Marekani yadai meli mafuta ya Singapore ilishambuliwa na Iran
Maafisa wa Marekani ambao majina yao hayakutangazwa hadharani wameviambia vyombo vya habari vya Marekani kwamba shambulio la Alhamisi dhidi meli ya mafuta karibu na Mlango-Bahari wa Hormuz lilitekelezwa na Jeshi la Wanamaji la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran IRGC.
Iran haijatoa tamko lolote kuhusiana na madai haya, lakini jeshi la majini la IRGC lilionya Jumatano usiku kwamba meli yoyote itakayopitia Mlango-Bahari wa Hormuz lazima ishirikiane na vikosi vya Irani.
Siku ya Alhamisi Mamlaka mpya ya Usimamizi ya Mlango Bahari wa Hormuz ilionya kwamba "haiwezi kuzihakikishia uslama meli zinazotumia njia ambazo hazijaidhinishwa".
Mashirika ya habari ya Iran yaliandika siku ya Alhamisi usiku: "Kujibu maswali yanayoulizwa mara kwa mara, Mamlaka ya Njia ya Majini katika Ghuba ya Uajemi (PGSA) imetangaza kwamba meli zozote zinazopita nje ya mfumo uliowekwa na mamlaka hii haitapewa dhamana ya usalama na hazitapewa bima na majukumu yanayohusiana nayo.
Tangazo la shirika hilo pia lilisisitiza kuwa: "Hasara itakayotokana na usafiri kupitia njia zisizo rasmi itasimamiwa na mmiliki, mwendeshaji, na nahodha wa chombo."
Onyo la IRGC Jumatano usiku lilikuja baada ya Oman kutangaza, wakati wa ziara ya wziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio katika nchi kadhaa za Ghuba, kwamba ilikuwa imeunda njia mpya ya baharini ili kurahisisha meli kupita kwenye Mlango -Bahari wa Hormuz.
Taarifa hizo ziliungwa mkono na Bahrain, lakini huenda Jeshi la majini la IRGC "lilikerwa" na hatua kwa kuundwa kwa njia hiyo.
Hata hivyo Iran bado haijakubali rasmi au kukana kuhusika na shambulio dhidi ya meli hiyo ya Singapore.
Soma zaidi: