Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwamuzi wa soka wa Nigeria Joseph Ogabor afungiwa mwaka mmoja
Shirikisho la soka Afrika, (Caf) imemfungia mwamuzi wa Nigeria, Joseph Ogabor kutojishughulisha na soka kwa mwaka mmoja kwa kosa la '' kujaribu kufanya udanganyifu kwenye mechi''.
Caf imesema uamuzi huo umekuja baada ya uchunguzi kufanyika na kupata ushahidi ambao uliwasilishwa kwa maafisa wa mechi hiyo nchini Afrika Kusini, ambao Ogabor aliwataka kutoa ''usaidizi wa kiufundi'' kwa timu ya Nigeria.
Plateau United ilitahadharishwa kujiepusha na vitendo vya ukarimu kama kutoa zawadi ambavyo vilionyesha kuwa na nia ya kutoa tafsiri mbaya.
''Shirikisho la soka la Afrika Kusini wameamriwa kuomba radhi kwa shirikisho la soka la Nigeria baada ya uchunguzi kuthibitisha kuwa hakuna ushahidi wa afisa yeyote wa shirikisho hilo kujihusisha na rushwa ya kiasi cha dola za Marekani 30,000''. ilihitimisha taarifa hiyo.