Uchaguzi Kenya 2022: William Ruto - Kutoka kuwa muuzaji wa kuku hadi kuidhinishwa kuwa mgombea wa urais

Kenya's Deputy President William Ruto speaks to media after meeting with Kenya's Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) chairman at the Bomas of Kenya cultural center in Nairobi, on October 3, 2017

Chanzo cha picha, Getty Images

    • Author, Na Evelyne Musambi
    • Nafasi, BBC News, Nairobi
  • Iliyochapishwa

Maisha ya utotoni ya William Ruto ni mfano halisi wa maisha ya watoto wengi masikini Wakenya.

Alikwenda shule miguu peku, ambapo alivaa kwa mara ya kwanza viatu akiwa na umri wa miaka 15. Aliuza kuku na karanga kando ya barabara katika maeneo ya kijijini kwao katika mkoa wa Bonde la ufa (Rift Valley).

kwa hiyo sio jambo la kushangaza kwamba anajielezea kama kiongozi wa masikini wakati anapogombea kiti cha urais katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika tarehe 9 Agosti.

Bw Ruto anawania kiti hicho chini ya Muungano unaofahamika kama Kenya Kwanza, akitoa ahadi ya kukuza uchumi.

Kiwango rasmi cha ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana wenye kati ya umri wa miaka 18 na 34 ni karibu 40%, na uchumi hautoi ajira za kutosha kuweza kuwaajiri vijana 800,000 wanaoingia katika soko la ajira kila mwaka.

Kwahiyo amebuni usemi "Hustler nation" , akimaanisha vijana wanaohangaika kutafuta riziki .

Bw Ruto ameahidi mfumo wa kiuchumi unaowainua watu wenye pato la chini , akisema utawanufaisha masikini ambao wanakabiliwa na gharama ya mzozo wa maisha ambao umeikumba dunia kufuatia janga na Corona na vita ya Ukraine.

Hili ni jaribio la kwanza la mwanaume huyu mwenye umri wa miaka 55 la kugombea urais. Ana tumaini la kushinda kwenye uchaguzi wa Agosti 9 sawa na alivyoshinda ubunge wa jimbo la Eldoret Kaskazini mwaka 1997.

William Ruto (C) and Marsabit County Governor Mohammed Muhamud Ali (R) walk with performers of the Turkana tribe during the 11th Marsabit Lake Turkana Culture Festival in Loiyangalani near Lake Turkana, northern Kenya, on June 28, 2018

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Bw Ruto huvutia umati mkubwa katika kampeni zake

Alijiunga na siasa katika mwaka 1992, ambapo alifunzwa , kama alivyosema na aliyekuwa rais wa Kenya wakati huo Daniel Arap Moi.

Bw Ruto alikuwa sehemu ya tawi la vijana la chama kilichotawala wakati mmoja cha Bw Moi , na alikuwa mmoja wa wanaharakati waliopewa jukumu la kuhamasisha wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi katika mwaka huo huo.

Kwa sasa ana sifa ya kuwa mzungumzaji mwenye mamlaka mwenye uwezo wa kukusanya umati mkubwa katika mikutano ya kisiasa, na mwenye kufanya vyema katika mahojiano na vyombo vya habari.

Mara nyingi huanza kuzungumza kwa kusema "Rafiki yangu", matamshi yanayomsaidia kuanzisha uhusiano na wapiga kura.

Kuhama miungano

Baada ya kushikilia nyadhifa mbali mbali za uwaziri- ikiwa ni pamoja na waziri wa elimu-alipanda cheo na kuwa Naibu wa rais baada ya uchaguzi wa mwaka 2013.

Bw Ruto aligombea uchaguzi huo kama mgombea mwenza wa rais anayeondoka madarakani Uhuru Kenyatta, ambapo aliwashangaza Wakenya wengi kwasababu walikuwa katika pande zinazopingana kisiasa katika uchaguzi uotangulia.

Ulikuwa ni muungano wa manufaa, kwani wote wawili walikuwa wameshitakiwa na mahakama ya Kimataifa ya uhalifu kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu baada ya kushutumiwa kuchochea ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007 ulioibua mgawanyiko mkubwa, ambapo watu 1,200 waliuawa. Katika uchaguzi huo, Bwana Ruto alikuwa ameunga mkono mgombea wa upinzani raila Odinga-ambaye sasa ni hasimu wake kisiasa-huku Bw Kenyatta akimuunga mkono aliyekuwa rais wakati huo -Mwai Kibaki katika azma ya kuwania tena urais.

Nani yuko kwenye kinyang'anyiro cha kuiongoza Kenya ?

Fahamu zaidi kuwahusu wagombea urais wa Kenya

Chagua mgombea ili kutazama wasifu wake

Raila Amollo Odinga

Muungano wa Azimio la Umoja

  • Mgombea huyo mwenye umri wa miaka 77 ni mhandisi aliyesomea Chuo Kikuu cha Ufundi cha Magdeburg (sasa kinajulikana kama Chuo Kikuu cha Otto-von-Guericke Magdeburg) nchini Ujerumani.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.
  • Hili litakuwa jaribio lake la tano baada ya kugombea katika: 1997, 2007, 2013 na 2017.
  • Bw Odinga alikuwa mmoja wa wapiganiaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya. Alikamatwa, akafungwa na wakati fulani akaenda uhamishoni kwa sababu ya kupigania haki hiyo
  • Aliwahi kuwa Waziri Mkuu, kuanzia 2008-2013.
  • Odinga alihusika kufanikisha miradi mikubwa iliyotekelezwa na serikali ya Kibaki, kama vile miradi ya umeme vijijini na barabara.
  • Kuafikia ukuaji wa uchumi wa tarakimu mbili kupitia uwekezaji katika biashara ndogo ndogo na sekta ya viwanda.
  • Utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.
  • Utoaji wa vifaa vya michezo na burudani kwa ukuaji wa kimwili, kiakili, kijamii, kimaadili na maendeleo ya watu.
  • Kufuatia jaribio la mapinduzi ya Agosti 1, 1982, Raila Odinga alikamatwa na kukabiliwa na mashtaka kadhaa, yakiwemo ya uhaini ambayo alizuiliwa bila kufunguliwa mashtaka. Tume ya Ukweli ya Haki na Maridhiano iliambiwa mwaka 2011 kwamba Odinga alikuwa na mawasiliano na mpangaji mkuu wa mapinduzi hayo. Odinga amekana kuhusika kila mara. - Makavazi ya Kitaifa ya Kenya.

William Samoei Ruto

Muungano wa Kenya Kwanza

  • Mgombea huyu mwenye umri wa miaka 55 ana Shahada ya Uzamifu/PhD katika Ikolojia ya Mimea na BSc katika Botany na Zoology kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi.
  • Anawania kiti cha urais kwa tikiti ya chama cha United Democratic Alliance ( chenye mafungamano na Kenya Kwanza).
  • Aliongoza Vuguvugu la vijana la Youth for Kanu '92 (YK'(92).
  • Wizara yake iliorodheshwa kama inayofanya bora zaidi serikalini alipokuwa Waziri wa Kilimo.
  • Alihudumu kama Naibu Rais wa kwanza wa Kenya chini ya katiba mpya ya 2010.
  • Alihudumu kama mbunge wa eneo bunge la Eldoret Kaskazini kuanzia 1997-2007.
  • Kutenga $424 milioni kila mwaka kwa biashara ndogo ndogo za kati.
  • Kuanzisha mfuko wa elimu wa kitaifa ili kukidhi gharama zisizo za masomo.
  • Tekeleza kikamilifu sheria ya usawa wa kijinsia ya thuluthi mbili katika uteuzi wa kisiasa na kutenga nusu ya baraza lake la mawaziri kwa wanawake.
  • Mnamo 2008, Mahakama Kuu ya Kenya iliamuru Naibu Rais William Ruto kusalimisha shamba la ekari 100 na kulipa $ 62,500 kwa Adrian Muteshi, mkulima ambaye alimshtaki kwa kuchukua mali hiyo baada ya uchaguzi wa 2007. - Kenya Law
  • Mnamo 2011, Bw Ruto alikabiliwa na kesi kwa makosa matatu dhidi ya binadamu: Mauaji, uhamisho wa watu kwa lazima na mateso ya watu katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu. Miaka mitano baadaye mahakama ilisitisha kesi hiyo kwa msingi kwamba - ushahidi wa upande wa mashtaka ulikuwa dhaifu. -ICC

George Wajackoyah

Chama cha Roots

  • Profesa huyo mwenye umri wa miaka 61 ana shahada ya uzamili katika sheria kuhusu maendeleo kutoka Chuo Kikuu cha Warwick na shahada ya uzamili , sheria (sheria za Marekani kutoka Chuo Kikuu cha Baltimore.
  • Bw Wajackoyah anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Roots Party.
  • Alihudumu kama Inspekta katika idara ya usalama ya Special branch wakati wa utawala wa marehemu Rais Daniel Moi kabla ya kulazimika kutorokea ng'ambo ili kuepuka kufunguliwa mashtaka na mamlaka.
  • Yeye ni mshirika katika kampuni ya mawakili aliyoianzisha mwaka wa 2018.
  • Alifunnza somo la sheria na uchumi katika vyuo vikuu vya Marekani, Uingereza na Kenya.
  • Kuhalalisha matumizi ya kiviwanda ya bangi
  • Badilisha siku za kazi hadi Jumatatu hadi Alhamisi.
  • Huduma ya afya ya bure na msaada kwa wazee, walio hatarini na wajawazito

David Mwaure Waihiga

Chama cha Agano

  • David Mwaure anawania kiti cha urais kwa tiketi ya Chama cha Agano.
  • Ni kiongozi wa Chama cha Agano.
  • Alihitimu na shahada ya sheria kutoka Chuo Kikuu cha Nairobi na ana Shahada ya Uzamili katika masomo ya uongozi.
  • Yeye ni wakili mkuu na amehudumu kama mwanasheria kwa zaidi ya miongo mitatu.
  • Ana kampuni ya uwakili na amewania viti mbalimbali vya kisiasa.
  • Ilianzishwa chama cha Agano mwaka 2006.
  • Kupambana na ufisadi uliokithiri.
  • kuunda nafasi za ajira.
  • Kurejesha mali ya Kenya iliyofichwa nje ya nchi.

Pata maelezo zaidi kuhusu sera za wagombea urais hapa

Muungano wao, ulioipachikwa jina la ''bromance'', ulizaa matunda kwani wanaume hao wawili walichukua mamlaka, yaliyowaweka katika nafasi imara ya kuondokana na tisho lililowakabili wote kutoka mahakama ya ICC- mafanikio ambayo waliyapata wakati mwendesha mashitaka alipomuondolea mashitaka Rais Kenyatta katika mwaka 2014 na Jaji akatupa nje kesi dhidi ya Bw Ruto mwaka 2016.

Kenya's president Uhuru Kenyatta (R) waves to the welcoming crowd flanked by deputy-president William Ruto on October 9, 2014 in Nairobi, a day after becoming the first sitting president to appear before the International Criminal Court on crimes against humanity charges

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Bw Kenyatta (Kulia) na Bw Ruto walikuwa timu moja hadi walipokosana

Hatahivyo Muungano wao ulivunjika katika mwaka 2018,wakati Bw kenyataa- katika mabadiliko mengine makubwa ya kisiasa alipoamua - kufanya maridhinao na Bw Odinga, na kuondoa matumaini ya Bw Ruto kwamba rais anayeondoka mamlakani angemuidhinisha kama mrithi wake katika kampeni za uchaguzi zinazoendelea kwa sasa.

Washirika wa rais wanamlaumu Bw Ruto kwa kukosa utiifu, madai ambayo anayakanusha, lakini amekiri kutofautiana, kwa kusema kuwa yeye na rais ''wanamtizamo tofauti wa siasa.''

Bw Ruto, amesalia kuwa mamlakani, kutokana na vipengele vya katiba vnavyomuwezesha Naibu rais kubakia mamlakani hadi muhula wake unapomalizika.

Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Chagua suala ambalo linakuvutia

Sera za kila chama

  • Azimio La Umoja One Kenya Coalition

  • Roots Party of Kenya

  • Chama cha Agano

  • Kenya Kwanza Alliance

Mwongozo huu ni muhtasari wa sera kuu zinazotolewa na kila chama.

Pata maelezo zaidi kuhusu wagombea urais wa Kenya hapa

End of Uchaguzi wa Kenya 2022: Vyama vinakuahidi nini?

Mmiliki wa ardhi kubwa na mkulima makini

Ufuasi ya kikabila una fursa kubwa katika siasa za kenya na bw Ruto anatoka katika kabila la tatu kwa ukubwa , la Kalenjin, ambapo limekwisha kuwa na rais mmoja tu, hayati daniel Arap Moi, ambaye alikuwa rais wa muda mrefu zaidi aliyeitawala Kenya.

Amemuoa Rachael, ambaye kwa mara ya kwanza walikutana katika mikutano vijana ya kanisa.

Wana watoto sita. Kijana wao mkubwa Nick, wakati mmoja alibarikiwa na wazee wa Kikalenjin, jambo lililochochea uvumi kwamba alikuwa anatayarishwa kwa ajili ya kuchukua wadhifa wa kisiasa, huku binti yao, June, akifany akazi katika wizara ya mambo ya nje.

William Ruto

Chanzo cha picha, Kenya Deputy President Office

Maelezo ya picha, Bw Ruto amekuwa akitoia mikokoteni kwa vijana huku akipigia debe biashara ndogo ndogo.

Bw Ruto anapenda ukulima , jambo ambalo limemfanya awe mkulima wa mahindi, ufugaji wa ng'ombe na kuku.

Anamiliki ardhi kubwa katika maeneio ya magharibi na kpwani ya Kenyana pia amewekeza katika sekta ya utalii.

bw Ruto amekuwa akihusishwa na kashfa za ufisadi katika serikali na vyanzo vya utajiri wake vimekuwa vikiibua tetesi nyingi.

Mwezi Juni mwaka 2013, Mahakama ya juu zaidi ilimuamuru asalimishe shamba la heka 100, na kulipa fidia kwa mkulima ambaye alimshutumu kunyakua ardhi wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.

Alikanusha kufanya kosa lolote, na anaendelea kuwaomba kura vijana, akiwaahidi kuwapatia fursa ya kuboresha maisha yao, kama alivyofanya yeye.

Election branding