Mashabiki wa Senegal wameanza kuteka Uwanja, Ufaransa dhidi ya Senegal (22:00 EAT)
Kumekuwa na taarifa kuhusu matatizo ambayo mashabiki kutoka Senegal wamekuwa nayo kupata visa ya kutazama timu yao ikicheza Kombe la Dunia.
Lakini kuna mashabiki wengi wa Senegal, ambao tayari wanaishi Marekani, ambao wamefika New Jersey ili kuwashangilia dhidi ya Ufaransa.
Bendera za kijani, njano na nyekundu zinaonekana uwanjani
Jambo moja lipo wazi kabisa. Senegal haitakosa wapenzi wa soka usiku wa leo.

