Uchaguzi Kenya 2022: Fahamu namna kura zinavyohesabiwa

Raw polling data shows incumbent President Kenyatta leading comfortably - but Mr Odinga has called these results "fake"

Chanzo cha picha, AFP/GETTY IMAGES

    • Author, Asha Juma
    • Nafasi, BBC Swahili
  • Iliyochapishwa

Mamilioni ya Wakenya siku ya Jumanne walishiriki katika shughuli ya upigaji kura kuwachagua viongozi wao baada ya kampeni kali iliyotawaliwa na mijadala kuhusu gharama ya maisha, ukosefu wa ajira na ufisadi.

Lakini bila shaka yoyote jukumu kubwa lipo mikononi mwa mwananchi katika kuamua hatma ya nchi hiyo.

Na katika makala hii tunaangazia jinsi kura zinavyohesabiwa baada ya wananchi kutekeleza wajibu wao wa kujitokeza na kupiga kura kulingana na maagizo na masharti ama ya Tume Huru ya Uchaguzi (IEBC) au Katiba.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Mchakato wa kuhesabu kura baada ya kumalizika kwa upigaji kura

Vituo vya kupiga kura vimefunguliwa saa kumi na mbili asubuhi kwa shughuli ya upigaji kura na punde tu maafisa wa tume wakishasema kuwa shughuli ya kupiga kura imefungwa, atakayekuja baada ya muda huo hataruhusiwa kupiga kura lakini wale wote ambao watakuwa wapo kwenye foleni wataruhusiwa kupiga kura zao.

Afisa msimamizi huchukua hatua zifuatazo za maandalizi (kuhusiana na hesabu):

Huhesabu kura zote ambazo hazijatumika na zilizoharibika na kuzirekodi katika shajara ya kituo cha kupigia kura.

Kulingana na idadi ya kura zilizotolewa kwa kituo cha kupigia kura, hukokotoa idadi ya kura zilizotumika na kurekodi kiasi hiki kwenye shajara.

Pia kinachorekodiwa ni kura ambazo hazijatumika na zilizoharibika.

Kisha, uchaguzi mmoja baada ya mwingine, kwa utaratibu uliowekwa katika kanuni, kazi inaendelea na upangaji: Mbele ya mawakala wa chama au wagombea na waangalizi, nambari za mihuri hutambuliwa na sanduku la kura kufunguliwa.

Kura zimepangwa, kila kura itabainishwa kuwa halali, kukataliwa (maana yake ni batili) au kupingwa.

Kura inayobishaniwa inachukuliwa kuwa halali kwa madhumuni ya kutangaza matokeo katika kituo cha kupigia kura - yaani, kura itaongezwa kwa mgombea mmoja.

Mgombea au wakala wake anaweza kupinga kukataliwa kwa kura.

Katika tukio hili, afisa msimamizi atapiga muhuri kura iliyokataliwa kama ''kukataliwa kunakopingwa''.

Kura zilizo na alama ya ''kukataliwa kupingwa'' na kura zinazobishaniwa zinaweza kukaguliwa na msimamizi wa uchaguzi katika eneo bunge au kituo cha kuhesabu kura cha eneo.

Kura halali lazima zijulikane kwa uwazi na ziwe chini ya taratibu za uwajibikaji.

Baada ya upangaji kukamilika, kura za kila mgombea huhesabiwa na afisa msimamizi.

Kisha kura zisizo sahihi (zilizokataliwa, na zilizopingwa) zinahesabiwa.

Wagombea au mawakala wao wanaweza, si zaidi ya mara mbili, kutafuta kuhesabiwa upya.

Kisha afisa msimamizi atatangaza na kurekodi kwenye fomu ya matokeo:

  • Wapigakura waliojiandikisha
  • Jumla ya waliojitokeza kupiga kura
  • Kura zisizo sahihi
  • Kura zitakazopatikana kwa kila mgombea
Uhuru Kenyatta won the August poll with 54% of the vote to Mr Odinga's 45%

Chanzo cha picha, Reuters

Kisha fomu za matokeo zitasambazwa kama ifuatavyo: Nakala halisi itatumwa kwa Msimamizi wa Uchaguzi (katika Kituo sahihi cha Kuhesabu kura.)

Nakala itabandikwa katika kituo cha kupigia kura

Nakala halisi ni matokeo rasmi na inaanza safari ya kusafirishwa na Msimamizi wa Uchaguzi katika Kituo cha kuhesabu kura Taifa.

Na kufikia hatua hii, matokeo ya awali sasa yatapitishwa kwa kutumia mfumo wa kielektroniki.

Kinyume na hapo awali ambapo kura zilihesabiwa katika kituo cha kujumlisha kura, tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC), imesema kuwa kura zitahesabiwa katika kituo cha kupiga kura, ili kuondolea mbali tashwishi zozote.

Kulingana na Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC), mawakala wa vyama vya kisiasa na pia wanahabari wataruhusiwa kupiga picha nakala ya matokeo ya uchaguzi katika kituo cha kupiga kura.

"Kupiga picha nakala hiyo kutawasaidia wawaniaji kuweza kulinganisha matokeo yanayotangazwa katika makao makuu na matokeo yaliyonakiliwa katika kituo cha kupiga kura," alisema Wafula Chebukati mwenyekiti wa tume ya IEBC.

Kuhesabu kura kunafuatia mtiririko wa Rais, Gavana, Seneta, MCA, Mbunge na hatimaye Mwakilishi wa Mwanamke (sawa na jinsi masanduku ya kura yanavyopangwa kwa ajili ya kupiga kura).

Na baada ya mchakato huo kumalizika, maafisa hao wanafaa kuwasilisha fomu 34A (fomu za matokeo katika vituo vya kupigia kura).

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Fomu 34A na 34B ni nini?

Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati

Chini ya Kanuni za Uchaguzi, Fomu 34A ndiyo fomu ya kwanza inayotumiwa kujumlisha matokeo ya uchaguzi wa urais.

Hujazwa na msimamizi wa chama baada ya kuhesabu kura kwenye kituo cha kupigia kura.

Ina maelezo ya kura alizopata kila mgombea na pia inaeleza jumla ya wapiga kura waliojiandikisha katika kituo hicho, kura zilizokataliwa, zilizopingwa, zinazobishaniwa na zile halali.

Wagombea au mawakala wao basi wanatakiwa kutia saini na kuthibitisha kwamba yaliyomo kwenye fomu hiyo ni sahihi.

Kifungu cha 39 cha Sheria ya Uchaguzi kinatoa masharti kwamba kwa uchaguzi wa urais, IEBC ''itatoa kwa njia ya kielektroniki, katika fomu iliyowekwa, matokeo yaliyoorodheshwa ya uchaguzi wa rais kutoka kituo cha kupigia kura hadi kituo cha kujumlisha kura za eneo bunge na kwa Kituo cha Kitaifa cha Kujumlisha Kura."

Fomu 34A inakabidhiwa msimamizi wa eneo bunge, ambaye anajaza Fomu 34B.

Inatumika kwa ujumuishaji wa matokeo ya uchaguzi wa urais kutoka kwa vituo vyote vya kupigia kura ndani ya eneo bunge.

Juu yake imeonyeshwa nambari ya kituo cha kupigia kura, jina la kituo, idadi ya wapiga kura waliojiandikisha, nini kila mgombea alipata na idadi ya kura halali zilizopigwa.

Msimamizi wa uchaguzi wa eneo bunge anakabidhi fomu kwa mwenyekiti wa IEBC ambaye pia ndiye msimamizi wa uchaguzi wa urais.

Tangazo la matokeo litatokana na Fomu 34B tutakazopata kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi.

Maafisa wa usalama

Wakati zoezi la kuhesabu kura linaendelea, kunakuwa na maafisa wa usalama wanaohakikisha hali ni shwari kwa kila mshiriki anayefanikisha uchaguzi huo.

Kura iliyoharibika ni ipi?

Kuna sababu nyingi ambazo husababisha kura kuharibika na hivyo kutohesabiwa.

Kuu zaidi huwa ni mpiga kura kuweka alama kwa njia isiyofaa wakati wa kuchagua mgombea au chama anachokitaka.

IEBC inasema mpiga kura anatakiwa kuweka "alama kwenye nafasi iliyotengwa kwa jina la chama/mgombeaji au picha ya chama unachokichagua."

Mpiga kura anafaa "kuweka alama kwa mgombeaji mmoja tu." Hufai kuweka alama yoyote nyingine kwenye karatasi ya kura.

Alama unayoweka inaweza kuwa alama ya ndio (✓), mkasi (✕), au hata alama ya kidole. Hata hivyo, huruhusiwi kuandika jina lako au kuweka sahihi yako kama alama ya kumchagua mgombea unayemtaka. Iwapo utafanya makosa bila kukusudia wakati wa kuweka alama yako kwenye karatasi ya kura na utambue hilo kabla ya kutumbukiza karatasi yako kwenye sanduku, unaweza kupewa karatasi nyingine ya kura. Unaweza kupewa karatasi mpya ya kura mara mbili pekee.

Baada ya kumaliza kuweka alama, unafaa kuikunja karatasi katikati -kutoka kushoto kwenda kulia ili kuweka siri uliyemchagua halafu utumbukize karatasi hiyo kwenye sanduku lifaalo.

Tume ya uchaguzi imepiga marufuku kurandaranda katika kituo baada ya kupiga kura. Vile vile, ni hatia kupiga picha katika kituo cha kupiga kura au kupiga picha karatasi za kura.

Uchaguzi
Maelezo ya picha, Uchaguzi Kenya

Uchaguzi Kenya 2022:Unaweza pia kusoma

Uchaguzi