Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 17.07.2020: Pogba, Havertz, Tagliafico, Sarr, Thiago

Chanzo cha picha, AFP
Kiungo Mfaransa Paul Pogba, 27 , yuko karibu kukubali mkataba mpya wa miaka mitano kuichezea Manchester United. (Sun)
Bayer Leverkusen wamekubali kuwa kiungo wa kati Mjerumani Kai Havertz, 21, amechagua kujiunga na Chelsea lakini klabu hiyo inataka kuusogeza mbele uhamisho mpaka mwishoni mwa mwezi Agosti.(Daily Star)
Beki wa kushoto wa Ajax Nicolas Tagliafico, 27,ni mchezaji muhimu kwa Manchester City msimu huu. (Sports Illustrated)
Kiungo wa Uhispania Thiago Alcantara,29, anaamini kuwa ataelekea Liverpool baada ya kukataa mkataba mpya na Bayern Munich.( Daily Mirror)

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal iko mbioni kumsajili beki Mfaransa Malang Sarr, lakini mchezaji huyo, 21, anayepatikana kwa uhamisho wa bila malipo akitokea Nice tayari ameshafuatiliwa na vilabu vya Italia na Ujerumani.( Sun)
Manchester United imekubali kuingia mkataba na beki wa kushoto wa Real Madrid, Alvaro Fernandez Carreras, 17, ambaye atatia saini mkataba wa miaka minne kukipiga Old Trafford. (AS-in Spanish)
Kocha wa zamani wa Southampton na Tottenham Mauricio Pochettino yuko kwenye orodha ya Inter Milan na Juventus ikiwa vilabu hivyo vya Italia vitawafuta kazi makocha wa zamani wa Chelsea - Antonio Conte na Maurizio Sarri - mwishoni mwa msimu. (Daily Telegraph)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kocha wa Inter, Conte analazimika kuishawishi bodi ya klabu kukubali mshahara wa N'Golo Kante na kumsajili kiungo huyo,29, kutoka Chelsea.(SempreInter)
Kiungo wa kati Muingereza Jude Bellingham, 17, amekamilisha vipimo vya matibabu katika klabu ya Borussia Dortmund kabla ya kuondoka klabu ya Birmingham, lakini kwanza atakamilisha msimu huu na The Blues (Sky Sports)
Tottenham inaweza kumkosa mchezaji wa nafasi ya ulinzi Serge Aurier, 27, baada ya kurudi Ufaransa kutokana na kifo cha kaka yake. (Evening Standard)
Everton imetoa ofa kwa kiungo wa Napoli Allan, lakini klabu hiyo ya Italia imesitisha makubaliano na mchezaji huyo Mbrazili,29, (Sport Witness)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kocha Roy Hodgson amesema kuwasili kwa sura mpya Crystal Palace msimu huu kutaruhusu klabu hiyo kuwa na malengo makubwa msimu ujao na kuwania nafasi 10 za juu. (Evening Standard)
Manchester City imekubaliana na masharti ya winga wa Valencia Mhispania Ferran Torres,20. (Eurosport)
Manchester United haina mpango wa kumjumuisha mchezaji wa nafasi ya ulinzi Muajentina Marcos Rojo,30, katika kikosi chao cha kwanza baada ya kukatishwa tamaa na kiwango cha mchezo wake akiichezea klabu ya Estudiantes kwa mkopo (Manchester Evening News)
Raia wa Argentina na beki wa zamani wa Italia Ezequiel Schelotto, 31, ameweka wazi kuwa anaondoka Brighton na amelenga kurejea Serie A. (The Argus)

Chanzo cha picha, Reuters
West Ham,Norwich na Watford zinamuwania kiungo wa kati wa QPR Ryan Manning,24. (Football Insider)
Kocha wa Leicester Brendan Rodgers anamfuatilia kwa karibu mchezaji wa Roma Amadou Diawara. Kiungo huyo wa kati anayetimiza miaka 23, Ijumaa ya leo,pia amehusishwa na Tottenham na Newcastle. (Leicester Mercury)
Walsall inaendelea kufanya mazungumzo na kiungo wa England Danny Guthrie ,33, kuhusu mkataba mpya. (Express & Star)
TETESI ZA SOKA ALHAMISI

Chanzo cha picha, Getty Images
Manchester City wametakiwa kuweka mezani kitita cha pauni milioni 65 kwa ajili ya beki wa Napoli Kalidou Koulibaly ,29, ambaye anauhishwa na taarifa za kuhamia Liverpool na Manchester United na awali alikuwa na thamani ya pauni milioni 80. (Daily Mirror)
Manchester City inamtazama mshambuliaji wa Inter Milan Muajentina Lautaro Martinez,22, kama mchezaji muhimu katika kuchukua nafasi ya Sergio Aguero,32. (Sky Sports)
Hatahivyo, Martinez yuko ukingoni kumalizana na hatua za uhamisho kuelekea Barcelona. (Marca)
Bayern Munich inatafuta pauni milioni 40 kwa ajili ya kiungo wao wa kati wa zamani Thiago Alcantare, Mhispania ,29. (Sport Bild via Daily Mirror)

Chanzo cha picha, Reuters
Bayern wanafikiriwa kujitoa katika kinyang'anyiro cha kumnasa kiungo Kai Havertz,21 anayekipiga na Bayer Leverkusen. (Sport Bild, via Daily Mail)
Everton, Atletico Madrid na Bayern Munich wanatarajiwa kuweka nia ya kumnyakua winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha msimu huu, huku Newcastle pia ikimfuatilia kwa karibu mchezaji huyo,27. (Daily Mail)
Southampton wana matumaini ya kupata mkataba wa kudumu wa pauni milioni 10 kwa ajili ya mchezaji wa nafasi ya ulinzi wa Totteham, Muingereza Kyle Walker-Peters,23, ambaye anakipiga Saints kwa mkopo tangu mwezi Januari (Sun)
Kocha wa Southamton Ralph Husenhuttl amekataa kufanya mazungumzo kuhusu uwezekano wa kubadilishana kiungo wa kati Pierre-Emile Hojbjerg,24, na Walker-Peters. (Sky Sports)

Chanzo cha picha, Reuters
Kiungo wa kati wa Birmingham Jude Bellingham,17 amekubali kuhamia Borussia Dortumund kwa kitita cha pauni milioni 22.5. (Bild)
Kiungo wa Ghana Thomas Partey,27, anaripotiwa kujiandaa kusaini mkataba mpya na Atletico Madrid, ambayo imemuahidi kumpa mshahara mara mbili zaidi. (Ghana SoccerNet,via Daily Mail)
Pep Guardiola amefungua mlango kwa ajili ya kiungo wa kati wa Aston Villa Douglas Luiz,22, kurejea Manchester City baada ya kufuguliwa kwa dirisha la usajili mwezi Julai. (Birmingham Mail)
Kiungo wa kati wa Liverpool Adam Lallana,32, ambaye anawaacha miamba hiyo kwa uhamisho huru msimu huu, ananyemelewa na Leicester,Burnley na Brighton. (Daily Star)

Chanzo cha picha, Reuters
Beki wa Tottenham Danny Rose,30, ameendelea kuwa na matumaini ya kuufanya mkataba wake kuwa wa kudumu katika klabu ya Newcastle, huku kukiwa na taarifa za kuhusishwa kwake na Lazio (Newcastle Chronicle)
Middlesbrough wanaelekea kukubali kumpoteza beki wao wa kulia, Muingereza Djed Spence,19 msimu huu wakati vilabu kadhaa vya primia wakiwemo Tottenham, West Ham na Brighton wakijiandaa kuongeza kasi ya kumnasa mchezaji huyo. (ESPN)
Kiungo wa Everton Mo Besic,27, atakuwa tayari kuuzwa au kuondoka kwa mkopo msimu huu. (Liverpool Echo)

Chanzo cha picha, Empics
Portsmouth inatazamia uhamisho kwa mkopo wa beki wa kushoto wa Brighton Alex Cochrane,20. (Argus)
Kocha wa Wolves Nuno Espirito Santo hana uhakika iwapo mshambuliaji Raul Jimenez,29, atakosa mechi yoyote kwasababu ya kutarajia kuzaliwa kwa mtoto wake wa kwanza. (Express and Star)
TETESI ZA SOKA JUMATANO

Real Madrid inaamini kuwa mshambuliaji Kylian Mbappe ,21, atakuwa na mazungumzo nao kuhusu uhamisho kutoka Paris St-Germain. (Marca)
Chelsea iko tayari kumpatia kipa wa Atletico Madrid na Slovenia Jan Oblak ofa £90.7m. (AS - in Spanish)
Paris St-Germain inamlenga mshambuliaji wa Manchester United na Marcus Rashford, 22,. (Independent)
Barcelona inamuuza kiungo mchezeshaji wa Brazil Philippe Coutinho, 28, kwa Arsenal na Newcastle huku wakijaribu kutafuta fedha za kumnunua mshambuliaji wa Inter Milan na Argentina Lautaro Martinez, 22. (Goal)

Chanzo cha picha, BBC/Twitter
Mshambuliaji wa Brazil Neymar, 28, anataka kurudi Barcelona, na Paris St-Germain wanapiga hesabu za thamani yake huku akiwa amesalia na kandarasi ya miaka miwili katika mkataba wake (Mundo Deportivo - in Spanish)
Kiungo wa kati wa Southampton na Denmark Pierre-Emile Hojbjerg, 24, anataka kujiunga na Tottenham, ambayo inaweza kumtumia beki wa England Kyle Walker-Peters 23,kuafikia. (Evening Standard)
Mshambuliaji wa Lille na Nigeria Victor Osimhen, 21, amechagua kujiunga na Napoli katika mkataba wenye thamani ya Yuro milioni 81m (£73.5m). (RMC Sport - in French)

Manchester United itakosa malipo ya £25m kutoka kwa wafadhili iwapo watafeli kufuzu katika michuano ya kombe la klabu bingwa Ulaya. (Daily Mail)
Beki wa Liverpool na Uskochi Andrew Robertson, 26, anavutiwa ba uhamisho lakini atatia kandarasi ya muda mrefu na. (Lockdown Tactics via Express)

Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic, 38, amesema hana uhakika kuhusu mustakabali wake ndani ya AC Milan kwa kuwa hakuna mazungumzo yoyote yaliofanyika kuhusu mkataba ikiwa sasa ni chini ya mwezi mmoja kabla ya mkataba wake kufikia ukingoni. (Sky Sports)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kai Havertz anataka kuondoka Bayer Leverkusen kwasababu walishindwa kufuzu katika michuano ya klabu bingwa Ulaya hivyobasi Chelsea watalazimika kuhakikisha wanafuzu katika michuano hiyo ili kumshawishi kiungo huyo wa Ujerumain 21 kujiunga na timu hiyo.. (Bild)
Bayern Munich wanajiandaa kuanza mchakato wa kumnasa Tanguy Ndombele ,23, wa Tottenham na Mfaransa mwenzie anayecheza katika nafasi ya kiungo cha kati katika klabu ya Monaco, Tiemoue Bakayoko,25. (Le 10 Sport via Daily Mail)
Nice imetoa ofa kwa kiungo wa kati Mhispania Rony Lopes anayekipiga Sevilla. (RMC Sport-in French)
Mkurugenzi wa michezo katika klabu ya Norwich Stuart Webber amesema kwamba ombi la kutaka kumnunua mchezaji kinda mwenye kipaji mwisho wa msimu litaanza kwa dau la £20m . (Norwich Evening News)

Chanzo cha picha, Getty Images
Brentford inamlenga winga wa Portsmouth Ronan Curtis, 24 kwa ajili ya kuchukua nafasi ya Said Benrahma ikiwa ataondoka kwenye klabu hiyo. (The News, Portsmouth)

Chanzo cha picha, AFP
Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu amekataa uwezekano wa mshambuliaji wa Paris St-Germain Neymar,28, kurejea Nou Camp lakini amesema klabu inafikiria uhamisho wa mshambuliajji wa Inter Milan Muajentina Laitaro Martinez, 22. (TV3 Mundo Deportivo)
Bartomeu pia amesema ana ''uhakika'' mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi,33, atasalia Nou Camp zaidi ya mwaka ujao. (TV3 via Evening Standard)
Manchester City itatoa ofa kwa kocha Pep Guardiola ya mkataba wa muda muda mrefu baada ya marufuku dhidi ya klabu hiyo kufutwa. (Mirror)

Guardiola atapatiwa karibu kitita cha pauni milioni 150 kwa ajili ya kukipa nguvu kikosi cha City. (Guradian)
Inter Milan wanafikiria kumnunua kiungo wa kati, Mfaransa N'Golo Kante huku Blues wakiwa tayari kusikiliza ofa kwa ajili ya kumuuza mchezaji huyo wa Ufaransa, 29. (Gazzetta dello Sport, via Metro)
Zenit St Petersburg wameeleza nia yao ya kumsajili beki anayekipiga katika klabu ya Liverpool Dejan Lovren, 31. (Liverpool Echo)
AC Milan wanafiukiria kumnunua mashambuliaji wa Real Madrid raia wa Serbia Luca Jovic, 22, ambaye anayekodolewa macho na Leicester City na Arsenal. (Calciomercato,via Leicester Mercury)
Bayern Munich wana mpango wa kuwanasa viungo wawili wanaocheza ligi kuu ya Ufaransa, Tonguy Ndombele wa Tottenham, 23, na Tiemoue Bakayoko. (Le 10Sport)












