Matokeo ya uchaguzi Kenya 2022: Vigogo wa William Ruto walioshindwa katika maeneo yao

Naibu wa Rais William Ruto

Chanzo cha picha, Ed Ram/Getty Images

Maelezo ya picha, Naibu ya Rais William RUto
    • Author, Abdalla Seif Dzungu
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Iliyochapishwa

Licha ya naibu wa rais William Ruto kuwa katika kinyang'anyiro kikali kati yake na kiongozi wa Muungano wa Azimio Raila Odinga katika uchaguzi wa urais , Kiongozi huyo hakuponea wimbi la chama cha mpinzani wake katika maeneo mbalimbali nchini.

Jijini Nairobi wakili Maarufu mjini na mgombea wa chama cha UDA katika eneo bunge la Westlands Nelson Havi alikuwa wa kwanza kukubali kushindwa na mgombea wa Muungano wa Azimio Tim Wanyonyi.

Harvey ambaye ni wakili maarufu alikiri kushindwa wakati ambapo matokeo bado yalikuwa yakitiririka kutoka vituo mbalimbali vya eneo bunge hilo.

Alimpongeza mpinzani wake Tim Wanyonyi kwa kutetea kiti chake.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Bwana Nelson Havi ni miongoni mwa mawakili wa Ruto waliowasilisha kesi ya pingamizi dhidi ya BBI.

Wakati huohuo aliyekuwa mbunge wa eneo la Lang'ata mjini Nairobi Nixon Korir alikiri kushindwa na mcheshi maarufu nchini Felix Odiwour Jalang'o katika kiti cha ubunge cha Langata.

Jalang'o aliyewania kiti hicho kwa tikiti ya chama cha ODM alimpatia kongole bwana Korir kwa kukubali kushindwa.

William Ruto na mgombea mwenza Rigathi Gachagua

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, William Ruto na mgombea mwenza Rigathi Gachagua

Vilevile Diwani wa wadi ya Sirikwa Alfred Mutai ametangazwa mshindi wa kiti cha eneo bunge la Kuresoi Kaskazini.

Afisa wa Uchaguzi wa eneo bunge hilo Lilian Akoth alimtangaza Bw Mutai kuwa mbunge mpya Alhamisi asubuhi baada ya kujizolea kura 25,365 dhidi ya wagombea wanne.

Bw Mutai ambaye alikuwa akiwania kwa tikiti ya UDA alikuwa kwenye kinyang'anyiro kikali na Moses Cheboi-naibu spika wa bunge la Kitaifa ambaye alikuwa anawania kama mgombea huru lakini katika mrengo wa naibu rais William Ruto.

Na hayo yakijiri mbunge wa Garisaa mjini Aden Duale alishindwa kuukabili umaarufu wa kiongozi wa Azimio Raila Odinga katika eneo bunge lake baada ya Odinga kujipatia kura nyingi ikilinganishwa na alizopata Naibu wa rais William Ruto. Duale ni mshirika wa karibu sana wa Ruto.

.

IEBC ina siku saba kutangaza matokeo.

Election branding