Kenyatta afikisha kura 7 milioni uchaguzi wa urais Kenya
Katika matokeo ya vituo 34713 kati ya 40883:
- Uhuru Kenyatta wa Jubilee ana kura 7,092,508 (54.89%)
- Raila Odinga wa ODM ana kura 5,721,889 (44.28%)
Kura zilizoharibika kufikia sasa ni 331,846.
Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Muungano wa upinzani nchini Kenya umepinga matokeo ya urais ambayo yamekuwa yakitangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi IEBC.
Katika matokeo ya vituo 34713 kati ya 40883:
Kura zilizoharibika kufikia sasa ni 331,846.
Tume ya uchaguzi imetangaza matokeo kutoka kwa vituo 34,180 kati ya jumla ya vituo 40883 ambapo:
Kura zilizoharibika kufikia sasa ni 326,001
Matokeo yaliyotolewa kwa sasa ni kutoka vituo 34016 kati ya jumla ya vituo 40883.
Matokeo ya vituo 33274 kati ya 40883 yanaonesha:
Katika matokeo ya vituo 32218 kati ya 40883:
Tume ya uchaguzi imetangaza matokeo kutoka kwa vituo 31947 kati ya jumla ya vituo 40883 ambapo:
Kura zilizoharibika kufikia sasa ni 307,252
Afisa mkuu mtendaji wa IEBC amesema matatizo yaliyoshuhudiwa mwanzoni wakati wa kupeperushwa kwa matokeo yalitokana na kufurika kwa matokeo kutoka vituoni.
“Kulikuwa na vituo 28,000 vilivyokuwa vinawasilisha matokeo kutoka nyanjani. Upande wa kuonesha matokeo kukawa na tatizo. Lakini sasa tatizo hilo limetatuliwa kwa kiasi kikubwa. Baada ya muda, hilo halitakuwa tatizo tena,” alisema Bw Chiloba.
Afisa huyo alisema pia kwamba baada ya vituo vyenye huduma ya simu ya 3G kumaliza kutuma matokeo, vituo ambavyo vitakuwa vikituma matokeo baadaye sana itakuwa ni maandishi pekee pia Fomu za matokeo, ingawa fomu hizo zitapakiwa mtandaoni baadaye.
Alisema hata hivyo, kwa sababu maafisa wa uchaguzi huenda wakalazimika kusafiri hadi maeneo yenye huduma nzuri ya simu, upeperushaji wa matokeo hayo huenda ukachukua muda kidogo.
Tume hiyo imesema itasubiri matokeo yote, kabla ya kutangaza mshindi wa urais.
Aidha, matokeo hayo yatatangazwa kwa kufuata fomu za matokeo kutoka kwa wasimamizi wa matokeo.
Matokeo ya tume ya uchaguzi ya vituo 30937 kati ya 40883 yanaonesha:
Mgombea urais wa muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) Raila Odinga amepinga matokeo ambayo yanaendelea kutangazwa na tume ya uchaguzi nchini humo, IEBC.
Bw Odinga amewaambia wanahabari kwamba tume hiyo imekuwa ikitangaza matokeo kwenye tovuti yake bila kufuata utaratibu ufaao.
Waziri mkuu huyo wa zamani amesema kabla ya matokeo yoyote kutangazwa, IEBC inafaa kuwapa maajenti wa vyama Fomu 34A kutoka vituoni.
Amesema kwa sasa, bila kuwepo kwa fomu hizo, ni vigumu kubaini matokeo yanayopeperushwa yanatoka wapi.
"Mfumo umeacha kufanya kazi. Sasa ni mitambo inayopiga kura. IEBC wamesema kwamba hakuna chama chochote kilichopinga matokeo. Lakini vyama vitapingaje matokeo bila kujua asili yake? Ni fomu 34A pekee zinazoonesha chanzo cha matokeo," amesema.
Soma zaidi hapa: Odinga apinga matokeo ya urais
Muungano wa upinzani nchini Kenya National Super Alliance (Nasa) umesema haujafurahishwa na matokeo ambayo yanaendelea kupeperushwa na tume ya uchaguzi IEBC kwa umma.
Mmoja wa viongozi wa muungano huo Musalia Mudavadi amewaambia wanahabari kwamba tume hiyo haifai kupeperusha matokeo ya uchaguzi wa urais bila kuwepo kwa Fomu 34A.
Matokeo yaliyotangazwa kufikia sasa kutoka vituo 29209 kati ya 40883 yanaonesha Uhuru kenyatta anaongoza akiwa na kura 6044745 (55.27%) naye Bw Raila Odinga wa chama cha ODM anayeungwa mkono na Nasa wa pili akiwa na kura 4805159 (43.93%).
Tume ya uchaguzi ya Kenya muda mfupi awali, kwenye kikao na wanahabari, imesema baada ya kukutana na wadau wa vyama, iliamua kwamba itaendelea kuonesha matokeo yanavyopokelewa kutoka vituoni.
Maafisa wa tume hiyo wamesema kufikia sasa hakuna aliyepinga matokeo ambayo yamekuwa yakipeperushwa na tume hiyo.
Matokeo yanatolewa kwa kasi kiasi sasa, tayari yamebadilika sasa na hali ni kama ilivyo hapa chini. Haya ni matokeo ya vituo 29209 kati ya jumla ya vituo 40883
Kutoka kwa kura 10 840 719 zilizohesabiwa na kukubalika kufikia sasa, Uhuru Kenyatta anaendelea kuongoza kinyang'anyiro cha urais akiwa na kura 5,989,509 (55,25%) dhidi ya mpinzani wake wa karibu Raila Odinga aliye na kura 4,764,577 kufikia sasa (43,95%).
Tume imetangaza matokeo ya vituo 28172 kati ya jumla ya vituo 40883.
Katika matokeo yaliyotangazwa kufikia sasa, Uhuru Kenyatta wa chama cha Jubilee anaongoza akiwa na kura 5,743,793 (55.25%).
Mpinzani wake mkuu Raila Odinga wa muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa) ana kura 4,568,561 (43.95%).
Matokeo hayo ni ya vituo 27683 kati ya 40,883. Kura zilizoharibika zimeongezeka pakubwa na kufikia 260588.
.
Matokeo ya vituo 27016 kati ya jumla ya vituo 40883
Baada ya matokeo ya vituo 26279 kati ya vituo 40883 kutangazwa:
Uhuru Kenyatta wa Jubilee ana kura 3,336,790 (54.86%)
Raila Odinga wa ODM 2,699,908 (44.39%)
Kura ambazo zilikuwa zimeharibika kufikia sasa ni 149, 634.
Matokeo ya vituo 9,405 kati ya 40,883
Matokeo ya vituo 5455 kati ya jumla ya vituo 40883
Shughuli ya kuhesabu kura za Wakenya wanaoishi nje ya nchi, ambao wamepigia kura mjini Arusha, Tanzania imekamilika.
Raila Odinga amepata kura 92, naye Uhuru Kenyatta 68.
Ekuru Aukot wa Thirdway Alliance amepata kura 2.
Upigaji kura umekuwa ukifanyika Arusha, katika katika balozi za Kenya miji ya Dar es Salaam, Kigali, Kampala na Pretoria.