''Safari ya kumtafuta baba yangu''

Iliyochapishwa

Nchini Kenya, zaidi ya theluthi moja ya watu hukua katika familia za mzazi mmoja. Africa Eye inafuatilia safari ya kibinafsi ya mwanahabari Namukabo Werungah, ambaye hajawahi kumjua baba yake na ameamua kutafuta sehemu hii ya utambulisho wake. Hajui ikiwa yu hai au amekufa, lakini harusi yake inakaribia, ameamua kuwa ni wakati wa kujua historia yake. Je, atampata mwanaume ambaye alitakiwa kumwita baba? Na ikiwa atafanya hivyo, atamtaka maishani mwake?