Iran yasema watu 40 wameuawa katika shambulio dhidi ya shule ya wasichana – ripoti
Afisa mmoja ameliambia Shirika la Habari la Taifa la Iran (IRNA) kuwa watu 40 wameuawa kufuatia shambulio la Israel dhidi ya shule ya msingi ya wasichana katika kaunti ya Minab, mkoa wa Hormozgan kusini mwa Iran, tarehe 28 Februari.
Gavana Mohammad Radmehr amesema watu wengine 48 walijeruhiwa, na kwamba idadi ya vifo kutokana na shambulio hilo katika Shule ya Wasichana ya Shajareh Tayyebeh inaendelea kuongezeka.
BBC haijaweza kuthibitisha taarifa hizi kwa njia huru, kwani mara nyingi mashirika ya habari ya kimataifa hukataliwa viza za kuingia Iran, hali inayopunguza uwezo wao wa kukusanya taarifa kuhusu matukio yanayoendelea ndani ya nchi hiyo.
Kando na hilo, Iran inakabiliwa na kukatika kwa huduma ya intaneti, sambamba na taarifa za awali za shambulio la kimtandao.
Soma zaidi: