Msemaji wa wapiganaji wa Hamas amesema wataanza kuwaua mateka
wanaowashikilia katika Ukanda wa Gaza iwapo Israel itaendelea kulipua makazi ya
raia.
Waziri wa mambo ya nje wa Israel amethibitisha zaidi ya watu mia moja
walichukuliwa mateka.
Kundi hilo la wapiganaji wa Kiislamu
ya lilitishia kumuua mateka wa Israel kila mara
Israel inaposhambulia kwa mabomu nyumba ya Wapalestina bila ya onyo, huku
Israel ikiwaita askari wa akiba 300,000 ambao hawakuwahi kushuhudiwa na kuweka
vizuizi katika Ukanda wa Gaza, na kuzusha hofu ilipanga shambulio la ardhini.
Ghasia hizo, ambazo zimegharimu maisha ya zaidi ya watu 1,500, zimesababisha
miito ya kimataifa ya kuiunga mkono Israel baada ya shambulio baya la mwishoni
mwa juma lililofanywa na Hamas, na kuomba kukomeshwa kwa mapigano na ulinzi wa
raia.
Taarifa kadhaa za televisheni za Israel zilisema idadi ya vifo kutokana na
shambulio la Hamas imepanda hadi Waisraeli 900, huku takriban 2,600
wakijeruhiwa, na makumi kadhaa wakichukuliwa mateka.
Miongoni mwa waliouawa Israel ni 260 wengi wao wakiwa vijana waliopigwa
risasi kwenye tamasha la muziki wa jangwani, ambapo baadhi ya mateka walitekwa
nyara.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aliapa kulipiza kisasi katika
hotuba yake kali akiwashutumu Hamas kwa kuwanyonga watoto waliokuwa wamefungwa
na ukatili mwingine. "Adui huyu mbaya alitaka
vita na atapata vita," alisema.
-
Mohammed Deif: Mfahamu kiongozi wa Hamas anayewanyima usingizi Israel
-
Masuala muhimu unayopaswa kujua kuhusu mzozo kati ya Israel na Palestina
-
Je, ni nini kilichotokea 1967 wakati israel ilipokabiliana kijeshi na mataifa matatu ya kiarabu katika vita vya siku sita?
-
Fahamu chanzo cha uhasama kati ya Israel na Palestina
-
Tunachojua kufikia sasa kuhusu raia wa Israel waliotekwa na Hamas