Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Moja kwa moja, Marekani yapunguza vikwazo vya mafuta huku Iran Ikikanusha madai ya Vance kuhusu wakaguzi wa nyuklia

Iran imekanusha madai ya Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, kwamba itaruhusu wakaguzi wa nyuklia kurejea nchini humo, baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Lizzy Masinga

  1. Mwanamke afariki baada ya gari la Tesla kutoka barabarani na kugonga nyumba

    Maafisa wa usalama wa usafiri nchini Marekani wanafanya uchunguzi kuhusu ajali mbaya iliyohusisha gari la Tesla lililotoka barabarani na kugonga nyumba.

    National Highway Traffic Safety Administration ilitangaza Jumatatu kuwa imefungua uchunguzi rasmi kuhusu ajali hiyo iliyotokea tarehe 19 Juni katika jimbo la Texas, ambapo gari la Tesla lilitoka nje ya barabara na kugonga nyumba ya makazi.

    Kwa mujibu wa polisi wa eneo hilo, mwanamke aliyekuwa ndani ya nyumba hiyo alipata majeraha mabaya na baadaye alifariki kutokana na ajali hiyo.

    Polisi walisema kuwa dereva hakuwa chini ya ushawishi wa pombe au dawa za kulevya. Dereva huyo aliwaambia wachunguzi kwamba gari lilikuwa likitumia mfumo wa usaidizi wa uendeshaji wa kiotomatiki wakati ajali ilipotokea.

    Msemaji wa NHTSA alisema:

    “Wakala umeanzisha uchunguzi maalumu kuhusu ajali hii.”

    Kwa upande mwingine, mwakilishi wa Tesla, kampuni inayomilikiwa na bilionea wa Marekani Elon Musk, hakujibu maombi ya kutoa maoni kuhusu tukio hilo au uchunguzi unaoendelea.

    Ajali hiyo ilitokea takribani saa 2:00 usiku kwa saa za eneo hilo siku ya Ijumaa.

    Ripoti ya polisi inaeleza kuwa dereva wa gari aina ya Tesla Model 3 “alishindwa kudhibiti gari akiwa katika njia ya kupita magari mengine, akatoka nje ya barabara na kugonga nyumba ya makazi.”

    Uchunguzi huo unalenga kubaini sababu halisi ya ajali hiyo na iwapo mfumo wa usaidizi wa uendeshaji wa gari ulikuwa na mchango wowote katika tukio hilo.

    Unaweza kusoma;

  2. Pesa za kikombozi zasababisha kifo cha Nancy Guthrie

    Noti liyotumwa kama kikombozi siku chache baada ya mama yake mtangazaji wa Marekani Savannah Guthrie kutekwa nyara kutoka nyumbani kwake kudai kuwa amefariki, kulingana na wachunguzi.

    Ujumbe huo ulikuwa kati ya mbili zilizoelekezwa kwa familia ya Nancy Guthrie na kutumwa kwa vyombo vya habari siku chache baada ya kutekwa nyara kwake Januari.

    Wa kwanza alidai mamilioni ya bitcoin ili aachiliwe, lakini wa pili alisema kuwa alikuwa amekufa, kulingana na vyanzo vilivyotajwa na vyombo vya habari vya Marekani.

    Barua kutoka kwa watekaji nyara inasemekana ilisema hawakuwa na nia ya kumuua na ilijumuisha kuomba msamaha kwa familia.

    Idara ya Polisi Kaunti ya Pima ilikataa kutoa maoni yake kuhusu yaliyomo kwenye maelezo hayo, lakini ilisema uchunguzi "unaendelea".

  3. Iran yakanusha madai ya Vance kuhusu wakaguzi wa nyuklia

    Iran imekanusha madai ya Makamu wa Rais JD Vance kwamba itawaruhusu wakaguzi wa nyuklia kurejea nchini, baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo kati ya Washington na Tehran kufikia makubaliano ya mwisho ya kumaliza vita.

    Kufuatia mazungumzo nchini Uswizi, Vance alisema majadiliano na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) yanaweza kuzuru nchi hiyo "hata leo".

    Lakini wizara ya mambo ya nje ya Iran iliambia vyombo vya habari vya serikali kwamba Tehran haikutoa "ahadi mpya" kuhusu ukaguzi wa nyuklia.

    Hayo yamejiri baada ya Marekani kutangaza kuwa imeiondolea Iran vikwazo kwa muda ili kuiwezesha kuuza mafuta kwa dola za Marekani kwa mara ya kwanza katika miongo kadhaa.

    Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa Jumatatu, wapatanishi wa Qatar na Pakistan walisema kwamba baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo katika mjini Bürgenstock Uswizi, Marekani na Iran zilikubaliana "njia ya kuelekea kufikia makubaliano ya mwisho ndani ya siku 60".

    Vance alielezea mazungumzo hayo kuwa "na tija".

    Makamu wa rais wa Marekani alisema timu hizo zilijadili kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz na "kumaliza mzozo kwa usitishaji mapigano wa kikanda".

    Soma pia:

  4. Lionel Messi mfungaji bora wa muda wote kwenye Kombe la Dunia

    Nahodha wa Argentina, Lionel Messi, alifunga mabao mawili katika mechi ya pili ya Kundi J ya Kombe la Dunia dhidi ya Austria, na kuiongoza Argentina katika ushindi wa mabao 2-0.

    Messi, ambaye pia alikosa penalti mapema katika mchezo huo, alifunga mabao yake katika dakika ya 38 na dakika ya 90+5, na kuhakikisha timu yake inapata ushindi muhimu.

    Nyota huyo wa Argentina, ambaye atatimiza miaka 39 tarehe 24 Juni, anaendelea kuweka historia kama mfungaji bora wa muda wote katika fainali za Kombe la Dunia, akiwa amefunga mabao 18 katika mechi 28 alizocheza.

    Baada ya Messi katika orodha hiyo ni Miroslav Klose wa Ujerumani na Kylian Mbappe wa Ufaransa, ambao kila mmoja ana mabao 16. Nafasi inayofuata inashikiliwa na Ronaldo wa Brazil mwenye mabao 15.

    Ushindi huo umeimarisha nafasi ya Argentina katika Kundi J huku Messi akiendelea kuonesha ubora wake licha ya umri wake mkubwa katika soka la kimataifa.

    Lionel Messi, ambaye amefunga mabao yote matano ya Argentina katika Kombe la Dunia 2026 hadi sasa, pia amesawazisha rekodi ya kufunga mabao katika mechi sita mfululizo za mashindano hayo.

    Messi sasa anajiunga na nyota wengine wawili wa soka waliofanikiwa kuweka rekodi hiyo: Just Fontaine wa Ufaransa na Jairzinho wa Brazil, ambao walifanya hivyo katika Kombe la Dunia la mwaka 1958.

    Unaweza kusoma;

  5. Pacha waoa pacha katika harusi ya pamoja Nigeria

    Wakati wageni walipokusanyika katika kanisa jijini Ibadan kusini-magharibi mwa Nigeria mwishoni mwa wiki, walijua walikuwa wakishuhudia tukio la kipekee.

    Ndugu mapacha wawili wa kiume, Taiwo na Kehinde Oguntoye, walifunga ndoa na dada mapacha wawili wa kike, Taiwo na Kehinde Adediran, katika sherehe ya pamoja iliyojaa furaha.

    Jamii ya Wayoruba, ambao ni wengi eneo la kusini-magharibi mwa Nigeria, inajulikana kwa kuwa na kiwango cha juu cha kuzaliwa kwa mapacha. Hata hivyo, si jambo la kawaida kuona jozi mbili za mapacha wakifunga ndoa kwa wakati mmoja.

    Akizungumza siku ya harusi yake, Taiwo Oguntoye alisema:

    "Tunawafahamu mapacha wengi, lakini ndoa hii inaonekana kama ilipangwa na Mungu. Siku zote tumekuwa na ndoto ya kuoa mapacha."

    Aliongeza kuwa yeye na mke wake wanaomba wapate watoto mapacha katika watoto wao wa kwanza na wa pili, kwani hilo ndilo tamanio lao kubwa.

    Katika utamaduni wa Wayoruba, mapacha huchukuliwa kuwa baraka maalumu. Majina yao pia hupewa kwa kufuata mila za kitamaduni. Mtoto anayezaliwa kwanza huitwa Taiwo, ambalo maana yake ni "yule anayekwenda kuujaribu ulimwengu", huku anayezaliwa baadaye akiitwa Kehinde, likimaanisha "yule aliyekuja baada yake".

    Tukio hilo limevutia watu wengi kutokana na nadra yake na umuhimu wake wa kitamaduni katika jamii ya Wayoruba.

  6. Trump: Sehemu ya fedha za Iran zimeachiwa na zitatumika kununua chakula

    Rais wa Marekani, Donald Trump, ametangaza kuachiliwa kwa sehemu ya kwanza ya mali za Iran zilizokuwa zimezuiwa, akisema kuwa Iran itatumia fedha hizo kununua chakula kutoka kwa wakulima wa Marekani.

    Abdolnaser Hemmati, mkuu wa Benki Kuu ya Iran, pia amethibitisha kwa njia isiyo ya moja kwa moja taarifa hizo. Amesema kuwa dola bilioni 6 za kwanza zilizofunguliwa zitatumika kununua chakula na dawa kulingana na makubaliano yaliyofikiwa kati ya Tehran na Washington mwaka 1402 kwa kalenda ya Iran.

    Hemmati aliongeza kuwa dola bilioni 6 za pili, baada ya kuachiliwa, zitatumika kununua bidhaa ambazo hazijafungwa na vikwazo vya kimataifa.

    Wakati huo huo, Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, aliondoka kuelekea Muscat saa moja baada ya kurejea kutoka Uswisi.

    Ziara hiyo imeelezwa kuwa ni kwa ajili ya “maandalizi ya Iran ya usimamizi wa Mlango-Bahari wa Hormuz” pamoja na kuimarisha ushirikiano wa pande mbili.

    Aidha, Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, anatarajiwa kufanya ziara nchini Pakistan katika siku zijazo kama sehemu ya juhudi za kidiplomasia na kuimarisha mahusiano ya kikanda.

    Kwa ujumla, hatua hizi zinaashiria kuendelea kwa mazungumzo na ushirikiano kati ya Iran, Marekani na nchi washirika wa eneo hilo, huku masuala ya uchumi, biashara na usalama wa njia ya bahari ya mlango bahari wa Hornuz yakipewa kipaumbele.

    Unaweza kusoma;

  7. Marekani yapunguza vikwazo vya mafuta huku Iran Ikikanusha madai ya Vance kuhusu wakaguzi wa nyuklia

    Iran imekanusha madai ya Makamu wa Rais wa Marekani, JD Vance, kwamba itaruhusu wakaguzi wa nyuklia kurejea nchini humo, baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo kati ya Washington na Tehran yenye lengo la kufikia makubaliano ya mwisho ya kumaliza vita.

    Baada ya mazungumzo yaliyofanyika nchini Uswisi, Vance alisema kuwa majadiliano na Shirika la kimataifa la nguvu za Atomiki (IAEA) kuhusu ukaguzi wa nyuklia yanaweza kuanza “hata leo”.

    Hata hivyo, Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran iliambia vyombo vya habari vya serikali kwamba Tehran haijatoa “ahadi mpya yoyote” kuhusu kuruhusu ukaguzi wa nyuklia.

    Wakati huo huo, Marekani imepunguza kwa muda baadhi ya vikwazo vyake dhidi ya Iran, na kuiruhusu kuuza mafuta kwa kutumia dola za Marekani kwa mara ya kwanza katika miongo kadhaa.

    Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa Jumatatu, wapatanishi Qatar na Pakistan walisema kuwa baada ya duru ya kwanza ya mazungumzo katika mji wa mapumziko wa Bürgenstock nchini Uswisi, Marekani na Iran zilikubaliana kuhusu mwelekeo wa kufikia makubaliano ya mwisho ndani ya siku 60.

    Vance alieleza kuwa mazungumzo hayo yameweka “msingi mzuri sana” wa maendeleo ya baadaye.

    Makamu huyo wa Rais pia alisema kuwa pande hizo zilijadili kufunguliwa tena kwa mlango bahari wa Hormuz pamoja na hatua za kuzuia migongano katika utekelezaji wa usitishaji mapigano wa kikanda.

    Msamaha wa vikwazo wa siku 60 uliotolewa na Wizara ya Fedha ya Marekani Jumatatu umeondoa kwa muda baadhi ya vipengele muhimu vya vikwazo vya muda mrefu vya Washington dhidi ya Iran, ambavyo kwa miaka mingi vimekuwa vikidhoofisha uchumi wa Tehran.

    Unaweza kusoma;

  8. Habari za asubuhi, karibu katika taarifa zetu hii leo