Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Tetesi za Soka Ulaya Alhamisi 15.02.2024
Wolves huenda wakamuuza Pedro Neto msimu huu wa joto ili kuhakikisha hawakiuki sheria za faida na uendelevu (PSR) na kumpa meneja Gary O'Neil pesa za kutumia kwingineko, huku Liverpool, Arsenal, Tottenham na Manchester United wakimwania Mreno huyo mwenye umri wa miaka 23. winga. (Sun)
Manchester United wanatarajia kufikia makubaliano na Newcastle ili kumteua Dan Ashworth kama mkurugenzi wa soka mapema wiki ijayo. (Mail)
Newcastle italipwa fidia ya zaidi ya pauni milioni sita ikiwa Ashworth atahamia Red Devils. (The I -Usajili unahitajika)
Manchester United wanatazamia kumnunua winga wa Crystal Palace mwenye umri wa miaka 22 Michael Olise, 22. (90min).
The Red Devils pia wanataka kumsajili beki wa Brazil Gleison Bremer, 26, kutoka Juventus msimu wa joto. (Calciomercato - kwa Kiitaliano)
Barcelona wamemuorodhesha kiungo wa kati wa Everton na Ubelgiji Amadou Onana mwenye umri wa miaka 22 kuwa mlengwa wao mkuu wa uhamisho wa majira ya joto. (Fichajes - kwa Kihispania)
Kocha wa zamani wa Brighton na Chelsea Graham Potter anapigiwa upatu kuchukua nafasi ya David Moyes iwapo ataondoka West Ham mwishoni mwa msimu huu. (Telegraph - usajili unahitajika)
Kiungo wa kati wa West Ham na Brazil Lucas Paqueta, 26, anafuatiliwa na Manchester City. (Football Insider)
Manchester City na Liverpool ni miongoni mwa klabu zinazopania kumnunua kiungo wa kati wa Shakhtar Donetsk na Ukraine Georgiy Sudakov, 21. (Calciomercato - kwa Kiitaliano).
Barcelona wanamfuatilia winga wa Uingereza Lauren Hemp huku kukiwa na sintofahamu kuhusu mustakabali wake, huku mkataba wake na Manchester City ukitarajiwa kumalizika msimu huu wa joto. (Standard)
Barcelona wameweka bei ya pauni milioni 85 kwa kiungo wa kati wa Uholanzi Frenkie de Jong, 26, ambaye anaendelea kuhusishwa na Manchester United na Chelsea. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)
Crystal Palace wamempanga meneja wa zamani wa Eintracht Frankfurt Oliver Glasner kuchukua mikoba iwapo watamtimua Roy Hodgson. (Guardian)
Everton na Crystal Palace wanamfuatilia mshambuliaji wa Marseille wa Senegal Iliman Ndiaye, 23. (La Provence via Sport Witness)
Chelsea imempa mkataba kocha mkuu wa Lyon, Sonia Bompastor kuchukua nafasi ya Emma Hayes, ambaye anaondoka mwishoni mwa msimu huu kwenda kuinoa timu ya taifa ya wanawake ya Marekani. (Athletic- Usajili unahitajika)
Imetafsiriwa na Ambia Hirsi