Moja kwa moja, Mjumbe wa Trump, Waziri wa Iran waelekea Uswizi kwa mazungumzo

Israel na Hezbollah walikubaliana kusitisha mapigano nchini Lebanon siku ya Ijumaa ambayo ni muhimu kwa ajili ya kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz.

Muhtasari

Skip Video and continue reading
  • xx
  • xx
  • d
  • s
  • a
  • Sonko
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • xx
  • Dangote
  • xx
  • Lydia Wanjiku

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Vifo takriban 30 katika kambi DRC vinaonyesha Ebola inaweza kuwa inaenea kwa kasi

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Watu wasiopungua 30 wamefariki tangu mwanzoni mwa mwezi Mei katika kambi moja ya watu waliokimbia makazi yao kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.

    Maafisa wa kambi walisema kiwango hicho cha vifo hakijawahi kushuhudiwa katika siku za nyuma, kutokana na dalili zilizoripotiwa, kunaweza kuashiria ugonjwa wa Ebola unaosambaa kwa kasi katika eneo hilo.

    Haikuwezekana kuthibitisha chanzo cha vifo hivyo kwa sababu wagonjwa na ndugu zao katika kambi ya Kigonze huko Bunia — kitovu cha mlipuko wa Ebola nchini DRC — walikuwa wamekataa kufanyiwa vipimo ama kwa walio hai au waliokufa, hadi siku ya Alhamisi.

    Hayo yalithibitishwa na msemaji wa kambi pamoja na shirika la misaada la Caritas.

    Hata hivyo, watu wote waliokuwa wamefariki walionyesha dalili kama maumivu ya kichwa, homa na kutapika, ambazo ni dalili zinazohusishwa na Ebola.

    Msemaji wa kambi, baba mmoja aliyempoteza mtoto, vyanzo vitatu vya misaada na kiongozi mmoja wa asasi za kiraia waliliambia shirika la habari la Reuters kuhusu hali hiyo.

    “Hapo kabla watu hawakuwa wakifa kwa namna hii,” alisema msemaji wa kambi, Desire Grodya Bapi, katika mahojiano na Reuters.

    Vifo hivyo katika kambi ya Kigonze, ambayo ina wakazi zaidi ya 15,000, vimezua hofu kwamba Ebola huenda inasambaa bila kugunduliwa miongoni mwa zaidi ya watu milioni 5 waliokimbia makazi yao mashariki mwa Congo.

    Upinzani dhidi ya vipimo pamoja na hali duni ya usafi wa mazingira vinaongeza ugumu wa kudhibiti ugonjwa huo.

    Soma zaidi:

  2. Treni mbili zagongana Uingereza na kusababisha majeraha mabaya

    .

    Chanzo cha picha, Dr Peter Knapp

    Dereva wa treni amefariki dunia na watu 89 kujeruhiwa baada ya treni mbili kugongana katika eneo la Bedford.

    Watu 11 walipata majeraha mabaya sana, 22 walijeruhiwa vibaya, na wengine 56 walipata majeraha madogo, kwa mujibu wa Huduma ya Ambulansi ya Mashariki mwa Uingereza.

    Ajali hiyo ilihusisha treni mbili za kampuni ya East Midlands Railway (EMR) zilizokuwa zikielekea kusini kwenda London St Pancras siku ya Ijumaa alasiri. Chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa.

    Katibu Mkuu wa chama cha wafanyakazi wa reli cha RMT, Eddie Dempsey, alisema chama hicho “kimehuzunishwa sana kusikia kwamba dereva wa treni na aliyekuwa mwakilishi wa RMT amefariki katika ajali hiyo.”

    Katika taarifa yake, Polisi wa Usafiri wa Uingereza (BTP) walisema wametangaza tukio hilo kuwa dharura kubwa baada ya mgongano huo uliotokea saa 11:15 jioni kwa saa za Uingereza.

    “Tunaelewa kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa na kwa masikitiko makubwa mtu mmoja amefariki dunia,” taarifa hiyo ilisema.

    Huduma za treni za East Midlands Railway kwenda na kutoka London St Pancras zilisimamishwa kwa muda wote wa Ijumaa jioni, na usumbufu wa safari unatarajiwa kuendelea hadi Jumamosi.

    Mmoja wa abiria, Dkt. Peter Knapp, aliiambia BBC kwamba alikuwa akisafiri katika behewa la mbele la treni iliyogongana na nyingine.

    “Niliposimama, niliona viti vimetapakaa kila mahali. Ilikuwa ni kana kwamba nilikuwa kwenye mlipuko wa bomu.

    “Niliposimama, niliona nyuso za watu zikiwa zimejaa damu, baadhi ya miguu yao ilionekana kuvunjika, na moshi ulikuwa kila mahali,” alisema.

    Akizungumza akiwa kando ya barabara, Dkt. Knapp alisema polisi walikuwa wakichukua taarifa za abiria huku baadhi yao wakipelekwa hospitalini.

  3. Marekani kusitisha ufadhili wa programu za HIV nchini Afrika Kusini

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Marekani imesema itasitisha ufadhili wa programu nchini Afrika Kusini zilizolenga kupambana na kuenea kwa Virusi vya UKIMWI na Ugonjwa wa UKIMWI.

    Zaidi ya watu milioni nane nchini Afrika Kusini wanaishi na HIV, ikiwa ni idadi kubwa zaidi kuliko nchi yoyote nyingine duniani.

    Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imeonekana kuhusisha uamuzi huo na madai kwamba Afrika Kusini imeshindwa kulinda jamii ya Waafrika wenye asili ya Kizungu, madai ambayo serikali ya Afrika Kusini imekuwa ikiyakana mara kwa mara.

    Wizara ya Afya ya Afrika Kusini ilijibu kwa kusema kwamba, ingawa haikuwa imefahamishwa rasmi kuhusu uamuzi huo, imekuwa ikifanya kazi kwa muda mrefu kwenye mpango wa kujitegemea kifedha.

    Hadi mwaka 2025, Marekani ilikuwa ikiunga mkono juhudi za Afrika Kusini za kupambana na virusi vya HIV kwa takribani dola milioni 400 za Marekani (£300 milioni) kwa mwaka kupitia Mfuko wa Dharura wa Rais wa Kukabiliana na Ukimwi (PEPFAR).

    Hata hivyo, tangu kuapishwa kwa Donald Trump, uhusiano kati ya nchi hizo mbili umeendelea kuzorota.

    Muda mfupi baada ya kuingia madarakani, Trump alitoa amri ya kiutendaji akidai kwamba sera nyingi za Afrika Kusini zimeondoa usawa wa fursa na kuchochea vurugu dhidi ya wamiliki wa ardhi wanaodaiwa kubaguliwa kwa misingi ya rangi.

    Serikali ya Afrika Kusini inapinga madai hayo na pia imezungumzia uhitaji wa sera yake iliyoanzishwa kurekebisha ukosefu wa usawa wa kiuchumi wa enzi ya ubaguzi wa rangi.

    Soma zaidi:

  4. Mjumbe wa Trump, Waziri wa Iran waelekea Uswizi kwa mazungumzo

    .

    Chanzo cha picha, Getty/Reuters

    Mjumbe wa Marekani Steve Witkoff na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi wameelekea Uswisi kwa mazungumzo, shirika la Axios liliripoti siku ya Ijumaa, huku usitishaji wa mapigano nchini Lebanon ukionekana kufufua juhudi za kubadilisha makubaliano ya muda ya kusitisha vita vya Iran kuwa mpango wa kudumu wa kikanda.

    Israel na Hezbollah walikubaliana kusitisha mapigano nchini Lebanon siku ya Ijumaa baada ya kuongezeka kwa mapigano yaliyotia shaka mazungumzo kati ya Marekani na Iran, ambayo ni muhimu kwa ajili ya kufunguliwa tena kwa Mlango-Bahari wa Hormuz na kuleta utulivu wa usambazaji wa mafuta.

    Hatua hiyo ilifuatia hati ya makubaliano yenye vipengele 14 ambayo pande hizo mbili zilitia saini wiki hii ili kusitisha mapigano na kufungua kipindi cha siku 60 cha kutatua mizozo kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, pamoja na masuala mengine magumu yanayohitajika ili kufikia makubaliano ya kudumu zaidi.

    Hata hivyo, makamu wa Rais wa Marekani JD Vance aliahirisha mipango siku ya Alhamisi ya kusafiri hadi Uswizi kwa mazungumzo hayo, huku kukiwa na mvutano unaoongezeka nchini Lebanon kati ya Israel na Hezbollah, kundi la wanamgambo linaloungwa mkono na Iran.

    Huku usitishaji mapigano ukiwa umeanza kutekelezwa, Witkoff anaelekea Uswizi kuungana na Jared Kushner, mkwe wa Rais Donald Trump, ambaye tayari yuko huko, Axios alisema. Araqchi anapanga kusafiri leo Jumamosi, iliongeza.

    Soma zaidi:

  5. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara kwa ajili ya kukujuza kinachotokea katika kila pembe ya dunia. Tarehe ni 20/06/2026, Mimi ni Asha Juma.