Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Kombe la Dunia 2018: Ubelgiji 3-2 Japan

Kombe la Dunia 2018: Ubelgiji 3-2 Japan

Moja kwa moja

  1. Jonathan Dos Santos aingia Mexico, 55' Brazil 1-0 Mexico

    Ni mabadiliko ya kutafuta bao la kusawazisha baada ya Brazil kuchukua uongozi!

  2. Herrera nje ya Robo fainali kikosi cha Mexico!, 55' Brazil 1-0 Mexico

  3. Neymar adumisha nyota yake!, 54' Brazil 1-0 Mexico

    Mchezaji wa bei ya juu zaidi duniani amedhihirisha ni kwa nini PSG ililipa Euro Milioni 200 kumsaini!

    Bao lake limeiweka Brazil mbele!

  4. Neyyyyyyymar hadi ndani!, Brazil 1-0 Mexico

  5. Tatizo sio Neymar, Muda wa mapumziko.

    Neymar ametengeza nafasi 14 za kufunga magoli Kombe la Dunia kufikia sasa.

    Hii ni baada ya kubuni nafasi 3 dhidi ya Mexico mechi inayoendelea na kuwa mchezaji mwenye kuunda nafasi zaidi Kombe hili.

    Linaudhi kufahamu kuwa Brazil imefunga mabao 5 pekee hadi sasa.

  6. Kipindi cha Kwanza kimekamilika., Baada ya kipindi cha kwanza: Brazil 0-0 Mexico

  7. Brazil yaweka matumaini kwa Gabriel Jesus, 44' Brazil 0-0 Mexico

    Gabriel Jesus tayari amemlazimu kipa wa Mexico Ochoa, kutema shuti zake.

    Je, atachukua majukumu ya Neymar na Coutinho ya ufungaji magoli?

  8. Filipe luis apokea kadi ya njano, 42' Brazil 0-0 Mexico

    Alijaribu kumzuia Carlos Vela, lakini akasababisha mkwaju wa ikabu.

    Mkwaju wa ikabu kwa Mexico!

  9. Neymar aumizwa, lakini ameinuka, 38' Brazil 0-0 Mexico

    Edison Alvarez wa Mexico amepokea kadi ya njano kwa kumkanyaga staa huyo.

    Neymar amepiga nje frikiki iliyopewa Brazil.

    Ni mpira wa kipa kwa sasa.

  10. Vela avuma na kuzua fujo Brazil, 37' Brazil 0-0 Mexico

    Mashabiki wa Arsenal wanafahamu vyema sana kwani aliwahi kuitumikia timu hiyo.

    Lakini mechini, mabeki wa Brazil wameweza kutambua uwezo wake.

  11. Kona kwa Brazil, Willian Kazini., 34' Brazil 0-0 Mexico

  12. Shida sio Nywele zake, ni fomu yake!, 31' Brazil 0-0 Mexico

    Neymar alikosolewa awali kwa kuwekeza kwa nywele zake, badala ya kuisaidia Brazil.

    Lakini hata baada ya kuingia kwenye mechi, bado makali yake hayajaonekana.

    Mabeki wa Mexico wamekaba kweli kweli.

  13. VVVVVeelaaaaaaaaaaa, voom juu!, 29' Brazil 0-0 Mexico

    Carlos Vela na nafasi nzuri kwenye sanduku, lakini mkwaju wake umepaa!

  14. Neymar kuwafuata Ronaldo na Messi nje ya Kombe?, 28' Brazil 0-0 Mexico

    Messi wa Argentina na Ronaldo wa Ureno kwa sasa wanatazama mechi za Kombe la Dunia tofauti na awali walipotazamwa, je, Nyota wa Brazil Neymar, ataondoka nao?

    Neymar amefunga bao moja tu Kombe la Dunia.

    Iliichukua Brazil dakika kumiliki mpira mbele ya lango la Mexico.

  15. Mexico wajenga ukuta, balaa kwa Brazil, 27' Brazil 0-0 Mexico

    Coutinho, amekatazwa. Jesus hakufanikiwa na sasa mpira unamilikiwa na Mexico.

  16. Ochoa aokoa!, 25' Brazil 0-0 Mexico

    Neymar alikaribia kuipa Brazil uongozi, lakini kipa wa Mexico amepangua!

  17. Brazil bila mbinu?, 23' Brazil 0-0 Mexico

    Andres Guardado, Carlos Vela, Hirving Lozano na Javier Hernandez 'Chicharito' wamekita kambi goli Brazil.

    Dalili za Mexico kupata bao mechini?

    Kumbuka Brazil ililazimishwa sare na Uswizi mechi yake ya kwanza.

  18. Mexico matatizo kwa Brazil, 18' Brazil 0-0 Mexico

    Usisahau kuwa waliwaliza mabingwa wa 2014, Ujerumani, mechi ya kwanza Kundi F Kombe la hili.

  19. Brazil kuwa bila Casemiro, Neymar na Coutinho robo fainali?, 17' Brazil 0-0 Mexico

    ......Watatu hao wanastahili kucheza kwa makini zaidi la sivyo, atakayepokea kadi ya njano hatoshiriki Robo fainali.

    Hilo huenda likaathiri mipango ya Brazil kuondoka na Kombe mwaka huu!

  20. Mtindo mpya wa nywele Chicharito., 11' Brazil 0-0 Mexico

    Achia mbali Neymar, kutana na Chicharito, nyota wa zamani wa Manchester United.