Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 02.01.2024

Iliyochapishwa

Liverpool na Real Madrid wanamtaka mshambuliaji wa Paris St-Germain, Kylian Mbappe, ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 25 yuko huru kusaini klabu nyingine mwezi huu. (Le Parisian)

Paris St-Germain wanawania saini ya kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 27, kutoka Manchester City mwezi huu. (Telegraph)

Manchester United na Liverpool wanaongoza mlolongo wa vilabu vinavyomtaka kiungo wa kati wa Ujerumani Joshua Kimmich, 28, mkataba wake na Bayern Munich utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu. (AS)

Liverpool na Tottenham wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Wolves na Korea Kusini, 27, Hwang Hee-Chan. (Football Insider)

West Ham wamewasiliana na Tottenham kuhusu kumnunua beki wa Uingereza, Eric Dier, ambaye yuko nje ya uwanja tangu kuwasili Ange Postecoglou. (Football Transfers)

Manchester City ni miongoni mwa timu inayomfuatilia mlinzi Leny Yoro mwenye umri wa miaka 18, huku Lille ikitaka pauni milioni 78. (Manchester Evening News)

Winga wa Morocco, Hakim Ziyech 30, anaweza kurejea Chelsea mwezi huu kwani Galatasaray inapanga kusitisha uhamisho wake wa mkopo wa msimu mzima. (NTV Spor)

Liverpool wanamfuatilia kiungo wa kati wa Genoa raia wa Denmark, Morten Frendrup, 22, lakini uhamisho wa mwezi Januari huenda usifanikiwe. (Liverpool Echo)

Nottingham Forest imeanza mazungumzo na Paris St-Germain kuhusu kumsajili tena kipa wa Costa Rica Keylor Navas, 37, ambaye alitumia nusu ya pili ya msimu uliopita kwa mkopo kwenye Uwanja wa City Ground. (Football Insider)

Newcastle United inamtaka mlinzi wa Chelsea mwenye umri wa miaka 19 Mbrazil, Andrey Santos, ambaye usajili wake kwa mkopo huko Nottingham Forest unatarajiwa kusitishwa mwezi huu. (Football 365)

Winga wa Burnley, Manuel Benson, 26, yuko kwenye mazungumzo na Hull City baada ya vilabu hivyo kukubaliana kwa mdomo mkataba wa mkopo hadi mwisho wa msimu. (Hull Daily Mail)

Fulham wameongeza mkataba wa mwaka mmoja kwa nahodha wa klabu na kiungo wa kati wa Scotland Tom Cairney, 32, baada ya kiwango chake cha hivi karibuni kuwa kizuri. (Sun)

Chelsea wameanza mchakato wa kumsajili beki wa Nice na Ufaransa, Jean-Clair Todibo, 24, ambaye pia anawindwa na Manchester United na Tottenham. (Teamtalk)

Chelsea wanamtaka mshindi wa Kombe la Dunia la vijana chini ya umri wa miaka 17 wa Ujerumani, David Odogu na mlinzi wa Wolfsburg mwenye umri wa miaka 17, ambaye hajacheza katika ligi ya Bundesliga. Pia anawindwa na Leicester City. (Sun)

Mshambulizi wa zamani wa Arsenal, Carlos Vela, 34, anaweza kurejea Real Sociedad kwa mkataba wa muda mfupi. Mchezaji huyo wa Mexico pia anawindwa na Cruz Azul baada ya mkataba wake na Los Angeles FC kumalizika. (AS Diario)

Imetafsiriwa na Rashid Abdallah