Chile yafunga ubalozi wake nchini Iran
Serikali ya Chile imetangaza kuwa itafunga ubalozi wake nchini Iran mwisho wa mwezi huu wa Agosti, lakini inasisitiza kuwa uamuzi huo hautavuja uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Chile imesema kuwa baada ya kufungwa kwa ubalozi huo mjini Tehran, masuala ya kibalozi ya nchi hiyo yatasimamiwa kupitia ubalozi mdogo wa Chile mjini Ankara, mji mkuu wa Uturuki.
Wizara hiyo ilitaja sababu za uamuzi huo kuwa ni marekebisho ya kiutendaji na kuweka vipaumbele katika rasilimali ili kufanikisha malengo ya sera ya kigeni ya serikali, pamoja na hatua za tahadhari zinazohusiana na hali ya usalama katika eneo la Mashariki ya Kati.
Uamuzi huo ulitangazwa wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Chile, Francisco Pérez Macena, akihitimisha ziara rasmi nchini China, ambayo ni mshirika mkuu wa kibiashara wa Chile.
Rais wa Chile mwenye msimamo wa mrengo wa kulia, José Antonio Caste, ambaye amekuwa madarakani tangu mwezi Machi, amedumisha misimamo inayolingana na ile ya utawala wa Trump.
Hata hivyo, baadhi ya maafisa wa utawala wake wametilia shaka mbinu inayotumiwa na Marekani katika uhusiano wake na Amerika ya Kusini katika wiki za hivi karibuni.