Matokeo ya Uchaguzi Kenya 2022: Mbivu na mbichi kujulikana

Shughuli ya kuhesabu kura inaendelea
Maelezo ya picha, Shughuli ya kuhesabu kura inaendelea
Iliyochapishwa

Matokeo ya muda yanaonesha ushindani mkali wa kura za urais nchini Kenya kati ya Naibu Rais William Ruto na waziri mkuu wa zamani Raila Odinga.

Huku ikiwa zaidi ya asilimia 90% ya matokeo yametumwa kutoka mashinani, hesabu za ndani za data zinaonesha kwamba wawili hao wamekabana koo.

Hata hivyo inaweza kuchukua siku kadhaa kabla ya matokeo rasmi kutagazwa.

Uchaguzi huu unajiri baada ya kipindi cha kampeni kali iliyotawaliwa na mijadala kuhusu gharama za maisha, ukosefu wa ajira na ufisadi.

Waliojitokeza kupiga kura wanakadiriwa kuwa karibu 60%, ikiwa ni idadi ndogo ikilinganishwa na asilimia 80% katika uchaguzi uliopita miaka mitano iliyopita.

Siku ya uchaguzi iliokuwa na amani kwa kiasi kikubwa ilikumbwa na ucheleweshaji wa vifaa na kushindwa kwa kifaa cha kielektroniki kutambua baadhi ya wapiga kura katika maeneo kadhaa nchini.

Baba dhidi dhidi ya 'Hustler'

Wapinzani wawili katika kinyang'anyiro cha urais ni wanasiasa wenye uzoefu.

Bw Odinga, 77, - kiongozi wa upinzani wa muda mrefu, anayeitwa Baba ("baba") , anawania urais kwa mara ya tano. Bw Ruto, 55, ambaye amejaribu kusisitiza uhusiano wake na Wakenya wa kawaida kwa kujiita "hustler", anawania wadhfa huo kwa mara ya kwanza.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Wagombea wengine wawili - David Mwaure na George Wajackoya - pia wako kwenye kinyang'anyiro hicho.

Rais anayeondoka Uhuru Kenyatta anaunga mkono Bw Odinga, mpinzani wake aliyegeuka kuwa mshirika wake, kumrithi, baada ya kutofautiana na Bw Ruto.

Ili kushinda kinyang'anyiro cha urais katika awamu ya kwanza, mgombea anahitaji:

  • Zaidi ya nusu ya kura zote zilizopigwa kote nchini
  • angalau 25% ya kura zilizopigwa katika angalau kaunti 24.

Baada ya kuhesabu kura, viongozi wa eneo hilo huchukua picha ya karatasi ya mwisho ya kujumlisha na kutuma picha hiyo kwa maeneo bunge na vituo vya kitaifa vya kujumlisha kura.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Vyombo vya habari, vyama vya kisiasa na mashirika ya kiraia yamekuwa yakikusanya hesabu zao kwa kutumia matokeo haya ya mwisho yaliyotangazwa katika vituo zaidi ya 40,000 vya kupigia kura.

Lakini tume ya uchaguzi pekee ndiyo inayoweza kutangaza mshindi wa uchaguzi wa urais baada ya kuthibitisha fomu halisi na za kidijitali zinazotumwa kwa kituo cha kitaifa cha kuhesabia kura.

.

IEBC ina siku saba kutangaza matokeo.

.