Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Buibui hatari na anayeogopeka zaidi aonekana Uingereza
Buibui hatari zaidi ameonekana kwa mara kwanza Uingereza.
Buibui huyu yuko kwenye orodha ya wadudu hatari zaidi na wanaogopwa nchini Uingereza.
Buibui wa aina hiyo ameonekana katika maeneo matatu pekee, huko Dorset na Surrey, na hawajawahi kuonekana tangu mwanzoni mwa mwaka 1990.
Mike Waite, ambaye alimgundua buibui huyo kupitia mafunzo ya wizara ya ulinzi katika eneo la Surrey, alisema alikuwa na furaha isiyo na kifani kwa ugunduzi wake huo.
Mtafiti huyo alipata buibui ambao walikuwa hawajakuwa, baada ya kuwatafuta kwa kipindi cha miaka miwili.
Buibui huyo hatari, 'Alopecosa fabrilis',anaishi ardhini na anaonekana zaidi usiku.
Ni miongoni mwa buibui wakubwa zaidi katika jamii ya buibui.
Kwa mujibu wa taasisi ya wanyama pori ya Surrey Wildlife Trust, wamesifia kugunduliwa kwa buibui huyo wa ajabu mwenye macho meusi nane.
Bwana Waite, kutoka taasisi ya Surrey Wildlife Trust, alisema: "Nimeshagazwa sana kuona kuwa buibui huyu hatari bado yupo Uingereza.
"Ingawa nmekuwa nafuatilia sana juu ya buibui, Nnajivunia kwa kutoa mchango huu muhimu kwa wanaayansi.