Nimesikia Mbowe yuko kwenye uzinduzi wa bwawa, wakati Mwenyekiti wake yuko Ukonga - Lissu

Chanzo cha picha, CHADEMA
Mwaka 2005, Rais Benjamin Mkapa aliondoka madarakani na nafasi yake kuchukuliwa na Jakaya Kikwete. Miaka yake ya kwanza madarakani ilikuwa ya vuguvugu la mageuzi ya kisiasa, Lissu amesema.
Ameendelea kusema kuwa mwaka 2010, uchaguzi ulifanyika chini ya mfumo huohuo wa uchaguzi, na kulizuka malalamiko makubwa, hususan Zanzibar. Kelele za kudai mabadiliko zikawa nyingi.
Alipochaguliwa kwa muhula wa pili, Kikwete alisema kulikuwa na haja ya kupata Katiba mpya ili kushughulikia changamoto hizo.
Mwaka 2014, wakati mchakato wa Katiba Mpya ukiwa kwenye hatua za mwisho chini ya Rasimu ya Jaji Joseph Warioba, CCM ilipinga baadhi ya mapendekezo yake. Baadaye, Kikwete alisema masuala hayo yangejadiliwa baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Mwaka 2015, chini ya mfumo huohuo wa uchaguzi, John Magufuli alichaguliwa kuwa Rais akiwa na Samia Suluhu Hassan kama Makamu wa Rais.
Majaji, nilisahau kutaja kwamba mwaka 2020 nilirudi kutoka uhamishoni ili kushiriki uchaguzi dhidi ya Magufuli kama mgombea urais wa CHADEMA.
Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, baada ya matokeo kutangazwa, Tume ya Uchaguzi huchapisha matokeo ya majimbo katika Gazeti la Serikali. Ukiangalia chaguzi zilizopita kabla ya mwaka 2020, utaratibu huo ulikuwa ukifuatwa.
Hata hivyo, mwaka 2020 matokeo ya urais hayakuchapishwa. Sina uhakika kuhusu uchaguzi uliofuata kwa sababu nilikuwa gerezani, lakini ninaamini kulikuwa na mambo mengi yasiyo ya kawaida.
Majaji, ukisoma taarifa za waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa pamoja na zile za Umoja wa Afrika, utaona walieleza kuwepo kwa dosari mbalimbali katika uchaguzi huo.
Ripoti ya Tume ya Uchaguzi ya mwaka 2020 iliwasilishwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan mwaka 2021. Kwa mujibu wa Lissu, mijadala kuhusu umuhimu wa mageuzi ya kisiasa na kikatiba iliendelea kujitokeza baada ya uchaguzi huo.
Baadaye, CHADEMA ilianzisha kampeni ya kudai Katiba Mpya. Katika kipindi hicho, Mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe, alikamatwa na kukabiliwa na kesi ya ugaidi iliyodumu kwa miezi kadhaa kabla ya kuhitimishwa.
"Jana nimesikia Mbowe yuko kwenye uzinduzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, wakati mimi niko hapa Ukonga," alisema Lissu.
Soma pia:












