Kocha, Julian Nagelsmann wa Ujerumani, ametaja kikosi kinachoanza cha Ujerumani kisichobadilika baada ya awali kushinda 7-1 dhidi ya Curacao.
Kai Havertz anaongoza safu yao ya ushambuliaji huku Jamal Musiala, Leroy Sane na Florian Wirtz wakimsaidia huku Deniz Undav, ambaye alifunga bao na kutoa pasi mbili za mabao akitokea bechi, ameanzia nje tena.
Kikosi cha Ujerumani: Neuer, Brown, Schlotterbeck, Tah, Kimmich, Pavlovic, Nmecha, Wirtz, Musiala, Sane, Havertz.
Wachezaji wa akiba: Rudiger, Anton, Goretzka, Leweling, Woltemade, Baumann, Gross, Beier, Stiller, Amiri, Nubel, Raum, Thiaw, Ouedraogo, Undav.
Emerse Fae amefanya mabadiliko matano kwa timu yake ya Ivory Coast huku winga wa Manchester United Amad Diallo akianza baada ya mechi iliyopita akitokea benchi akafunga bao la ushindi la dakika ya 90 dhidi ya Ecuador.
Odilon Kossounou, Ibrahim Sangare, Christ Inao Oulai na Ange Bonny pia wameanza huku Guela Doue, Seko Fofana, Elye Wahi, Nicolas Pepe na Bazoumana Toure wakitupwa benchi.
Kikosi cha Ivory Coast: Yahia Fofana, Konan, Agbadou, Kossounou, Singo, Yan Diomande, Sangare, Kessie, Diallo, Inao Oulai, Bonny.
Wachezaji wa akiba: Ousmane Diomande, Seri, Seko Fofana, Adingra, Wahi, Operi, Diakite, Kone, Doue, Pepe, Ndicka, Guessand, Lafont, Toure, Guiagon.