Hata wakongwe hawajaachwa nyuma kuhakisha kuwa wametekeza haki yao ya kupiga kura

Muungano wa upinzani nchini Kenya umepinga matokeo ya urais ambayo yamekuwa yakitangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi IEBC.

Maeneo mengi ya miji yamebaki bila watu, wengi wakielekea katika vituo vya kupigia kura kupiga kura. Mwandishi wetu Idris Situma amepiga picha hizi mjini Nakuru.







Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC amekuwa akiwahutubia wanahabari ukumbi wa Bomas.
Amesema anafahamu kwamba baadhi ya Wakenya walirauka hata kabla ya vituo kufunguliwa.
Amewahimiza wapiga kura ambao hawajafika vituoni kufanya hivyo.
Bw Chebukati amesema anafahamu kwamba katika baadhi ya vituo kumeshuhudiwa changamoto na wanaangazia kuzitatua.
Katika baadhi ya maeneo, amesema mvua kubwa ilitatiza uchukuzi na wamelazimika kutumia helikopta.
"Katika vituo vilivyochelewa kufunguliwa, tutaongeza muda wa kufunga vituo, sawia na muda uliocheleweshwa."
Wapiga kura wamekuwa wakijitokeza kwa njia mbalimbali na wakiwa wamevalia mavazi mbalimbali. Lakini utafanyaje kuonesha uzalendo? Pengine uvalie kama watatu hawa katika kituo cha Mutomo, Gatundu ambapo Rais Kenyatta anatarajiwa kupiga kura baadaye.

Upigaji kura unaendelea katika kituo cha Kosachei katika kaunti ya Uasin Gishu ambapo Naibu Rais William Ruto anatarajiwa kupiga kura yake baadaye leo.


Tume huru ya uchaguzi nchini Kenya imesema inafahamu kwamba kuna baadhi ya vituo vya kupigia kura ambavyo vilifunguliwa kwa kuchelewa.
Tume hiyo imeandika kwenye Twitter kwamba maafisa wake wanashughulikia hilo na tahakikisha hakuna mpigaji kura anayetatizika.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Katika baadhi ya vituo, kuna foleni ndefu. Mfano ni katika kituo hiki cha Kipsigis County Council mjini Kericho kama alivyoshuhudia mwandishi wa BBC Rob Wilson.
Je, wewe ni Mkenya, hali iko vipi ulipo?
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe




Raia wa Kenya waishio Tanzania wamekuwa wakipiga kura nchini Tanzania katika miji ya Dar es Salaam na Arusha.
Mwandishi wa BBC Halima Nyanza yupo katika kituo cha kupigia kura mjini Arusha ambapo ameshuhudia upigaji kura ukiendelea.



Mwandishi wa BBC Abdinoor Aden anasema mitambo ya kuwatambua wapiga kura katika kituo cha shule ya Olympic, Kibra imeanza kukubwa na hitilafu.
Shughuli ya upigaji kura imesimama kwa muda maafisa wa tume ya uchaguzi wakijaribu kutatua tatizo hilo.
Afisa msimamizi wa ucahguzi kituo hicho Aggrey Mulera amesema wanajaribu kutafuta suluhu.


Watu wa jamii ya Kalasinga hawajaachwa nyuma katika mji wa Kisumu, magharibi mwa Kenya. Mwandishi wetu Odeo Sirari amekutana na wawili hawa kwenye foleni kituo cha Ukumbi wa Aga Khan.

Mpiga kura huyu anasema hakuweza kutofautisha rangi za karatasi za kupiga kura, rangi ya karatasi za wawakilishi wa wadi na wawakilishi wa wanawake.
Rangi ya karatasi ya kupigia kura inafanana na rangi ya vifuniko vya masanduku ya kutumbukiza kura.
Rangi ya karatasi ya urais ni nyeupe na vivyo hivyo, masanduku ya kura za urais yana vifuniko vyeupe.
Ugavana rangi ni ya samawati. Kura ya seneta ni ya manjano, mbunge ni kijani kibichi na mwakilishi wa wanawake ni ya kizambarau nazo za mwakilishi wa kaunti biji.

Upigaji kura katika kituo cha kupigia kura cha Maktaba ya Garissa umechelewa kuanza. Mwandishi wa BBC Bashkas Jugsodaay anasema upigaji kura umeanza dakika chache zilizopita.

Mwandishi wetu Odeo Sirari yupo katika kituo cha Aga Khan mjini Kisumu na amewapiga piga wapiga kura hawa ambao walikuwa miongoni mwa waliopiga kwanza kituoni humo.


Upigaji kura umeanza katika kituo cha Wabungo, Kwale pwani ya Kenya na baadhi ya watu washamaliza kupiga kura.
Pichani ni mmoja wa waliopiga kura kwanza.

Shughuli ya upigaji kura imeanza katika kaunti ya Garissa, mashariki mwa Kenya. Usalama umeimarishwa.
Pichani ni maafisa wa Tume ya Uchaguzi wakijiandaa kwa upigaji kura.

Hivi ndivyo hali ilivyo kituo cha kupigia kura cha Mwabungo kaunti ya Kwale. Hapa, watu wa jamii ya Makonde watapiga kura mara ya kwanza baada ya kutambuliwa kuwa raia wa Kenya.


Vituo vya kupigia kura nchini Kenya vimefunguliwa rasmi.