Uchaguzi wa Uganda 2020: Bobi Wine kurejelea kampeni zake Jumatatu licha ya mikutano kupingwa

Bobi wine

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Wine anasema Museveni hazingatii maadili yaliomuongoza kwa wakati mmoja
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Mgombea urais nchini Uganda wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) Robert Kyagulanyi Ssentamu ambaye pia anajulikana kama Bobi Wine atarejelea shughuli zake za kampeni Jumatatu.

Kampeni za Bobi Wine zilikatizwa Jumatano baada ya kukamatwa katika eneo la Luuka na kupelekwa kituo cha polisi cha Nalufenya.

Katika ujumbe aliouweka hii leo kwenye mtandao wa Twitter, Bobi Wine ameashiria kutokata tamaa ya kile anachotaka kufikia.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Kwa mujibu wa msemaji wa chama chake cha NUP Joel Ssenyonyi, Bobi Wine atarejelea kampeni zake Jumatatu 23, Novemba katika eneo la Kyenjojo na Fort portal.

Pia inasemekana kwamba kuna mipango ya kupanga tena kampeni katika maeneo alikotakiwa kufika kabla ya kukamatwa.

Baada ya kuchiwa huru, Bobi Wine alisema wafuasi wake wamejitolea kuendelea kupigania mabadiliko nchini humo na kuongeza kuwa hatua ya kuongezwa kwa maafisa wa usalama ni ishara ya uoga, hofu na ukosefu wa matumiani.

Wafuasi wa mwanamuziki aliyegeuka mwanasiasa Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine, walibeba mabango na kuandamana katika maeneo tofauti ya Uganda kupinga hatua ya kukamatwa kwake mapema wiki hii

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Waandamanaji walikusanya na kuchoma tairi za magari katika mji mkuu wa Kampala, mapema wiki jana

Bobi Wine alifanya maombi maalum na kutuma rambi rambi zake kwa familia zilizopoteza wapendwa wao wakati wa vurugu zilizotokea wiki jana baada ya kukamatwa kwake.

Jumamosi asubuhi, magari ya vikosi vya usalama yaliegeshwa katika maeneo tofauti mjini Kampala huku polisi wakishika doria katika maeneo karibu na makao makuu ya chama cha upinzani cha People's Power.

Polisi imetangaza kuwa ni watu 28 waliofarika katika maandamano ya siku ya Jumatano na Alhamisi, japo vyombo vya habari nchini Uganda vinanukuu vyanzo vya hospitali kuu kwamba idadi ya waliofariki ni watu 37.

Bobi Wine aliachiwa kwa dhamana siku ya Ijumaa, baada ya kushtakiwa kwa kukiuka kanuni za kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona.

Anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka saba gerezani akipatikana na makosa.

Yoweri Museveni

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Rais wa Uganda Yoweri Museveni

Kwa upande wake Rais Yoweri Museveni, ameweka wazi kwamba hakuna haja ya kuahirisha uchaguzi mkuu nchini Uganda.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Bwana Museveni ameongeza kuwa kutofanya mikutano ya kampeni sio mwisho wa dunia na hilo halitakubalika kipindi hiki cha janga la virusi vya corona.