Uchaguzi wa Uganda 2020: Bobi Wine kurejelea kampeni zake Jumatatu licha ya mikutano kupingwa

Chanzo cha picha, AFP
Mgombea urais nchini Uganda wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) Robert Kyagulanyi Ssentamu ambaye pia anajulikana kama Bobi Wine atarejelea shughuli zake za kampeni Jumatatu.
Kampeni za Bobi Wine zilikatizwa Jumatano baada ya kukamatwa katika eneo la Luuka na kupelekwa kituo cha polisi cha Nalufenya.
Katika ujumbe aliouweka hii leo kwenye mtandao wa Twitter, Bobi Wine ameashiria kutokata tamaa ya kile anachotaka kufikia.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Kwa mujibu wa msemaji wa chama chake cha NUP Joel Ssenyonyi, Bobi Wine atarejelea kampeni zake Jumatatu 23, Novemba katika eneo la Kyenjojo na Fort portal.
Pia inasemekana kwamba kuna mipango ya kupanga tena kampeni katika maeneo alikotakiwa kufika kabla ya kukamatwa.
Baada ya kuchiwa huru, Bobi Wine alisema wafuasi wake wamejitolea kuendelea kupigania mabadiliko nchini humo na kuongeza kuwa hatua ya kuongezwa kwa maafisa wa usalama ni ishara ya uoga, hofu na ukosefu wa matumiani.

Chanzo cha picha, Getty Images
Bobi Wine alifanya maombi maalum na kutuma rambi rambi zake kwa familia zilizopoteza wapendwa wao wakati wa vurugu zilizotokea wiki jana baada ya kukamatwa kwake.
Jumamosi asubuhi, magari ya vikosi vya usalama yaliegeshwa katika maeneo tofauti mjini Kampala huku polisi wakishika doria katika maeneo karibu na makao makuu ya chama cha upinzani cha People's Power.
Polisi imetangaza kuwa ni watu 28 waliofarika katika maandamano ya siku ya Jumatano na Alhamisi, japo vyombo vya habari nchini Uganda vinanukuu vyanzo vya hospitali kuu kwamba idadi ya waliofariki ni watu 37.
Bobi Wine aliachiwa kwa dhamana siku ya Ijumaa, baada ya kushtakiwa kwa kukiuka kanuni za kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona.
Anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka saba gerezani akipatikana na makosa.

Chanzo cha picha, AFP
Kwa upande wake Rais Yoweri Museveni, ameweka wazi kwamba hakuna haja ya kuahirisha uchaguzi mkuu nchini Uganda.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Bwana Museveni ameongeza kuwa kutofanya mikutano ya kampeni sio mwisho wa dunia na hilo halitakubalika kipindi hiki cha janga la virusi vya corona.












