'Bruce Lee' achaguliwa kuwa diwani Afrika Kusini

Uchaguzi wa Afrika Kusini
Maelezo ya picha, Uchaguzi wa Afrika Kusini
Iliyochapishwa

Baada ya Vasco da Gama kuwa spika wa baraza la mji wa Johannesburg nchini Afrika Kusini,sasa Bruce Lee amechukua wadhfa katika baraza la mji wa Tshwane nchini humo.

Kwa wale waliokosa somo la historia ,Vasco da Gama alikuwa baharia maarufu ambaye amerikodiwa kuwa mtu wa kwanza kusafiri majini kutoka Ulaya hadi India kupitia Cape of Good Hope.

Na muda mfupi baadaye,orodha ya majina ya madiwani yaliotolewa huko Tshwane nchini humo humo yalionyesha 'Bruce Lee' akiwa katika wadhfa wa maendeleo ya kiuchumi katika baraza hilo.

Bruce Lee ni mcheza filamu kutoka nchini Marekani.