Moto uliozuka katika hospitali ya corona Iraq: Watu 82 wafariki baada ya 'tangi la Oksijeni kulipuka'

Maelezo ya video, Ndani ya hospitali ya Ibn Khatib ambapo moto mkali ulitokea
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Takriban watu 82 wamefariki katika moto uliozuka katika hospitali ya kutibu wagonjwa wa Covid 19 katika mji mkuu wa Iraq Baghdad.

Zaidi ya watu 100 walijeruhiwa katika moto huo uliozuka katika hospitali ya Ibn Khatib siku ya Jumamosi usiku.

Ripoti zinasema kwamba ajali ilisababisha tangi la oksijeni kulipuka na kusababisha moto huo.

Kanda za video zinaonesha wazima moto wakijaribu kuuzima moto huo huku watu wakitoroka jumba hilo.

Waziri mkuu wa Iraq Mustafa al-Kadhimi alitoa wito wa kufanyika kwa uchunguzi wa haraka kuhusu chanzo cha kile alichokitaja kuwa ajali mbaya.

Maafisa wa kukabiliana na hali ya dharura walilazimika kuwatibu wagonjwa na ndugu zao

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Maafisa wa kukabiliana na hali ya dharura walilazimika kuwatibu wagonjwa na ndugu zao

Mkuu wa ulinzi wa umma Jenerali Kadhim Bohan, alisema kwamba moto huo ulianzia katika chumba cha wagonjwa mahututi katika ghorofa iliotengwa kuwasaidia watu kupumua.

Takriban wagonjwa 30 walikuwa katika chumba hicho cha wagonjwa mahututi kilichotengewa watu waliokuwa hatarini na corona mjini Baghdad, chanzo kimoja cha hospitali kiliambia chombo cha habari cha AFP.

Wagonjwa wote wamehamishwa katika hospitali iliopo karibu.

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

1px transparent line

Moto huo ulidhibitiwa mapema siku ya Jumapili , alisema mkuu wa ulinzi wa umma nchini humo.

Gavana wa mji wa Baghdad Mojammed Jaber aliunga mkono wito wa waziri mkuu kuhusu kufanyika kwa uchunguzi wa haraka ili kubaini iwapo kuna mtu yeyote anayepaswa kuchukuliwa hatua.

Katika taarifa , tume ya haki za kibinadamu inayomilikiwa na serikali imesema kuwa tukio hilo ni uhalifu dhidi ya wagonjwa waliochoshwa na ugonjwa wa corona.

Ripoti zinasema kwamba tangi la oksijeni lililolipuka ndio chanzo cha moto huo

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Ripoti zinasema kwamba tangi la oksijeni lililolipuka ndio chanzo cha moto huo

Hospitali za Iraq zimezidiwa na idadi ya wagonjwa wa Covid 19 wakati wa mlipuko wa ugonjwa huo, ukiongezewa na vita vya wenyewe kwa wenyewe, kupuuzwa na ufisadi.

Maambukizi ya Covid yamekua yakiongezeka kwa kasi tangu mwezi februari nchini Iraq na idadi hiyo imepitisha kiwango cha wagonjwa milioni moja wiki hii.

Wizara ya Afya imerekodi wagonjwa 1,025,288 na vifo 15,217 .

Taifa hilo limezindua kampeni yake ya chanjo mwezi uliopita na imepokea dozi 650,000, nyingi zikitoka kwa mpango wa WHO wa Covax, ambao ni wa kusambaza chanjo duniani.