa nje kwa miaka 10

Aliyekuwa naibu spika Farah Maalim amerejea kwenye ulingo wa siasa baada ya kushinda kiti cha ubunge eneo la Dadaab.

Farah Maalim anarejea kwenye siasa baada ya kuwa nje kwa miaka 10 kumi kupitia chama cha Wiper.

Maalim aliwakilisha eneo bunge kubwa la Lagdera kuanzia 2007 hadi 2013 na mwaka huo wa 2013 aliwania kiti cha Seneti lakini akashindwa na Yussuf Haji (aliyefariki).

Mnamo 2017 aligombea ubunge wa Garissa Township lakini akashindwa na Aden Duale.

Hadi wakati huo, alidai kura ziliibiwa na kwenda mahakamani lakini baadaye akafuta kesi hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutangazwa mshindi na kukabidhiwa cheti, Maalim aliwashukuru wapiga kura kwa kumpa nafasi ya kuhudumu kwa mara nyingine.

"Sina maneno ya kutosha kuwashukuru watu wa Dadaab kwa kunipa imani ya kuwaongoza kwa mara nyingine tena. Imekuwa safari ndefu lakini iliyoisha kwa mwisho mwema. Sasa safari ya kweli na kazi ya kubadilisha maisha ya watu wetu inaanza," alisema.

"Kama ilivyo siku zote tunataka kuweka kipaumbele katika masuala ya maji, elimu na uboreshaji wa jumla wa miundombinu. Pia nitafanya kazi kwa karibu na serikali zote mbili kwa ajili ya kuboresha watu wetu."

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Samuel Gonzi Rai

Gonzi Rai

Chanzo cha picha, Gonzi Rai/FACEBOOK

Maelezo ya picha, Gonzi Rai

Gonzi Rai ameshinda kiti cha ubunge katika eneo la Kinango nafasi aliyoshika kwa miaka 20 katika vipindi tofauti tofauti.

Bwana Gonzi Rai ambaye amesimama kupitia chama cha Pamoja Africa Alliance ameibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake wa karibu Benjamin Dalu Tayari aliyesimama kupitia chama cha UDA.

Bwana tayari ndiye aliyemnyanganya tonge mdomo katika uchaguzi wa mwaka 2017.

Bwana Gonzi Rai ambaye amekuwa uongozini tangu mwaka 1992 hadi 2007 wakati huo akiwa chini ya chama cha KANU, kabla ya kuondolewa na Simeon Mkalla.

Hata hivyo katika safari yake hii, Gonzi Rai amekuwa ndani ya vyama kadha wa kadha.

Katika uchaguzi wa mwaka 2002 na 2007, Gonzi Rai aliwania ubunge kupitia chama cha Ford People huku mwaka 2013 akijitoza uwanjani kupitia chama cha TNA.

Wakati wa kampeni yake, miongoni mwa masuala alioahidi kuyatafutia ufumbuzi ni pamoja na maji, kukabiliana na kutojua kusoma na kuandika na kuimarisha usalama wa chakula katika eneo bunge lake.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Danson Mungatana

Danson Mungatana

Chanzo cha picha, Danson Mungatana/FACEBOOK

Maelezo ya picha, Danson Mungatana

Katika eneo bunge la Garsen, baada ya kujaribu mara mbili, kurejea kwenye ulingo wa siasa bila mafanikio, mbunge wa zamani Danson Mungatana hatimaye ana kila sababu ya kutabasamu.

Bw Mungatana ambaye amesimama kupitia chama cha (United Democratic Alliance) ametangazwa kuwa seneta mteule wa Tana River baada ya kuwashinda wapinzani wake.

Bwana Mungatana amekaa nje ya siasa kwa miaka 10 tangu alipopoteza kiti chake cha ubunge.

"Hii ni ndoto iliyotimia. Mwanzo wa hatma yenye matumaini kwa watu wa kaunti ya Tana River, mimi mwenyewe na familia yangu," alisema.

Mnamo 2013, Bw Mungatana ambaye pia ni wakili, alijaribu bahati yake katika kiti cha ugavana Tana River na kuibuka wa nne.

Tena mnamo 2017, alijaribu tena kwa mara ya pili, na kuibuka wa nne.

Pia naye, aliwahi kukumbana na jinamizi linaloumiza wengi mjini baada ya kupatana na matapeli wa Afrika Magharibi, na kupoteza Sh76 milioni waliokuwa wamemuahidi kuwa bilionea.

Mwaka 2019, alikamatwa na shirika la kupambana na ufisadi kwa madai ya kuhusika katika ufujaji wa Sh51 milioni katika Kaunti ya Kilifi.

Mwalimu Harrison Garama Kombe

Huko Magarini, Kilifi, Harrison Kombe wa chama cha (ODM) amepata ubunge baada ya kutokuwepo kwa miaka mitano.

Mwalimu Harrison Garama Kombe aliingia katika siasa mwaka 2002 baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge katika bungee la 9 kuwakilisha Jimbo la Magarini kwa tiketi ya Shirikisho.

Bw Kombe, ambaye alihudumu kwa mihula miwili kuanzia 2002-2007 kupitia chama cha Shirikisho na 2013-2017.

Aidha, alizua utata mwaka wa 2017 alipodai kuwa anaweza kutibu VVU kwa kutumia tiba ya reflexology.

Mnamo mwaka 2007, kiti hicho kilitangazwa wazi na mahakama kuu ikiwa kumesalia miezi tisa kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu na uchaguzi mdogo ulifanyika ambapo alishindwa na Amason Kingi Jeffah.

Mnamo mwaka wa 2007 katika uchaguzi mkuu, aligombea tena lakini akashindwa tena na Amason Kingi Jeffah.

Na kuanzia 2008, alirejea kufundisha katika Shule ya Upili hadi 2013 alipowania tena kiti cha Magarini na kukinyakua kwa tikiti ya URP kupitia muungano wa Jubilee.

th

Pia unawezakusoma:

th