Mzozo wa Ukraine: Mambo matano ambayo hukujua kuhusu uvamizi wa Urusi huko Ukraine

Chanzo cha picha, Reuters
Katika siku ya tano ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, mapigano hayo yalienea katika miji kadhaa huku wawakilishi wa Ukraine na Urusi wakifanya mazungumzo yao ya kwanza ya ana kwa ana tangu vita hivyo kuanza.
Urusi inazingirwa huku Rais Putin akitangaza hali ya hatari kuhusu mpango wa nyuklia wa Urusi, na hivyo kuzua ghadhabu kubwa.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amesema shambulio la Urusi mjini Kharkiv ni uhalifu wa kivita.
Bw Zelensky alisema kuna mashahidi waliosema raia walikuwa wakilengwa makusudi.
Wizara ya mambo ya ndani ilisema makumi ya watu wameuawa.
Picha ya satelaiti ya Marekani inasema msafara wa wanajeshi wa Urusi unaelekea katika mji mkuu, Kiev.

Urusi imeshutumiwa kwa kulipua maeneo ya umma
Watu kadhaa wameuawa katika uvamizi unaoongozwa na Urusi dhidi ya Ukraine, na makombora yameshambulia mji wa Kharkiv, kulingana na maafisa wa Ukraine.
Picha zilizochapishwa kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha makombora yakipiga mji wa Kharkiv, ambao ni wa pili kwa ukubwa Ukraine na makazi kwa watu milioni 1.4, huku mamia wakiripotiwa kujeruhiwa.
Urusi imekanusha kuhusika na mauaji hayo.
Wakati huo huo, wawakilishi wa Urusi na Ukraine walifanya mazungumzo huko Belarus.
Matarajio ya uamuzi wa haraka katika mkutano huo hayakuwa makubwa, na mazungumzo yalifanyika saa kadhaa baadaye, na ripoti kwamba duru ya pili inaweza kufanyika katika siku zijazo.
Tahadhari zimesikika mjini Kiev, na wakaazi wamekimbilia kwenye vituo vya treni huku kukiwa na ripoti kwamba wanajeshi wa Urusi wameshambulia maeneo ya viunga vya mji mkuu.
Picha za satelaiti zinaonyesha wanajeshi wa Urusi wakisonga mbele kusini mwa mji mkuu Kiev.

Urusi yaishambulia Ukraine:Mengi zaidi
- MOJA KWA MOJA:Ukraine na Urusi: Shambulio la pili lapiga mji wa pili kwa ukubwa Kharkiv
- YA MSINGI:Mzozo wa Ukraine: Kwanini Urusi inaivamia Ukraine na Putin anataka nini?
- UFAFANUZI:Mzozo wa Ukraine: Swift ni nini na kwa nini kuipiga marufuku Urusi ni muhimu sana?
- UCHAMBUZI:Mzozo wa Ukraine: Putin humsikiliza nani?
- KWENYE RAMANI:Uvamizi wa Ukraine: Shambulio la Urusi kwenye ramani
- ZELENSKY:Volodymyr Zelensky: Mfahamu rais wa Ukraine aliyeacha umaarufu wake wa TV na kuingia kwenye siasa
- PUTIN:Vladimir Putin: Rais wa Urusi aliyeagiza shambulio Ukraine

'Vita huunganisha watu'

Maoni ya mwandishi wa BBC, Oleg Karpyak, mjini Kyiv
Watu wamekimbilia kwenye vituo vya treni kwa kuogopa makombora, treni inaendeshwa kwa saa moja hadi mbili, nusu ya treni haina watu.
Waandamanaji wa leo wanazungumza Kirusi, wakishutumu serikali ya Ukraine kwa kusababisha madhara.
Mwandishi huyo alikutana na Tamara, mwanamke anayezungumza lugha ya taifa ya Ukraine na Kirusi, na akaelezea hisia zake kuhusu msaada na umoja wa watu wa Ukraine.
Alisema mumewe anatoka Kharkiv, mji pekee unaozungumza Kirusi mashariki mwa Ukraine, na kwamba makombora ya Kirusi yamepiga Kharkiv leo.
Mwandishi huyo aliongeza kuwa alimuona kijana akiwa amebeba bunduki aina ya AK-47 akiwa amefungwa kitambaa cha manjano kwenye mkono wake wa kulia - ishara kwamba alikuwa mmoja wa watu waliojitolea kushiriki katika mapigano hayo.
Artem, ambaye anazungumza Kirusi, alisema hakuwa na matatizo yoyote na Ukraine kabla ya uvamizi wa Urusi.
"Vita vimeunganisha watu kama zamani," Artem alisema.

Mgogoro mkubwa wa wakimbizi
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) linasema watu nusu milioni sasa wameikimbia Ukraine na kuelekea nchi jirani.
Mwandishi wa BBC Jeremy Bowen anaona watu wakiwa kwenye foleni ndefu kuingia Poland.
Alisema baadhi ya watu wanatembea kwa miguu huku wengine wakiwa kwenye magari, na watu wengi ni watoto.
Zaidi ya watu 100,000 pia wamekimbia makazi yao ndani ya Ukraine, kulingana na Umoja wa Mataifa.

Viwango vya riba vya Urusi vyaongezeka mara mbili
Urusi imepandisha ushuru wake kwa asilimia 20 huku vikwazo walivyowekewa vikiathiri uchumi wa nchi hiyo.
Thamani ya sarafu ya nchi hiyo imeshuka, huku kukiwa na misururu mirefu katika mashine za kutolea pesa pamoja na baadhi ya maduka ya vyakula.
"Hatuna dola, tuna rubles za Kirusi lakini sipendezwi," mwanaume mmoja katika benki ya Urusi aliambia BBC.
Licha ya kuzorota kwa uchumi, Kremlin inasema Urusi "inaondoa" vikwazo vya kiuchumi.

Vitendo vya kukataliwa, ujasiri na vikwazo
Wakati uvamizi wa Urusi nchini Ukraine ulipoanza, idadi kubwa ya raia wa Ukraine walionekana kwenye mitandao ya kijamii wakipinga jeshi la Urusi.
Baadhi ya waliokuwa na hasira walikabiliana na askari huku wengine wakijaribu kuzuia vifaru kuingia maeneo yenye watu wengi.
Wengine walichukua silaha kujaribu kusaidia kutetea nchi yao.
Mmoja wa wabunge hao Lesia Vasylenko aliIambia BBC kwamba baba mkwe wake alimfundisha kutumia bunduki aina ya AK-47.













