AU yakaribisha wito wa Tigray wa mazungumzo ya amani ya Ethiopia

Iliyochapishwa

 

Umoja wa Afrika umekaribisha tangazo la waasi wa Tigray  kaskazini mwa Ethiopia kwamba wako tayari kushiriki katika mazungumzo ya amani.

Mkuu wa Kamisheni ya AU, Moussa Faki Mahamat, alisema ni fursa ya kipekee kumaliza mzozo huo na kuwataka waasi na serikali ya Addis Ababa kutekeleza usitishaji vita mara moja.

Mapigano yalianza tena mwezi Agosti baada ya miezi kadhaa ya utulivu, lakini siku ya Jumapili uongozi wa Tigray  ulisema uko tayari kushiriki katika mchakato wa amani chini ya mwamvuli wa Umoja wa Afrika.

Viongozi wa Tigray  hapo awali wamekuwa wakikosoa upatanishi unaoongozwa na AU, badala yake walimpendelea Rais wa Kenya anayeondoka Uhuru Kenyatta kuongoza mazungumzo hayo.

Hakujawa na majibu ya moja kwa moja kutoka kwa serikali ya Ethiopia lakini hapo awali imesema ingezungumza wakati wowote, mahali popote.