Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Muislamu kutengeza majeneza ya wakristo? Nilitengwa!
Tatizo la ajira nchini Tanzania, limewasukuma baadhi ya vijana kujiingiza katika biashara ambazo zinaonekana kukinzana na imani za kidini, mila pamoja na desturi zao.
Atwai Mwinyi Mkaga ni kijana aliyejiingiza katika utoaji wa huduma za kutengeza majeneza na hivyo kutokana na imani yake ya dini ya kiislamu, alijikuta akiwa na wakati mgumu ikiwemo kutengwa na familia yake ambayo awali haikufurahishwa na biashara ya kutengeza majeneza kwa waktristo.
Atwai maarufu kwa jina la Mwinyi katika hospitali ya Mt. Meru jijini Arusha, anamsimulia mwandishi wa BBC Aboubakar Famau jinsi alivyopambana kubadilisha dhana hiyo katika jamii yake.