Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Iran yafanya mashambulizi mapya, ndege za Marekani zaanguka Kuwait

Wakati huo huo nchini Lebanon, mshambulizi ya Israel yamewauwa takriban watu 31, wizara ya afya inasema. Israel inasema ilikuwa ikijibu mashambulizi ya ndege zisizo na rubani na roketi kutoka kwa Hezbollah.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Ambia Hirsi & Asha Juma

  1. Israel na Iran wafunga anga zao kwa safari za ndege za raia

    Israel imefunga anga yake kwa safari za ndege za kiraia kufuatia shambulio dhidi ya Iran Jumamosi asubuhi, kulingana na ripoti katika vyombo vya habari vya Israeli.

    Shirika la Habari la Tasnim, ambalo lina uhusiano na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, linaripoti anga ya Iran pia imefungwa.

    Majid Akhavan, msemaji wa Shirika la Usafiri wa Anga nchini Iran, alitangaza: "Kulingana na NOTAM iliyotolewa, anga ya nchi nzima imefungwa hadi ilani nyingine."

    Wakati huo huo, Wizara ya Afya ya Iran imetangaza kuwa hospitali ziko katika hali ya kusubiri na kwamba idadi ya waliojeruhiwa itatangazwa baada ya uthibitisho wa mwisho.

    Soma pia:

  2. Marekani na Israel zafanya mashambulizi ya 'tahadhari' dhidi ya Iran

    Shirika la habari la Reuters limemnukuu Waziri wa Ulinzi wa Israel akisema Jumamosi kuwa Israel imefanya shambulio la makombora la kuzuia kabla dhidi ya Iran.

    Jeshi la Israel lilitangaza kuwa limewasha ving’ora vya tahadhari ya mashambulizi ya anga katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo “kuwaandaa wananchi kwa uwezekano wa kurushwa kwa makombora kuelekea Israel” kama hatua ya kulipiza kisasi.

    Wakati huo huo, Rais wa Marekani Donald Trump amechapisha video ya dakika nane kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social na kuthibitisha kuwa Marekani ilihusika katika shambulizi dhidi ya Iran.

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jumamosi ya tarehe 28 Februari 2026, kwamba Marekani ilikuwa imeanzisha "operesheni kubwa zaidi" nchini Iran.

    "Lengo letu ni kutetea watu wa Marekani kwa kuondoa tishio lililo karibu na utawala wa Iran," Bw. Trump alisema kwenye video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

    Soma pia:

  3. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja ya tarehe 28/02/2026, tutakuarifu taarifa zinazochipuka. Ungana nasi hadi tamati.