Ndege ya Iran yaanguka barabarani baada ya rubani kukosa mwelekeo

Ndege hiyo ilisimama katika barabara kuu karibu na uwanja wa ndege wa Mahshahr

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Ripota mmoja wa runinga ya taifa hilo amesema kwamba kulikuwa na tatizo katika matairi ya ndege hiyo
Iliyochapishwa
Muda wa kusoma: Dakika 2

Ndege ya abiria ya Iran ilijipata katika barabara ya umma baada ya kuteleza katika barabara ya uwanja wa ndege ilipokuwa ikitua.

Abiria wawili kati ya 136 waliokuwa wakiabiri ndege hiyo walipata majeraha ya miguu kufuatia kisa hicho katika mji wa Mahshahr, kulingana na maafisa wa afya.

Ndege hiyo ya kampuni ya Caspian iliondoka mjini Tehran . Matairi yake hayakujitokeza kabisa wakati ilipotarajiwa kutua.

Picha za abiria waliokuwa wakitoka katika ndege hiyo zilichapishwa katika mitandao ya kijamii.

Runinga ya serikali ilinukuu maafisa wa usafiri wa angani wakisema kwamba rubani aliishusha ndege hiyo kuchelewa hivyobasi akakosa barabara ya ndege.

Ripota mmoja ambaye alikuwa ndani ya ndege hiyo alisema kwamba matairi ya nyuma ya ndege hiyo yaliharibika na kwamba ndege hiyo iliteleza bila matairi yake.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Presentational white space

Msemaji wa shirika la udhibiti wa safari za angani Reza Jafarzadeh aliambia chombo cha habari cha Isna news kwamba ndege hiyo iliteleza kutoka katika barabara yake siku ya Jumatatu alfajiri .

Aliongezea kwamba uchunguzi unaendelea.

Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Presentational white space

Iran ina rekodi mbaya ya safari za ndege . Watu 66 walifariki katika ajali ya ndege mnamo mwezi Februari 2019, huku makumi wakifariki 2019 wakati ndege ya IranAir ilipovunjika vipandevipande baada ya kuanguka 2011.

Muungano wa Ulaya umepiga marufuku kampuni mbili za ndege kutotumia anga yake kutokana na wasiwasi wa kiusalama.

Iran ilikuwa imepanga kuimarisha ndege zake zilizozeeka baada ya vikwazo vya miaka mingi kuondolewa ikiwa ni miongono mwa makubaliano ya mkataba wa kinyuklia wa 2015 na mataifa yenye uwezo mkubwa.

Hatahivyo wizara ya fedha nchini Marekani ilifutilia mbali leseni ya kampuni kuuzia Iran ndege za abiria baada ya rais Donald Trump kujiondoa katika makubaliano hayo 2018.