Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu 9 wauwawa katika mashambulio ya mabomu nchini Indonesia
Idadi ya watu waliouwawa katika shambulio la kigaidi nchini Indonesia, imepanda kutoka watu wawili na kufikia watu 9.
Watu wengine 13 wamejeruhiwa, katika mashambulio ya kigaidi yaliyolenga makanisa kadhaa katika mji wa pili kwa ukubwa nchini humo wa Surabaya.
Miongoni mwa waliouwawa ni pamoja na mhanga wa kujitoa kufa.
Idara ya polisi kupitia kwa msemaji wake Frans Barung Mangera, imesema kuwa mashambulio matatu tofauti yalitokea kwenye makanisa- Kusini mwa Java.
Idara ya usalama imeongeza kusema kuwa, milipuko yote mitatu ilitokea dakika kumi baada ya nyingine.
Mashambulio hayo yanaminika kutekelezwa na Kundi la Islamic State linalojiita Jemaah Ansharut Daulah (JAD).