Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kwa nini wanawake walionyoa vichwa wanatuchanganya?
Mnamo Februari 2007, mwimbaji Mmarekani Britney Spears aliingia kwenye saluni huko Los Angeles na kumwomba Esther Tugnozzi kuzinyoa nywele zake kabisa.
Wakati Esther alipokataa, kwa kuhofia kufunguliwa mashitaka ya "kuhujumu sura ya msanii huyo", Spears alinyakua wembe na kuupitisha kichwani ili kunyoa nywele zake kabisa, katika harakati ambazo wapiga picha walifanikiwa kunasa na kuwa moja ya picha maarufu ulimwenguni.
Picha ya Spears inayomuonyesha akiwa na wembe huo kwenye kichwa chake kilicho kitupu, isipokuwa nywele chache ambazo bado hajagusa. Anahusishwa na mfadhaiko wa kisaikolojia uliomkumba kati ya matatizo ya kibinafsi aliyokumbana nayo baada ya kutengana na mumewe.
Ikiwa kukata nywele kwa mwanamke daima kunahusishwa na hisia zake, kwa sababu nywele ni sehemu rahisi ya mwili kubadilika, unyanyapaa wa wanawake ambao huchagua kukata huonyesha viwango vingine vya tabia na kitamaduni.
Na ingawa waigizaji wa kike wa kigeni wamenyoa nywele zao ili kutekeleza majukumu fulani, kama vile Demi Moore, Natalie Portman na Charlize Theron, utata unaonekana kuibuka tu unapotokana na chaguo la mwanamke. Mshtuko unaoonyeshwa na umma kwa mwanamke aliye na kichwa kilichonyolewa yaweza kuonyesha kile kilicho ndani zaidi katika mtazamo wa wanawake.
Kutoka kwa hadithi hadi dini
Kihistoria, nywele za wanawake zimekuwa na maana nyingi. Daima inahusishwa na jinsia yake, na kwa dhana ya uke kwa ujumla, pamoja na kuchukuliwa kuwa kiashiria muhimu ya tofauti hakika kati ya wanaume na wanawake.
Kwa mfano, nywele ndefu za Rapunzel zilikuwa na nguvu za miujiza katika hadithi maarufu ya Ujerumani. Hapo awali, nywele za Medusa zilikuwa maarufu, ambazo mungu wa kike Athena alibadilisha katika hadithi ya Uigiriki kuwa viboko vya nyoka kama adhabu.
Mbali na hadithi, nywele za wanawake zilichukua nafasi maalum katika dini tatu za Mungu mmoja.
Kwa mujibu wa sheria ya Kiyahudi (halakhah), baada ya kuolewa, mwanamke wa Kiyahudi lazima afunika kichwa chake akiwa mbele ya wanaume nje ya familia. Miongoni mwa Haredim, bado ni kawaida kwa mwanamke aliyeolewa kuvaa wigi, inayoitwa "shettle". Baadhi ya wanawake pia hunyoa vichwa vyao kabisa kabla ya kuvaa wigi, ili kuonyesha kujitolea zaidi kwa dini na mume.
Katika Ukristo, waraka wa kwanza wa Mtakatifu Paulo kwa Wakorintho ndio marejeo pekee katika eneo hili, ambapo aliwaita wanawake kufunika vichwa vyao (maana "mwanaume ndiye kichwa cha mwanamke", kama inavyoonyeshwa katika sura ya tano ya barua ya Paulo. kwa Waefeso) akionyesha chuki kwa mwanamke aliyenyolewa: "Na kama vile mwanamke awaye yote asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, anaaibisha kichwa chake, kwa maana ni kama amenyolewa."
Na anaongeza katika barua hiyo hiyo: "ikiwa mwanamke hajafunikwa, basi nywele zake zikatwe. Na ikiwa mwanamke hataki kukata au kunyoa, basi afunike ".
Katika Uislamu, mafaqihi hutegemea aya za Qur'an ambazo mara nyingi zimefasiriwa kuwa zinawataka wanawake kuvaa sitara na kufunika sehemu nyingine za mwili, kama vile shingo na kifua mbele ya wanaume ambao si Mahram. (Mwanaume anayekaribiana na mwanamke na ambaye hawezi kusherehekea naye ndoa, kwa mujibu wa sharia. Marufuku haya yamewekwa kwa sababu ya uhusiano wa umoja, muungano au kunyonyesha).
Kashfa na unyanyapaa
Katika msimu wa tano wa mfululizo maarufu wa "Game of Thrones", Malkia Cersei Lannister (Lena Headey) anaadhibiwa baada ya kukiri uzinzi kwa kufanya "Kutembea kwa Upatanishoambapo inabidi atembee katikati ya umati baada ya kuvuliwa na kukatwa nywele.
Tukio hilo linatokana na adhabu halisi ambayo ilifanyika Ulaya ya zama za kati, ambapo wahalifu wa uzinzi (hasa wanawake, kama wanaume kawaida waliweza kutoroka) waliadhibiwa kwa kutembea nusu uchi na kukatwa nywele zao katikati ya watu kwa lengo la kuwadhalilisha maisha yao yote.
Katika filamu ya "Malina", wanawake wa mjini humo wamvamia gwiji huyo kwa jina (Monica Bellucci) baada ya ukahaba wake kwa kumpiga na kumkata nywele katika viwanja vya mji kwa nia ya kumdhalilisha.
Mifano hii miwili ni sehemu ya anuwai ya kazi za filamu na fasihi (kwa mfano, The Scarlet Letter) ambapo kukata nywele za mwanamke kuliwakilisha adhabu na unyanyapaa wa kimaadili hadharani.
Mwisho wa "kutokuwa na hatia"
Kutokana na hili, labda tunaweza kuelewa hasira iliyofuatana na mtindo wa kukata nywele kwa wanawake huko Marekani mwanzoni mwa karne ya 20.
Katika dhihirisho moja la hasira hii, Brownmiller anasema katika kitabu chake kwamba magazeti ya Marekani yalichapisha picha za mwigizaji Mary Pickford, ambaye alikuwa maarufu kwa nywele zake ndefu, akikata nywele, na kichwa cha habari "Mwisho wa Enzi ya Hatia".
Mmoja wa waigizaji ambaye alianza mtindo wa nywele fupi wakati huo, Erin Castle, aliandika katika gazeti la Murra, kwamba alilaumiwa sana "kwa nyumba zilizoharibiwa na mahusiano yalivyovunjwa kwa kukata nywele zake".
Vile vile, gazeti la Times lilijibu mwaka wa 1916 kwa mwito wa mwandishi wa riwaya wa Marekani Charlotte Gilman kwa wanawake kukata nywele zao, akisema kwamba utekelezaji wa wito huu uliitisha "mwisho wa mapenzi".
Kujinyima
Kuna maoni ambayo yanasema kwamba kubadili mtindo wa nywele kwa mwanamke hutangaza mapinduzi yake dhidi ya muonekano wake kama kitu cha tamaa ya kudumu ya mwanaume.
Anaachana na mikunjo yake mirefu ambayo huonekana kama sababu kuu ya kutongozwa, na kuchukua fomu ambayo kawaida hudhibitiwa na wanaume wasio na nywele, ambayo wakati mwingine huchukuliwa kuwa ishara ya mwanamume.
Anavuka mstari mwekundu unaowakilisha nywele kama alama utofauti kati ya mwanamume na mwanamke.
Kwa hiyo, chaguo la mwanamke kufanya jambo ambalo hapo awali lilikuwa la fedheha, ambapo dini na zilichukulia nywele za wanawake na kukataa kwake kimakusudi kuunda sura yake kwa mwanamume, yote ni sababu tosha ya kuelewa mshtuko na mkanganyiko unaorudiwa katika jamii zetu.