Safari ya Ronaldo katika Kombe la Dunia yafikia mwisho kwa machozi
Mmoja wa wasakata kabumbu mahiri kuwahi kutokea duniani Cristian Ronaldo wa Ureno amelazimika kuimaliza kazi yake bila kutwaa tuzo kubwa zaidi duniani baada ya mechi yake ya mwisho kwa Ureno kumalizika kwa kushindwa 1-0 na Hispania katika hatua ya 16 bora.
Ronaldo alibubujikwa machozi huku hadithi yake ya Kombe la Dunia ikimalizika jijini Dallas baada ya kushuhudia goli la dakika za majeruhi la Mikel Merino likiwapa majirani zao nafasi ya kutinga robo fainali.
Mshindi huyo wa Ballon d'Or mara tano, mshindi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mara tano na bingwa wa Euro 2016 mwenye umri wa miaka 41, ana rekodi ya dunia ya kufunga mabao 976 kwa vilabu na nchi yake.
Amefunga mabao sita kwa rekodi ya Kombe la Dunia. Lakini ushindi wake wa karibu zaidi ya kombe la dunia ni wakati Ureno ilipocheza nusu fainali katika fainali zake za kwanza mwaka 2006 huko Ujerumani.
Leo usiku ni Misri dhidi ya Argentina na Uswisi ikicheza na Colombia kukamilisha hatua ya 16 bora.
Unaweza kusoma;