Uchaguzi Kenya 2022: Ukweli wabainishwa kuhusu kauli za Naibu wa Rais William Ruto katika mdahalo wa urais

William Ruto at TV debate podium

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Bw Ruto alionekana akiwa peke yake katika mjadala wa TV siku ya Jumatano
    • Author, Na Peter Mwai
    • Nafasi, BBC Reality Check
  • Iliyochapishwa

Huku uchaguzi nchini Kenya ukiwa umesalia wiki chache tu, nchi hiyo imekuwa na mdahalo wa kwanza wa televisheni kwa wagombea urais katika uchaguzi huu.

Mmoja wa wagombea wawili wakuu, William Ruto, alishiriki peke yake kwa sababu mwanasiasa mkongwe - na waziri mkuu wa zamani - Raila Odinga, aliamua kutohudhuria.

Kwa sasa Bw Ruto ndiye naibu wa rais, na tumetathmini baadhi ya majibu aliyotoa kwa maswali aliyoulizwa.

'Tuna vijana milioni tano ambao hawafanyi kazi'

Madai ya Bw Ruto kwamba vijana milioni tano hawana kazi ni ya juu zaidi kuliko takwimu rasmi zinavyopendekeza.

Taarifa za hivi punde kutoka kwa ofisi ya kitaifa ya takwimu ni kwamba kuna Wakenya milioni 2.5 wenye umri wa kufanya kazi (miaka 15 hadi 64) ambao hawana kazi kwa sasa.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

William Ruto at Nariobi Pumwami road event

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Naibu wa rais William Ruto akifanya kampeni Nairobi

Haijabainika haswa ni rika gani ambalo Bw Ruto alikuwa akimaanisha, ingawa ufafanuzi rasmi wa vijana nchini Kenya ni umri wa miaka 18-34.

Kulingana na sensa ya mwaka wa 2019 nchini Kenya, kulikuwa na watu milioni 1.6 pekee wasio na ajira katika kundi hilo la umri wakati ambapo sensa ilifanywa.

Tumepata marejeleo ya zaidi ya watu milioni tano wasio na ajira na "wenye ajira ya chini" katika ripoti ya 2015 kuhusu nguvu kazi nchini Kenya.

Idadi hii ilikuwa ya rika zote (sio vijana tu), na inajumuisha sio tu wale ambao hawana kazi kabisa, lakini pia wale ambao walisema saa zao hazitoshi, ujuzi wao haukutumiwa ipasavyo au hawakuwa na tija kadri walivyoweza .

'Tuna Wakenya milioni 15 ambao leo wameorodheshwa katika CRBs [Mashirika ya kuweka taarifa za waliokosa ama kushindwa kulipa mikopo]'

Bw Ruto anarejelea hapa vyombo vinavyoidhinisha Wakenya kuwa wanastahili kupewa mikopo.

Tulipata nakala ya gazeti kutoka Februari 2021, ambayo ilitaja idadi ya chini kidogo - milioni 14 - lakini kwa akaunti za mkopo zilizodaiwa mwezi uliopita, sio watu wenye malimbikizo.

Sam Omukoko kutoka Metropol, mojawapo ya mashirika matatu ya CRB nchini Kenya, alithibitisha kwenye kituo cha runinga cha KTN News kwamba idadi hiyo ya milioni 14 mwaka wa 2021 ilikuwa ya malimbikizo ya akaunti.Hatujapata takwimu za hivi majuzi zaidi.

"Wakenya wana wastani wa takriban akaunti tano," alisema, akiongeza walikopa kutoka kwa benki, taasisi ndogo za fedha na vyama vya kuweka akiba.

Inayomaanisha kuwa idadi ya watu halisi walio na madeni inaweza kuwa ndogo sana, ikizingatiwa kuwa kwa ujumla wana zaidi ya akaunti moja.

Aidha, idadi ya malimbikizo ya akaunti huenda ikapungua katika kipindi cha miezi sita iliyopita, baada ya Rais Kenyatta kuagiza kusitishwa kwa muda kuorodhesha wale ambao wamekosa kulipa kiasi cha chini ya shilingi milioni tano za Kenya ($42,000; £34,800).

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

'...karibu asilimia 80 ya mikopo yetu yote ni ya ndani'

Naibu rais Ruto alisema nchi imekuwa ikikopa pesa zaidi kutokea ndani "hiyo ina maana kwamba pia tunadhuru biashara zetu mashinani."

"Upatikanaji wa mikopo unakuwa changamoto kubwa [na] lazima tufikirie jinsi tunapaswa kupunguza kasi ya kukopa ndani ya nchi," aliongeza.

Lakini kiasi cha deni wanalodaiwa wakopeshaji wa kimataifa, na kiasi kinachodaiwa na wakopeshaji wa ndani (kama vile benki za biashara) kimesalia takribani sawa katika miaka ya hivi karibuni, huku deni la nje kwa ujumla likiwa juu kidogo kama sehemu ya jumla ya deni.

Takwimu za Benki Kuu ya Kenya zinaonyesha kuwa mnamo Desemba 2021, wakati jumla ya deni la umma lilikuwa shilingi trilioni 8.2, deni la ndani lilikuwa trilioni 4 na deni la nje trilioni 4.2.

Ripoti ya Benki ya Maendeleo ya Afrika mwaka jana ilibainisha kuwa "idadi ya deni la nje (kama asilimia ya deni lote) ilipanda kutoka 44.5% mwaka 2013 hadi 52.5% mwaka 2020."

Ni kweli kwamba wakati wa muhula wa kwanza wa Bw Kenyatta na Bw Ruto kati ya 2013 na 2017, ukopaji wa ndani ulikuwa mkubwa kwa muda kabla ya deni la nje kuanza kuongezeka.

'Asilimia 50 ya gharama ya mafuta ni kodi'

A fuel station attendant in Nairobi

Chanzo cha picha, AFP

Bw Ruto alisema nchi inahitaji kuangalia upya ushuru wa mafuta, akiulaumu kwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kupanda kwa bei.

"Jambo la kwanza tunalohitaji kufanya ni kuangalia ushuru kwa sababu karibu 50% ya gharama ya mafuta nchini Kenya ni ushuru," alisema, akiongeza kuwa kuna ushuru aina 15 tofauti wa mafuta.

Lakini data kutoka kwa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Petroli (EPRA) inaonyesha ushuru na tozo unajumuisha takriban 40% ya gharama ya jumla ya mafuta.

Katika mapitio ya hivi majuzi zaidi ya bei ya petroli, kati ya shilingi 159.12 za Kenya kwa lita moja ya petroli, 64.06 kati ya hizo huenda kwa serikali kama kodi.

Na kodi na ushuru ni asilimia tisa - si 15. Zinajumuisha ushuru wa bidhaa, ushuru wa matengenezo ya barabara, ushuru wa usafirishaji wa mfanyabiashara na Kodi ya Ongezeko la Thamani(VAT).

Ripoti ya ziada kutoka kwa Victor Komen,Nairobi

th

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

th
Reality Check branding