Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
NATO imekiri shambulio la Marekani Kabul liliwadhuru raia
Iliyochapishwa
NATO imekiri kwamba shambulio la anga la majeshi ya Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Kabul, wakati wa ziara ya waziri wa ulinzi wa Marekani Jim Mattis ulisababisha madhara kwa raia.
NATO wanasema kuwa kombora lilishindwa kulipuka,jambo wanalosema lilisababisha usumbufu mkubwa kwa watu wasio wanajeshi.
Serikali ya Afghanistan inasema kuwa mtu mmoja alikufa na wengine saba kujeruhiwa.Shambulio hilo lilifanyika katika kuwakabili washambuliaji wa kujitoa muhanga waliokuwa katika uwanja wa ndege wakiwa wamevalia vifaa vya kujilipua.