Habari za hivi punde, Trump asema Kiongozi Mkuu wa Iran amekufa
Khamenei, mmoja wa watu waovu zaidi katika Historia, amekufa," Rais wa Marekani Donald Trump ameandika kwenye Truth Social.
'Haki si kwa watu wa Iran pekee, bali kwa Wamarekani wote Bora' - Trump
Katika akaunti yake kwenye mtandao wa Truth Social, Rais wa Marekani Donald Trump ameandika.
"Hii si haki kwa watu wa Iran pekee, bali kwa Wamarekani wote Bora," amesema.
"Hakufanikiwa kukwepa Majasusi wetu na Mifumo yetu ya Ufuatiliaji ya Kisasa, na, kwa ushirikiano wa karibu na Israeli, hakukuwa ambalo yeye, au viongozi wengine awaliouawa pamoja naye, wangeweza kufanya."
"Hii ndiyo fursa kubwa zaidi kwa watu wa Iran kuirudisha Nchi yao," ameongeza.
Awali, Rais Donald Trump wa Marekani alizungumza na NBC News kwa njia ya simu - na wamemuuliza kuhusu ripoti kwamba kiongozi mkuu wa Iran ameuawa na mashambulizi ya anga ya Marekani na Israel.
"Nimezungumza na watu wengi, tunahisi huu ni ukweli," Inaripotiwa Trump amemwambia mtangazaji wa Marekani.
"Idadi kubwa ya viongozi wao pia wameuawa," aliongeza, akirudia kile alichoambia ABC News.
Pia aliambia NBC News kwamba operesheni ya Marekani nchini Iran "tayari imefanikiwa".
Trump asema 'viongozi wengi wa Iran wameuawa
Awali, Rais Trump alizungumza na ABC News na kusema kwamba mashambulizi ya Marekani "tayari yamesababisha uharibifu mkubwa" na kuwa viongozi "wengi" wa Iran wameuawa.
"Hatujui yote, lakini mengi yanajulikana," Trump amesema katika mahojiano ya simu. Rais pia ameongeza kuwa Marekani "ina maono mema" juu kundi lijalo la viongozi wa Iran.
Alipoulizwa kuhusu ni nani atakayechukua nafasi ya Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Khamenei, Trump kisha ameiambia NBC: "Sijui, lakini wakati fulani watanipigia simu kuuliza ni nani ningependa."
"Ninakuwa na mzaha kidogo ninaposema hivyo," Trump ameongeza:
Trump alipoulizwa ikiwa ana 'uhakika' kiongozi mkuu wa Iran ameuawa
Rachel Scott, mwandishi mkuu wa habari za kisiasa katika shirika la ABC News, amesema Donald Trump amemwambia tu kwamba "anaamini" kiongozi mkuu wa Iran amekufa.
Alipoulizwa kama ana "uhakika", Trump inasemekana alisema: "Sitaki kusema chochote kwa uhakika hadi nitakapoona kwa maco yangu lakini tunaamini amekufa."
"Na viongozi wao wengi wameuawa. Sio tu kutoka kwenye eneo moja bali pia kutoka kwenye maeneo mengine mawili ambayo pia tumeshambulia. Tulikuwa na taarifa nyingi za ujasusi hivyo basi, tunaamini viongozi wengi wameuawa."
Soma zaidi: