Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Watu 7 wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wahukumiwa kifo Somalia
Iliyochapishwa
Mahakama moja ya kijeshi eneo lililojitenga nchini Somalia la Puntland, imewahukumu washukiwa saba wa ugaidi kifo kwa kuwaua maafisa kadha wa vyeo vya juu wa eneo hilo, akiwemo mkurugenzi wa ikulu ya rais wa Puntland Aden Hurus.
Baadhi ya wanaume hao wanalaumiwa kwa kuwa wanachama wa mrengo wa al-Qaaeda wa kundi la al-Shabab, waliongea kwa sauti wakisema kuwa hawana hatia kabla ya kusomwa kwa hukumu na mahakama ya mji wa Basaso.
Wakili wao alisema atakata rufaa kupinga hukumu hiyo kwa sababa hakuna ushahidi wa kutosha kuwahukumu watu hao saba.