Tetesi za Soka Ulaya Jumapili: Alvarez yuko tayari kuhamia Arsenal

Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Mshambuliaji wa Argentina Julian Alvarez, 26, yuko tayari kujiunga na klabu ya Arsenal, licha ya hapo awali kupendelea kuhamia Barcelona. Uhusiano wake na Atletico Madrid umeanza "kuzorota". (Standard)

Kocha wa Arsenal Mikel Arteta na mkurugenzi wa michezo wa klabu hiyo Andrea Berta wameendelea kuwasiliana mara kwa mara na Alvarez katika kipindi hiki cha usajili. Ingawa bado anapendelea kuhamia Barcelona, lakini sasa anaiona Arsenal kama chaguo mbadala. (AS)

Tottenham ina matumaini ya kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Misri Omar Marmoush, 27, kutoka Manchester City wiki ijayo. (Fabrizio Romano)

Mshambuliaji wa England Ollie Watkins ameiambia Aston Villa kwamba anataka kuondoka klabuni hapo, huku Al-Hilal ya Saudi Arabia ikiwa interested katika kumsajili. (GiveMeSport)

Beki wa kushoto wa Barcelona Alejandro Balde, 22, ameamua kuondoka klabuni hapo, huku Manchester United ikitaka kumsajili. Hata hivyo, ripoti nyingine zinasema Balde anataka kuendelea kupigania nafasi yake Barcelona. (Metro via Jijantes, Mundo Deportivo)

Real Madrid haitaki kumuuza mshambuliaji wa Brazil Endrick, 20, kwenda Liverpool, lakini iko tayari kumuuza mshambuliaji wa Hispania Gonzalo Garcia, 22, kwenda Fulham katika dirisha hili la usajili. (Football Insider)

Chelsea imekataa ofa ya mkopo kutoka Roma kwa ajili ya mshambuliaji wa England Under-21 Jamie Bynoe-Gittens, 22. (Talksport)

Tottenham imemuweka kiungo Pape Matar Sarr, 23, kwenye orodha ya wachezaji wanaoweza kuuzwa, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Senegal akitarajiwa kujiunga na Galatasaray. (Sacha Tavolieri via Teamtalk)

Besiktas imewasilisha ofa kwenda Newcastle United kwa ajili ya kumsajili kiungo wa England Joe Willock, 27, ambaye ni miongoni mwa nyota wanaosakwa na klabu hiyo katika dirisha hili la usajili. (Fabrizio Romano)

Liverpool imepata matumaini katika jitihada zake za kumsajili mshambuliaji wa Paris St-Germain Bradley Barcola, 23, na mshambuliaji wa Senegal Ibrahim Mbaye, 18, baada ya wachezaji hao wawili kutokuwamo katika kikosi cha PSG kilichocheza dhidi ya Rennes Jumapili. (Standard via RMC)

Liverpool bado haijaamua kama itamtoa kwa mkopo mshambuliaji wa England U-21 Jayden Danns, 20, baada ya kupona majeraha. (Liverpool Echo)