Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.

Bofya kuelekea tovuti kuu

Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data

Matokeo ya uchaguzi wa Marekani 2020: Biden aongoza Pennsylvania na Georgia kwa mara ya kwanza

Mgombea wa chama cha Democratic katika uchaguzi wa urais wa Marekani Joe Biden amechukua uongozi wa jimbo hilo kwa mara ya kwanza.

Moja kwa moja

Asha Juma

  1. Habari za hivi punde, Jimbo la Georgia kurudia hesabu ya kura za urais

    Waziri wa masuala ya kigeni katika jimbo la Georgia Brad Raffensberger ametangaza kwamba jimbo hilo litahesabu upya kura zake za urais.

    Anasema kwamba kura 4169 hazijahesabiwa na kwamba kura 8000 za wanajeshi bado zimo katika barua na kwamba sitahesabiwa zitakapowasili mwisho wa siku.

  2. Joe Biden achukua uongozi wa jimbo la Pennsylvania

    Sio muda mrefu sasa, usiku kucha , Joe Biden amempiku Donald Trump katika mji wa Georgia .

    Na huku matokeo ya kura yakitolewa, Biden amechukua uongozi dhidi ya Trump katika jimbo la Pennsylvania.

    Georgia yenye wajumbe 16 inatosha kumfanya Biden kupata matokeo sawa na Trump katika idadi ya wajumbe, huku akisubiri matokeo maengine kutoka majimbo mengine.

    Pennsylvania itamfanya Biden kuingia katika Ikulu ya Whitehouse.

  3. habari zetu mubashara zinaendelea

  4. Matokeo ya uchaguzi wa Marekani 2020:Itakuwaje ikiwa wagombea urais watapata kura sawa za wajumbe?

    Kura za wajumbe zikiwa 538 ni nadra sana wagombea kupata kura sawa yaani 269.

    Hata hivyo ni jambo linaloweza kutokea.

    Ikiwa ni iwe hivyo, Donald Trump atahitajika kushinda katika majimbo ya Arizona, North Carolina, Nevada na Pennsylvania, lakini ashindwe katika jimbo la Georgia.

    Ikiwa hivyo, kipi kitatokea?

    Ikiwa hakuna mgombea kati yao aliyepata wingi wa kura za wajumbe, Bunge ndio litakaloamua.

    Bunge la wawakilishi litapiga kura kuamua nani atakuwa rais, huku kila wabunge wa jimbo wakiwa na kura moja.

    Ili kupata wingi wa kura, mgombea atahitajika kupata kura 26.

    Naibu rais atachaguliwa na bunge la Seneti huku maseneta wote 100 wakihitajika kupiga kura.

    Wabunge waliochaguliwa katika uchaguzi wa 2020 ndio watakaoshiriki mchakato huo – lakini hadi kufikia sasa kuna baadhi ya majimbo ambayo hayajamaliza kupiga kura.

    Maelezo zaidi:

  5. Matokeo ya uchaguzi wa Marekani 2020: Vichwa vya habari Duniani vyajikita katika ‘vurugu za Marekani’

    Marekani bado shughuli ya kuhesabu kura inaendelea, lakini vyombo vya habari vya dunia vinaangazia hatua za kisheria zilizochukuliwa na Donald Trump na kuendeleza mjadala wa vurugu zinazokumba shughuli ya kuhesabu kura.

    Tuanze na nchini Kenya ambapo gazeti la The Standard kichwa chake cha habari kinasoma "Vurugu hadi mwisho".

    Gazeti la Punch nchini Nigeria liliangazia taarifa yenye kichwa "wasiwasi na mvutano" Marekani.

    Gazeti la China la Global Times limesema kura zinazoendelea kuhesabiwa zimesababisha "mgawanyiko, ghasia na machungu makali" nchini Marekani. China, inasema uchaguzi huo umekuwa kama "burudani", "jamii iliyokumbwa na ghasia", gazeti hilo limeongeza.

    Kwengineko shirika la habari la Iran limeangazia ghasia zilizotokea mitaani wakati shughuli ya kuhesabu kura inaendelea katika majimbo kadhaa. Radio Iran (VIRI) imesema "Sintofahamu iliyokumba matokeo nchini Marekani, huku ghasia za uchaguzi zikiongezeka".

    Nchini Urusi, uchaguzi wa Marekani haukuwa tena gumzo badala yake vituo vyote vilijikita katika matamshi ya Trump ya wizi wa kura bila kutaja ushahidi wowote.

    Na gazeti la Corriere della Sera nchini Italia limesema uchaguzi wa mwaka huu ni "mtihani mkubwa sana kwa demokrasia”, na unaoonesha "uimara na udhaifu wa mfumo wao wa upigaji kura" Marekani.

    Pia unaweza kusoma:

  6. Habari za hivi punde, Matokeo ya uchaguzi wa Marekani 2020:Biden anaongoza Georgia kwa mara ya kwanza

    Georgia, moja ya majimbo muhimu ambapo kura bado zinaendelea kuhesabiwa, wanaofuatilia uchaguzi kwa karibu pamoja na chombo cha habari cha CNN kimesema kwamba mgombea wa Democrat Joe Biden amechukua uongozi wa jimbo hilo kwa mara ya kwanza.

    Biden anaongoza kwa kura kidogo huku ikisemekana kwamba asilimia 99 ya kura tayari zimehesabiwa.

    Aidha, vyombo vya habari vya eneo pia vinaonesha kwamba Biden yuko mbele ya Donald Trump kwa zaidi ya kura 900 kulingana na kura zinazohesabiwa katika kituo cha kaunti ya Clayton.

    Bwana Trump hana njia mbili zaidi ya kupata ushindi wa jimbo la Georgia ili aweze kubaki na mwanya wa kupata ushindi.

    Kulingana na data ya hivi karibuni Bwana Biden anaongoza huku kura nyingi zikiwa zimeshahesabiwa.

    Jimbo la Georgia lina kura za wajumbe 16 , na kushinda jimbo hilo kutafanya Bwana Biden kusalia na kura moja pekee ya kumuwezesha kufikia kura 270 za wajumbe zinazohitajika ili aweze kupata ushindi.

    Ikiwa Bwana Trump atashindwa kupata ushindi wa jimbo la Georgia, kura za wajumbe ambazo anaweza kupata itakuwa ni 269 ikimaanisha kwamba hatakuwa amefikisha idadi ya kura zinazohitajika.

    Malezo zaidi:

  7. Watani wa jadi Yanga na Simba kumaliza ubishi kesho

      • Author, Eagan Salla
      • Nafasi, BBC Swahili, Dar es Salaam

    Ni mchezo unaovuta hisia za mashabiki wengi wa soka Tanzania na kwingineko duniani kutokana na ukubwa wa vilabu hivi viwili nchini Tanzania.

    Wawili hao wamekuwa wakitambiana kila mmoja akijivunia ubora wa kikosi chake msimu huu mara ya mwisho simba ili iliigaragaza Yanga 4 – 1 kwenye mchezo wa nusu fainali wa kombe la ligi (Azam Federation Cup).

    Mara hii Yanga ikiwa chini ya kocha Mrundi Cedric Kaze watakuwa nyumbani kwenye dimba la Mkapa jijini Dar es salaam kuiakaribisha Simba inayonolewa na kocha Mbelgiji Sven Vandenbroeck.

    Kaze ameshaiongoza Yanga kwenye michezo minne na kati yake ameshinda mitatu na kutoa suluhu mmoja huku Scven yeye amekuwa na Simba toka msimu uliopita.

    Yanga wamezoeleka kucheza mpira ya pasi ndefu na kasi huku Simba wao wakipiga pasi nyingi mpaka golini, kwenye mchezo wa kesho Yanga wanaingia wakivunia kuwa na ukuta imara zaidi wakiwa hawajafungwa mchezo hata mmoja msimu huu huku wakiwa wameruhusu magoli mawili tu.

    Simba wao wanaingia kifua mbele wakiwa na safu imara zaidi ya ushambuliaji wakiwa wameshajikisanyia jumla ya magoli 21 mpaka sasa huku watani wao wakiwa na magoli 11 tu.

    Mchezo wa kesho utachezeshwa na waamuzi sita wawili wakiwa nyuma ya magoli, mtendaji mkuu wa bodi ya ligi Almasi Kasongo alitangaza azma hiyo kutokana na kuwepo kwa malalamiko ya mara kwa mara kutokana na makosa yanayofanya na waamuzi kwenye micheozo ya ligi kuu.

  8. Matokeo ya uchaguzi wa Marekani 2020:Kwanini baadhi ya Republicans wangefurahi kumuona Trump akipoteza Urais?

    Profesa wa somo la Sheria katika Chuo Kikuu cha Southampton, Jacob Eisler, ameiambia BBC Radio 5 Live kwamba kesi zilizowasilishwa na kampeni ya Trump ni "dhaifu".

    Aliongeza kuwa ana wasiwasi kwamba Trump huenda akang'ang'ania madarakani.

    "Kile kinamshinikiza kufanya hivyo [Trump] ni maslahi yake binafsi," amesema.

    "Trump, ana fursa ya kukabiliana na mtihani huu huku akiendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika chama cha Republican."

    Pia unaweza kusoma:

  9. Matokeo ya uchaguzi Marekani 2020:'Usalama waimarishwa' kwa Biden

    Usalama umeimarishwa kwa Joe Biden kuanzia Ijumaa wakati inatarajiwa kuwa huenda akatangazwa kuwa mshindi, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na gazeti la Washington.

    Bwana Biden ataongezewa idadi ya maafisa wa usalama baada ya timu yake ya kampeni kuiambia idara husika kwamba anaweza akatoa hotuba muhimu Ijumaa, gazeti hilo limeandika kwa kunukuu watu wenye ufahamu wa mipango hiyo.

    Bwana Biden na timu yake ya kampeni wamekuwa katika kituo cha Wilmington, Delaware.

    Maelezo zaidi:

  10. Matokeo ya uchaguzi Marekani 2020: Polisi yachunguza njama za kuvamiwa kwa kituo cha kuhesabiwa kura cha Philadelphia

    Polisi huko Philadelphia inachunguza njama ya kuvamia kituo kikuu cha kuhesabu kura cha Pennsylvania, ambako kura zinahesabiwa.

    Shirika la utangazaji la ABC News limesema kundi la watu – ambalo huenda likawa familia – lilikuwa kuvamia kituo hicho kutoka Virginia kwa kutumia gari aina ya Hummer SUV kutekeleza shambulio hilo.

    Polisi wameshika gari hilo na kumkamata mwanaume mmoja, taarifa hiyo inasema.

    Philadelphia sasa hivi ni moja ya miji michache inayofuatiliwa kwa karibu katika kinyang’anyiro cha kuingia Ikulu.

    Wakati shughuli ya kuhesabu kura inaendelea, kura zile alizopata Trump katika jimbo hilo ambazo zilionesha anaongoza kwa kura nyingi zaidi zinazidi kupungua hatua ambayo imefanya timu ya kampeni yake kutaka shughuli ya kuhesabu kura kusitishwa.

    Hata hivyo, licha ya rais kuchukua hatua za kisheria akitaka shughuli ya kuhesabu kura kusitishwa, kwa kukosa imani na matumaini dhidi ya wafuasi wa Joe Biden katika jimbo hilo imekuwa ambao wameanza hata kusherehekea nje ya kituo kikuu cha kuhesabu kura.

    Maelezo zaidi:

  11. Diamond Platnumz akutana na watoto wake kwa mara ya kwanza tangu 2018

    Mwanamuziki maarufu nchini Tanzania Diamond Platnumz hatimaye amekutana na watoto wake kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2018.

    Aliyekuwa mke wake Zari aliwasili Tanzania Alhamisi usiku pamoja na watoto wao Tiffah na Nillan.

    Picha za Video zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zinamuonesha Diamond Platnumz akiwalaki watoto wake wawili.

    Baada ya watoto hao kupokelewa, mmoja aliulizwa na wanahabari "umemletea nini baba na bibi yako?" na kujibu ‘’Pizza’’.

  12. Matokeo ya uchaguzi Marekani 2020: Usalama waimarishwa katika kituo cha kuhesabu kura Nevada

    '“Hatutamruhusu yeyote kutuzuia kutekeleza jukumu letu la kuhesabu kura,” hayo ni maneno ya Joe Gloria, msajili wa eneo la Clark huko Nevada, amewaambia wanahabari.

    Amesema maafisa wa usalama wamepelekwa eneo hilo huku hatua zingine za kiusalama zikichukuliwa kuhakikisha wafanyakazi wako salama kuendelea na shughuli ya uhesabuji wa kura.

    Lakini pia ameongeza kuwa masanduku ya mwisho ya kura yanayotarajiwa kuwasilishwa baadae huenda matokeo yakatolewa wiki ijayo kabla ya matokeo kamili kufahamika.

    Joe Biden sasa hivi anaongoza kwa kura kidogo huko Nevada, na kampeni ya Trump imetishia kuwasilisha kesi ya madai ya udanganyifu mahakamani ingawa hadi kufikia sasa hakuna ushahidi wowote uliotolewa.

    Akijibu madai ya udanganyifu wa kura, Bwana Gloria alisema: "Hatufahamu lolote kuhusu uhesabu wa kura zisizostahili."

    Maelezo zaidi:

  13. Hujambo na karibu katika matangazo yetu ya moja kwa moja hii leo ikiwa ni tarehe 6/11/2020.