Kwanini China iko tayari kupigana vita na ulimwengu ili kutetea bahari yake ya kusini mwa China?

Iliyochapishwa

Bahari ya Kusini mwa China imekuwa kwenye mjadala kwa miaka kadhaa iliyopita. China inadai kuwa eneo hilo ni lake na liko kwenye mradi mkubwa wakijenga kisiwa katika eneo hilo.

Ikiwa suala hilo lilikuwa la China tu, hakukuwa na mzozo, lakini nchi zinazozunguka Bahari ya Kusini mwa China pia zinadai sehemu zao kwenye sehemu ya eneo hilo. Wakati huo huo, Marekani na nchi za Magharibi, haswa NATO, wameelezea wasiwasi wao mara nyingi kuhusu mradi wa China katika eneo hili.

Wataalam wanaamini kuwa mzozo katika Bahari ya Kusini mwa China ni zaidi ya mzozo kati ya baadhi ya nchi. Kuingilia kwa China hapa pia ni ishara ya mabadiliko mapya katika ramani ya ulimwengu na inaweza kuwa sababu ya mzozo mkubwa katika nyakati zijazo.

Kwanini bahari ya kusini mwa China ni eneo muhimu kwa China? Na ni kwasababu gani China inataka kulidhibiti eneo hili kwa gharama zozote?

Katika mwaka wa 2018, wakati ndege ya jeshi la anga la Marekani ilipofika karibu na Bahari ya Kusini ya China, jeshi la China liliionya irudi. Kulikuwa pia na timu ya BBC kwenye ndege hii. Timu hii pia ilikwenda Bahari ya China Kusini miaka michache iliyopita. Timu ilishuhudia China ikilijenga haraka eneo hilo

Kuna karibu visiwa vidogo na vikubwa 250 katika Bahari ya Kusini ya China. Karibu visiwa vyote havina watu. Baadhi ya hivi vingekuwa vimezama ndani ya maji kwa miezi mingi kutokana na mawimbi, wakati vingine vikiwa vimezama kabisa. Sehemu hii iko kati ya Bahari ya Hindi na Bahari ya Pasifiki na imezungukwa na China, Taiwan, Vietnam, Malaysia, Indonesia, Brunei na Ufilipino. Mbali na Indonesia, nchi nyingine zote huita sehemu ya eneo hilo kuwa yao wenyewe.

Fang Jung, mtaalamu wa masuala ya mahusiano ya kimataifa ya China, katika Chuo Kikuu cha kitaifa cha Australia, amesema kuwa China inadai kuwa miaka elfu mbili iliyopita, mabaharia na wavuvi waligundua eneo hili, waliliita jina na kuanza kufanya kazi hapa.

Dkt.Fang Jung anasema, "Wakati wa Vita vya pili vya dunia, eneo lote la Bahari ya Kusini mwa China lilikaliwa na Japan kuanzia mwaka 1939 hadi 1945. Baada ya kushindwa kwa Japan, China ilituma meli zake za kivita za majini hapa kuudhibiti tena."

Bahari ya kusini mwa China

China imesema kuwa nchi zilianza kuonesha nia na bahari ya kusini mwa China walipoanza uchunguzi wa mafuta katika eneo hilo.

Dkt.Fang Jung anasema kuwa dai hili la China linaonekana kuwa kweli kwa kiwango fulani kwa sababu hakuna mtu mwingine aliyepinga madai ya China kabla ya miaka ya 1970.

Anasema, "Moja ya hoja za China imekuwa kwamba kihistoria imekuwa ikidai eneo hili, wakati sivyo ilivyo kwa nchi nyingine. Leo, ikirudisha eneo lake lililopotea.Serikali ya China inaiona kuwa ni muhimu sana katika mchakato wa ujenzi wa taifa la kisasa. "

Kwa hivyo kipande hiki cha bahari ni muhimu kwa China kwa sababu tu kihistoria imeikiita yake au kuna sababu yoyote thabiti ya kiuchumi nyuma yake?

Profesa Clive Schofield, mkurugenzi wa zamani wa Kituo cha Kitaifa cha Australia cha Rasilimali na Usalama wa Bahari, anasema China na nchi nyingine zinaanza kugundua kuwa mahali hapa panaweza kudhihirika kuwa muhimu kiuchumi na kimkakati.

Anasema, "Maslahi ya nchi nyingi yameongezeka katika eneo hili kwa sababu wanaamini kuwa wanaweza kupata hazina za mafuta ghafi mahali hapa. Hatahivyo, nina shaka kuhusu uwezekano wa kuwa na hazina hapa."

Hakuna taarifa ya wazi kuhusu ni kiasi gani mafuta yanaweza kupatikana katika eneo hili. Ingawa Profesa Clive anasema kwamba kuna aina tofauti ya utajiri hapa ambayo ni muhimu kwa China. Kuna aina elfu thelathini za samaki hapa. Na kwa upande wa uzalishaji wa samaki, kinazalisha asilimia 15 ya samaki ulimwenguni na kazi hii inafanywa kutoka Bahari ya Kusini ya China.

Anasema, "Ushindani wa rasilimali za bahari uko juu sana katika Bahari ya Kusini mwa China na haiwezekani hata kidogo kutengeneza mazingira ya mzozo kati ya nchi ili rasilimali hizi ziende kwenye eneo hili."

Kwa sababu ya mvutano huu kuongezeka katika eneo hili na kukabiliana nayo, China inataka kuimarisha msimamo wake hapa.

Kesi ya kupendeza sana ilitokea Scarborough Shoal hapa mnamo 2012 wakati China ilipozuia wavuvi kutoka Ufilipino kuvua hapa. Kwa mujibu wa Ufilipino, eneo hili ni sehemu ya eneo lake maalumu la Uchumi. Mzozo uliongezeka na Ufilipino iliwasiliana na Mahakama ya Kimataifa ya Haki.

Mahakama iliundwa chini ya mkutano wa 'Sheria ya Bahari' ya Umoja wa Mataifa kuchunguza suala hilo. Mahakama hiyo ilitoa uamuzi huo kwa niaba ya Ufilipino. Mahakama ilisema "China kihistoria haikuwa na msingi wa kisheria kudai rasilimali ndani ya maeneo ya baharini."

Profesa Clive anasema kuwa jibu la China katika suala hili lilikuwa tofauti. Kujibu uamuzi wa mahakama, China ilisema kuwa uamuzi huu ni kipande cha karatasi tu ambacho kinapaswa kutupiliwa mbali na suala hilo linapaswa kutatuliwa kupitia mazungumzo.

Profesa Clive anasema, "China haikuhudhuria kikao hicho na ilikataa kukubali mamlaka ya mahakama hiyo. Na kwa tofauti hii,kati ya nchi zilizo karibu na Bahari ya Kusini ya China na maoni ya China Uwezekano wa mvutano ulianza kuongezeka.

Lakini sio kwamba mvutano kati ya nchi kuhusu Bahari ya Kusini ya China umekuwa tu juu ya haki za uvuvi au rasilimali nyingine. Bahari ya Kusini mwa China pia ni moja wapo ya njia za baharini zilizo na pilika nyingi zaidi ulimwenguni.

Kwa mujibu wa makadirio ya Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Biashara na Maendeleo, asilimia 80 ya biashara duniani hufanywa na bahari na karibu theluthi moja ya biashara hii hupita Bahari ya Kusini ya China.

Kulingana na Kituo cha Mafunzo ya Mkakati na Kimataifa, njia hii inazalisha biashara ya karibu dola trilioni 3.37 za Marekani kila mwaka.

Katika hali hiyo, ni kawaida kwa nchi nyingi kupendezwa nayo. Profesa Clive anasema, "Wataalamu wengi wanaamini kuwa madai ya China kuhusu umiliki wa eneo hili yanahusiana moja kwa moja na kupata udhibiti wa biashara kupitia hapa."

Marekani pia inavutiwa sana na eneo hili kutochukuliwa na nchi yoyote. Pamoja na meli za mavalry, meli zake za kivita pia hupitia eneo hili mara kwa mara. Marekani inaiita "uhuru wa kusafiri" lakini China inaiita njia yake ya shari.

Mike Pompeo pia aliweka wazi hili wakati wa uongozi wake kama Waziri wa Mambo ya Nje wakati huo. Alisema, "Bahari ya Kusini mwa China sio nyongeza ya himaya ya China baharini. Tunaunga mkono viongozi wa nchi za ASEAN kwamba mzozo katika eneo hili unapaswa kutatuliwa kwa mujibu wa sheria za kimataifa."

Lakini matarajio ya China katika eneo hili sio kwa masilahi ya kiuchumi tu. Peter Jenning, mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Sera ya Mkakati ya Australia, anakubali kwamba imeongeza kwa kiasi kikubwa shughuli zake za kijeshi katika eneo hili na kwa sababu hii wasiwasi wa majirani zake umeongezeka.

China ilituma tena makombora katika Bahari ya Kusini mwa China

Mnamo 2013, China iliunda eneo la kitambulisho cha Ulinzi wa Anga (ADIZ) katika Bahari ya Mashariki ya China. Inataka pia kuunda ukanda katika Bahari ya Kusini ya China ili iweze kuitwa eneo lisiloingilika.