Trump alisuta bunge la Marekani kwa kusitisha hatua za kijeshi dhidi ya Iran: Hii ilikuwa ni kumsaidia adui
Rasi wa Marekani Donald Trump ameandika ujumbe mtandaoni kukosoa hatua ya bunge la seneti la nchi hiyo kuidhinisha mswada wa kudhibiti mamlaka yake ya vita. Trump alisema:
''Nilikuwa nimeiweka Iran chini ya shinikizo kali, walikuwa tayari kurudi nyuma, na walikuwa karibu kutupatia chochote. Kwa mara ya kwanza katika miongo kadhaa, Iran iliiheshimu sana Marekani na rais wake, (mimi). Lakini Seneti ya Marekani iliamua wakati mbaya zaidi, kupiga kura isiyo na maana ya Sheria ya Nguvu za Kivita, kutuma ujumbe kwa taifa linalofadhili ugaidi kwamba Marekani haijafurahishwa na hatua ninazochukua dhidi yao na kwamba lazima niache. Wamempa msaada adui. Warepublican wanne walipiga kura na Democrats, na sasa Iran inawauliza wawakilishi wangu, 'Kura hii inamaanisha nini?' Maseneta hawa wamefanya kazi yangu kuwa ngumu zaidi, lakini sitarudi nyuma, hata iweje, kwa sababu hivyo ndivyo ninavyofanya kazi kila wakati!"



















