Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ndege za kivita za Uigereza zazizuia ndege 2 za Urusi katika pwani ya Uskochi
Ndege za kivita za Uingereza zimezizuia ndege mbili za Urusi katika pwani ya Uskochi , maafisa wakuu wa ulinzi nchini humo wamesema.
Wizara ya ulinzi imesema kwamba ndege hizo za RAF zilizuiwa baada ya kuingia katika anga ya kimataifa inayodhibitiwa na Uingereza .
Ndege hizo za Urusi zilitambuliwa kama TU -142 Bear F maritime reiconessance na ndege ya kivita ya kukabiliana na manuwari.
Ndege hizo za jeshi la Uingereza kwa sasa zinafanya kazi kutoka kambi ya Leuchars huko Fife.
Msemaji wa wizara ya Ulinzi alisema kwamba udhibiti wa maeneo hayo ulizifanya ndege nyengine kupita kwa usalama ikiwemo ndege za abiria.
Kambi hiyo ya zamani ya wanajeshi wa Uingereza RAF kwa sasa ni kituo cha jeshi la Uingereza , kambi inayotumika na walinzi wa ufalme wa Uskochi.
Hatahivyo wanajeshi hao wameondoka kwa muda kutoka kambi hiyo iliopo Lossiermouth huku barabara ya ndege ikifanyiwa ukarabati..