Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

‎Maandamano Saba saba: 10 wakamatwa Nairobi huku Tanzania kukiwa kimya

Hali ya ulinzi imeonekana kuimarishwa zaidi katika jiji kuu la kibiashara la Tanzania Dar es Salaam, huku mamia ya maafisa polisi na jeshi wakionekana kutanda katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo.

Muhtasari

Moja kwa moja

Lizzy Masinga, Rashid Abdallah & Asha Juma

  1. Safari ya Ronaldo katika Kombe la Dunia yafikia mwisho kwa machozi

    Mmoja wa wasakata kabumbu mahiri kuwahi kutokea duniani Cristian Ronaldo wa Ureno amelazimika kuimaliza kazi yake bila kutwaa tuzo kubwa zaidi duniani baada ya mechi yake ya mwisho kwa Ureno kumalizika kwa kushindwa 1-0 na Hispania katika hatua ya 16 bora.

    Ronaldo alibubujikwa machozi huku hadithi yake ya Kombe la Dunia ikimalizika jijini Dallas baada ya kushuhudia goli la dakika za majeruhi la Mikel Merino likiwapa majirani zao nafasi ya kutinga robo fainali.

    Mshindi huyo wa Ballon d'Or mara tano, mshindi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mara tano na bingwa wa Euro 2016 mwenye umri wa miaka 41, ana rekodi ya dunia ya kufunga mabao 976 kwa vilabu na nchi yake.

    Amefunga mabao sita kwa rekodi ya Kombe la Dunia. Lakini ushindi wake wa karibu zaidi ya kombe la dunia ni wakati Ureno ilipocheza nusu fainali katika fainali zake za kwanza mwaka 2006 huko Ujerumani.

    Leo usiku ni Misri dhidi ya Argentina na Uswisi ikicheza na Colombia kukamilisha hatua ya 16 bora.

    Unaweza kusoma;

  2. Zelensky kuishinikiza NATO kuipatia Ukraine mifumo ya ulinzi wa anga baada ya mashambulizi makali ya Urusi

    Rais wa Ukraine anapanga kutumia mkutano wa NATO nchini Uturuki kuwahimiza washirika wa Kyiv kuipatia mifumo ya ulinzi wa anga inayohitaji kwa dharura ili kujilinda dhidi ya mashambulizi ya Urusi yanayozidi kuongezeka.

    Wito wa Volodymyr Zelensky wa kuomba msaada umeongezeka uzito baada ya makombora ya Urusi kushambulia mji mkuu wa Ukraine mara mbili ndani ya kipindi kisichozidi wiki moja, yakipiga majengo ya makazi na kusababisha vifo vya zaidi ya raia 50.

    Mkutano huo mjini Ankara pia utampa Zelensky fursa ya kukutana na Donald Trump katika mazungumzo muhimu na kusisitiza hoja yake kwamba mashambulizi ya "kikatili" ya Urusi yanaonesha udhaifu badala ya nguvu, na kwamba Vladimir Putin anapaswa kushinikizwa kuingia katika mazungumzo yatakayolenga kufikia amani yenye "heshima."

    Mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya Ukraine yanakuja wakati nchi hiyo imekuwa ikiongeza mashambulizi yake ya masafa marefu kwa kutumia ndege zisizo na rubani dhidi ya Urusi, ikilenga viwanda vya kusafisha mafuta na maeneo ya kijeshi, hali iliyosababisha upungufu mkubwa wa mafuta na kukatika kwa umeme katika baadhi ya maeneo ya Urusi.

    Unaweza kusoma;

  3. Vitisho na wito wa kuwaua "wauaji wa Khamenei" katika mazishi Tehran

    Shughuli rasmi za mazishi ya aliyekuwa kiongozi wa Jamhuri ya Kiislamu katikati mwa Tehran, pamoja na mabadiliko na hali ya kutokuwepo kwa mwafaka iliyowachanganya maelfu ya watu, iliambatana pia na kauli kali dhidi ya Masoud Pezeshkian, Abbas Araqchi na wajumbe wa mazungumzo na Marekani.

    Picha zilizotolewa kutoka kwenye maandamano hayo, ikiwa ni pamoja na kurushiwa mawe picha ya Donald Trump na wito wa "kuwaua wauaji" wa Ali Khamenei, zilikuwa miongoni mwa mambo yaliyovutia katika hafla hiyo, ambayo ilifanyika kwa uratibu na maandalizi makubwa ya serikali.

    Donald Trump ametoa tena vitisho vipya dhidi ya Iran, akisema kwamba ikiwa makubaliano hayatapatikana na Iran, "atakamilisha kazi."

    Akijibu tishio hilo, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kwa Rais wa Marekani: "Zungumza kwa heshima na watu wa Iran, la sivyo tutakujibu kwa lugha tofauti."

    Unaweza kusoma;

  4. Habari za asubuhi,katika taarifa zetu